Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 11:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kutatokea chipukizi katika shina la Yese, tawi litachipuka toka mizizi yake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 11:1
26 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mungu wa Israeli amesema, Yeye Jiwe la Kufichamia la Israeli ameniambia: Mutu anayetawala watu kwa haki, anayewatawala akimwogopa Mungu,


Watasema juu ya utukufu wa ufalme wako, na kutangaza juu ya nguvu yako kubwa,


Siku ile chipukizi wa Yese atakuwa kitambulisho kwa mataifa; mataifa yatamutafuta na makao yake yatatukuka.


Siku ile, tawi Yawe atakalochipuza litakuwa zuri na tukufu, nayo matunda ya inchi yatakuwa na heshima na utukufu kwa wale Waisraeli watakaobaki. Waisraeli watakaobaki watasifiwa na kujivunia mazao ya inchi yao.


Maana, mbele ya Yawe, mutumishi wake alikomaa kama kichipukizi, kama muzizi katika inchi kavu. Hakukuwa na umbo wala sura ya kupendeza, wala hakukuwa na uzuri wowote wa kutuvuta.


Hata kukibaki sehemu moja ya kumi ya watu, nao vilevile watateketezwa. Hao watakuwa kama muti wa muvinje au wa mwalo ambao shina lake limebaki kisha kukatwa. Shina hilo ni mbegu takatifu ya mwanzo mupya.


Utawala wake utastawi siku zote, amani ya ufalme wake haitakoma. Atakamata madaraka ya mufalme Daudi na kutawala juu ya ufalme wake; ataustawisha na kuuimarisha kwa kufuata sheria ya Mungu na kutenda kwa haki tangu sasa na hata milele. Yawe wa majeshi atafanya mambo hayo.


Yawe ametoa neno juu ya Yakobo nalo litamupata Israeli.


Siku zinakuja ambapo nitaotesha kichipukizi cha haki toka kizazi cha Daudi. Huyo atatawala kama mufalme, atatenda kwa hekima naye ataimarisha sheria yangu na haki katika inchi.


Katika siku hizo, katika wakati huo, nitaotesha chipukizi wa haki wa uzao wa Daudi. Chipukizi huyo ataimarisha sheria yangu na haki katika inchi.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi mwenyewe nitatwaa kichipukizi cha incha ya juu ya muti wa mwerezi. Nitavunja tawi changa kutoka matawi yake ya juu na kulipanda juu ya mulima murefu sana.


Watakaa katika inchi ya wazee wao ambayo nilimupa Yakobo. Wao na watoto wao na wajukuu wao wataishi humo milele. Naye Daudi, mutumishi wangu, atakuwa mutawala milele.


Hivyo Mungu atawaachilia watu wake kwa waadui, mpaka yule mwanamuke mwenye kuwa na mimba atakapozaa. Kisha wandugu zake waliobakia, watarudi na kuungana na Waisraeli wenzao.


Sasa sikiliza kwa uangalifu, ewe Yoshua, Kuhani Mukubwa; musikilize vilevile enyi makuhani wenzake munaokuwa pamoja naye, ninyi munaokuwa kitambulisho cha wakati muzuri unaokuja: Nitamuleta mutumishi wangu anayeitwa Tawi.


na kumwambia kwamba Yawe wa majeshi anasema hivi: Hapa kuna mutu anayeitwa Tawi. Yeye atastawi pale anapokuwa na kulijenga hekalu la Yawe.


Haya ni majina ya babu za Yesu Kristo, wa uzao wa Daudi, wa uzao wa Abrahamu. Abrahamu alizaa Isaka, Isaka alizaa Yakobo, Yakobo alizaa Yuda na wandugu zake, Yuda alizaa Peresi na Zera kutoka muke wake Tamari, Peresi alizaa Hesironi, Hesironi alizaa Ramu, Ramu alizaa Aminadabu, Aminadabu alizaa Nasoni, Nasoni alizaa Salmoni, Salmoni alizaa Boazi kutoka muke wake Rahaba, Boazi alizaa Obedi kutoka muke wake Ruta, Obedi alizaa Yese, Yese alizaa mufalme Daudi, Daudi alizaa Solomono (mama yake ndiye yule aliyekuwa muke wa marehemu Uria), Solomono alizaa Rehoboamu, Rehoboamu alizaa Abiya, Abiya alizaa Asa, Asa alizaa Yosafati, Yosafati alizaa Yoramu, Yoramu alizaa Uzia, Uzia alizaa Yotamu, Yotamu alizaa Ahazi, Ahazi alizaa Hezekia, Hezekia alizaa Manase, Manase alizaa Amoni, Amoni alizaa Yosia, Yosia alizaa Yekonia na wandugu zake, wakati Waisraeli walipohamishwa kwenda Babeli. Nyuma ya kuhamishwa kwa Waisraeli kwenda Babeli, Yekonia alizaa Saltieli, Saltieli alizaa Zerubabeli, Zerubabeli alizaa Abihudi, Abihudi alizaa Eliakimu, Eliakimu alizaa Azoro, Azoro alizaa Zadoki, Zadoki alizaa Akimu, Akimu alizaa Elihudi, Elihudi alizaa Eleazari, Eleazari alizaa Matani, Matani alizaa Yakobo, Yakobo alizaa Yosefu, yule alikuwa mume wa Maria, mama ya Yesu, anayeitwa Kristo.


Isaya naye anasema: “Muzao wa Yese atatokea, atatawala watu wa mataifa, nao watamutumainia.”


Kwa maana inajulikana wazi kwamba Bwana wetu alitoka katika kabila la Yuda, na juu ya kabila lile Musa hakusema hata neno moja linaloelekea ukuhani.


“Mimi Yesu, nimemutuma malaika wangu kwa kuwashuhudia maneno haya yote katika kanisa. Mimi ni wa shina na wa uzao wa mufalme Daudi. Mimi ni nyota ya asubui.”


Basi mumoja kati ya wale wazee akaniambia: “Usilie. Angalia, simba wa kabila la Yuda, wa uzao wa mufalme Daudi, amepata ushindi. Yeye anaweza kuvunja vile vifundo saba vya muhuri vya kizingo na kukifungua.”


Wanawake wajirani wakatangaza jina wakisema: “Mutoto amezaliwa kwa Naomi”, nao wakamwita jina la Obedi. Kisha Obedi akamuzaa Yese aliyemuzaa Daudi.


Saulo akamwuliza Daudi: “Kijana, wewe ni mwana wa nani?” Daudi akajibu: “Mimi ni mwana wa mutumishi wako Yese, kutoka muji wa Betelehemu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ