Hata kama munategemea Misri kupata magari ya vita na waaskari wapanda-farasi, hamuwezi kumurudisha nyuma mutu mumoja wa cheo cha chini sana kati ya watumishi wa bwana wangu.
Anayetaka kujivuna, ajivune kwamba ananifahamu mimi, kwamba anajua kwamba mimi Yawe ninatenda mema, ninafanya mambo ya haki kufuatana na sheria yangu katika dunia. Watu wa namna hiyo ndio wanaonipendeza. –Ni ujumbe wa Yawe.
Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kutoka upande wa kaskazini nitamuleta Nebukadneza, mufalme wa Babeli, mufalme wa wafalme, akiwa na farasi, magari ya vita, waaskari wapanda-farasi na kundi kubwa, akuje kukushambulia.