Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 11:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Furaha yake itakuwa kumutii Yawe. Hatatoa hukumu kulingana na yale anayoona, wala kuamua kufuatana na yale anayosikia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 11:3
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Nami mujakazi wako nilifikiri hivi: ‘Neno la bwana wangu mufalme litanipa amani ndani ya moyo, maana wewe bwana wangu mufalme ni kama malaika wa Mungu katika kupambanua mazuri na mabaya.’ Yawe, Mungu wako, akuwe pamoja nawe.”


Mufalme akamwambia yule mwanamuke: “Rudi kwako nitaamuru jambo lako liangaliwe.”


Watu wote wa Israeli waliposikia juu ya hukumu ya mufalme, walimwogopa. Wakatambua kwamba alikuwa na hekima ya Mungu iliyomuwezesha kutoa hukumu za haki.


Kwa hiyo, ninakuomba unipe mimi mutumishi wako moyo wa hekima nipate kuamua watu wako, niweze kutambua mazuri na mabaya; maana ni nani anayeweza kuhukumu watu wako wanaokuwa wengi hivi?”


Sikio halipimi maneno kama vile ulimi unavyoonja chakula?


Sikio linapima maneno, kama vile ulimi unavyoonja chakula.


utaelewa maana ya kumwogopa Yawe, utafahamu maana ya kumujua Mungu.


Ukinisikiliza, utafahamu haki, usawa, na kufuata sheria ya Mungu; utafahamu kila njia nzuri.


Enyi watu wa Yerusalema, Yawe atawajalia usalama, atawaokoa na kuwapa hekima na maarifa. Akiba yenu kubwa ni kumwogopa Yawe.


Huo ndio urizi wa mufalme katika Israeli. Hivyo mufalme hatawatesa watu wangu, lakini ataacha inchi igawanywe kwa Waisraeli kulingana na makabila ya Israeli.


Mungu atatoa hukumu kati ya mataifa mengi, atakata mashauri ya mataifa makubwa ya mbali. Nayo yatafua mapanga yao kuwa majembe, na mikuki yao kuwa visu vya kuvuna. Taifa halitapigana na taifa lingine, wala hayatafanya tena mazoezi ya vita.


Na Yesu alizidi kuwa na hekima, na kuongezeka kimo na kuendelea kumupendeza Mungu na watu.


Naye hakuhitaji kupewa ushuhuda juu ya mutu yeyote, kwa maana yeye mwenyewe alijua yanayokuwa ndani ya mioyo ya watu.


Muache kuhukumu kufuatana na hali ya inje, lakini muhukumu kwa haki.”


Lakini chakula kigumu ni kwa ajili ya watu wazima, ndio wale waliozoeza mafikiri yao hata wapate kutambua mema na mabaya.


Lakini Yawe alimwambia: “Usiangalie sura yake wala urefu wake. Mimi nimemukataa maana siangalii mambo kama vile wanadamu wenye kufa wanavyoangalia. Mwanadamu anaangalia umbo la inje, lakini mimi ninaangalia ndani ya moyo.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ