Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 10:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Nilimutuma kuliazibu taifa ovu, nilimwamuru kuwaazibu watu niliowakasirikia, kuwanyanganya na kuteka vitu vyao, na kuwakanyaga chini kama matope katika njia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 10:6
38 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Niliwatwanga, wakakuwa kama mavumbi, nikawaponda na kuwakanyaga kama matope katika barabara.


Zaidi ya hayo, munafikiri nimekuja bila amri ya Yawe kwa kuishambulia na kuiangamiza inchi hii? Yawe ndiye aliyeniambia: Uishambulie inchi hii na kuiangamiza!”


Yuda atakuwa kitisho kikubwa kwa Wamisri. Wote watakaoambiwa habari za Yuda wataingiwa na woga kwa sababu ya jambo Yawe wa majeshi aliloamua kuwatendea.


Maana leo Yawe wa majeshi ametuletea fujo, kushindwa na wasiwasi katika Bonde la Maono. Kuta za muji zimebomolewa. Kilio cha wakaaji wake kinasikilika mpaka kwenye milima.


Watu wameichafua dunia maana wamezivunja sheria za Mungu, wamegeuka mbali na masharti yake, wamelivunja agano lake la milele.


Bwana anasema: Watu hawa wanakuja kuniabudu kwa maneno tu, lakini mioyo yao iko mbali nami. Wananiheshimu kulingana na desturi ya watu tu, jambo walilojifunza wao wenyewe.


Wapumbafu wanasema maneno ya upumbafu, na mafikiri yao ni kutenda maovu, kutenda mambo ya watu wasiomujua Mungu, kusema maneno ya kumutukana Yawe. Wanawaacha wenye njaa bila chakula, na wenye kiu wanawanyima kinywaji.


Ole kwako! Unaangamiza ingawa hauangamizwi. Unadanganya ingawa haudanganywi. Utakapokwisha kuangamiza, wewe utaangamizwa! Utakapomaliza kudanganya, wewe utadanganywa.


Wenye zambi katika Sayuni wanaogopa, wasiomwamini Mungu wanatetemeka na kusema: Nani anayeweza kuvumilia moto huu mukali? Nani anayeweza kuvumilia ndimi za moto usiozimika?


Nimetokeza mutu toka kaskazini, naye amekuja; nimemuchagua mutu toka mashariki, naye atalitaja jina langu. Yeye atawakanyaga wafalme kama matope, kama vile mufinyanzi anavyoponda udongo wake.


Watakaokujenga upya wanakuja haraka, wale waliokuharibu wanaondoka.


Yawe anasema hivi: Kweli! Hata mateka za shujaa zitarudishwa, wafungwa wa mutu mutesaji wataokolewa. Mimi mwenyewe nitawapiganisha waadui zako, mimi mwenyewe nitawaokoa watoto wako.


Kwa hiyo hasira ya Yawe iliwawakia watu wake, akaunyoosha mukono wake juu yao, akawaazibu. Milima ikatetemeka, maiti zao zikakuwa kama takataka katika barabara za muji. Hata hivyo, hasira yake haijatulia, angali ananyoosha mukono wake kwa kuwaazibu.


Waaskari wao wananguruma kama simba; wananguruma kama simba wakali ambao wamekamata nyama wao na kuwapeleka mbali ambapo hakuna anayeweza kuwanyanganya.


Na sasa nitawaambia jinsi nitakavyolifanya hilo shamba langu. Nitaubomoa upango wake, nalo litaharibiwa. Nitaubomoa ukuta wake, nalo litakanyagwakanyagwa.


Kweli, nimekamua mizabibu peke yangu, wala hakuna mutu aliyekuja kunisaidia. Nimeyakanyaga mataifa kwa hasira yangu, niliyapondaponda kwa kasirani yangu. Nguo zangu zimejaa madoa ya damu yao, imechafua kabisa nguo yangu.


Kwa hasira yangu niliwaponda watu, niliwalewesha kwa kasirani yangu; damu yao niliimwanga chini.


Yawe atakuletea wewe pamoja na watu wako na jamaa yote ya kifalme siku za taabu kuliko zile zote zilizotokea tangu wakati watu wa Efuraimu walipojitenga na watu wa Yuda; ni kusema, atawaletea ninyi mufalme wa Asuria.


Maana mbele mutoto huyu hajafikia umri wa kuweza kutamka neno “Baba” au “Mama”, utajiri wa muji wa Damasiki na vitu walivyonyanganya kule Samaria vitapelekwa kwa mufalme wa Asuria.


Utaingia ndani ya inchi ya Yuda kwa nguvu na kufurika na kupanda mpaka kwenye shingo. Utaenea juu ya inchi yako yote, ee Emanueli!


Uovu unawaka kama moto unaoteketeza michongoma na miiba; unawaka kama moto katika pori, na kutoa moshi muzito unaopanda juu katika anga.


wananyanganya upande mumoja na hawatosheki; wanakula upande mwingine lakini hawashibi. Kila mumoja anamushambulia mwenzake.


basi, nitayaita makabila yote ya kaskazini pamoja na mutumishi wangu Nebukadneza, mufalme wa Babeli. –Ni ujumbe wa Yawe.– Nitawaleta waishambulie inchi hii na wakaaji wake pamoja na mataifa yote jirani. Nitawaangamiza kabisa, na kuwafanya kuwa kitu cha kuchukiza, cha kuzomewa na kuzarauliwa milele.


Pamoja na hayo yote, Yuda, dada mudanganyifu wa Israeli hakunirudilia kwa moyo wote, lakini kwa unafiki tu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Nitawaamuru nao wataurudia katika muji huu. Wataushambulia, watauteka na kuuteketeza kwa moto. Nitaifanya miji ya inchi ya Yuda kuwa ukiwa bila wakaaji. –Ni ujumbe wa Yawe.


Wewe Yerusalema, usafishe maovu ya moyo wako, kusudi upate kuokolewa. Mpaka wakati gani utaendelea kuchunga maovu?


Nimemupa inchi ya Misri kuwa mushahara wa jasho lake kwa maana waaskari wake walifanya kazi kwa ajili yangu. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Utanyanganya na kuteka mali za watu wanaokaa katika miji ambayo ilikuwa jangwa. Watu hao wamekusanywa kutoka katika mataifa na sasa wana makundi ya nyama na mali; nao wanakaa kwenye kitofu cha dunia.


Wakaaji wa Seba na Dedani pamoja na wachuuzi wa Tarsisi na wa vijiji vyake watakuuliza: Umekuja kunyanganya? Umekusanya kundi lako la waaskari kwa kushambulia na kutwaa mateka na kubeba feza na zahabu, makundi ya nyama na vitu, na kuondoka na vitu vingi?


Halafu adui yangu ataona hayo naye atafunikwa na haya; maana aliniambia: Basi Yawe, Mungu wako, yuko wapi? Mimi mwenyewe nitamwona adui akianguka; atakanyagwakanyagwa chini kama matope katika njia.


Wewe si ndiwe Yawe, tangu zamani sana? Wewe ndiwe Mungu wangu, Mutakatifu wangu, usiyekufa. Ee Yawe, umewachagua Wakaldea watuhukumu! Ewe kimbilio letu, umewaimarisha kusudi watuazibu!


Watu wa Yuda watakuwa kama mashujaa katika vita, watawakanyaga waadui zao ndani ya matope katika njia. Watapigana kwa sababu mimi Yawe nipo pamoja nao; nao watawafezehesha hata waaskari wapanda-farasi.


Ninyi wanafiki! Isaya alitabiri vema juu yenu, wakati aliposema maneno haya:


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ