Zaidi ya hayo, munafikiri nimekuja bila amri ya Yawe kwa kuishambulia na kuiangamiza inchi hii? Yawe ndiye aliyeniambia: Uishambulie inchi hii na kuiangamiza!”
Haujasikia, ewe Saniharibu, kwamba mimi Yawe nilipanga jambo hili tangu zamani? Ninachotimiza sasa nilikipanga zamani. Nilikuweka uifanye miji yenye kuzungukwa na kuta kuwa lundo la mabomoko.
Ee Yawe, mukono wako uwafukuze kati ya watu, tukio lao likuwe kutengana na wanaokuwa wazima. Uwashibishe kwa akiba uliyowawekea, watoto wao nao washibe na kuacha sehemu, wawaachie hata na wajukuu wao.
Shoka litaweza kujisifu mbele ya yule anayelitumia? Musumeno unaweza kujivuna mbele ya mwenye kukata nao? Ni kama kwamba vile fimbo ingeweza kumwinua anayeishika, au gongo kumwinua mwenye kuitumia!
Nitauvunja uwezo wa Waasuria katika inchi yangu; nitawakanyagakanyaga katika milima yangu. Nitawaondolea watu wangu nira yao ya unyanganyi, na muzigo wa mateso yao.
(Ni Wakaldea, wala si Waasuria, waliowaacha nyama wa pori waushambulie muji wa Tiro. Wao ndio waliouzungushia muji huo minara ya kuushambulia, wakabomoa nyumba zake na kuufanya mabomoko.)
Muangalie, Yawe mwenyewe anakuja tokea mbali! Amewaka hasira na moshi unafuka; midomo yake inaonyesha kasirani yake, maneno anayosema ni kama moto unaoteketeza.
Yawe atawafanya watu wote waisikie sauti yake tukufu na pigo la nguvu yake lionekane kwa hasira nyingi. Kutakuwa ndimi za moto mukali, ngurumo, zoruba na mvua ya mawe.
Mutayaona hayo na mioyo yenu itafurahi; mifupa yenu itastawi tena kama vile majani mabichi. Kwa hiyo itajulikana kwamba mimi Yawe ninawalinda watumishi wangu, lakini nikikasirika ninawaazibu waadui zangu.
Yawe atakuletea wewe pamoja na watu wako na jamaa yote ya kifalme siku za taabu kuliko zile zote zilizotokea tangu wakati watu wa Efuraimu walipojitenga na watu wa Yuda; ni kusema, atawaletea ninyi mufalme wa Asuria.
Maana mbele mutoto huyu hajafikia umri wa kuweza kutamka neno “Baba” au “Mama”, utajiri wa muji wa Damasiki na vitu walivyonyanganya kule Samaria vitapelekwa kwa mufalme wa Asuria.
Mufalme atafanya kama anavyopenda. Atajitukuza na kujivuna kwamba yeye ni mukubwa kuliko miungu yote, na kumutukana Mungu wa miungu. Ataendelea kufanikiwa mpaka kasirani ifikie ukomo wake, maana yaliyopangwa sherti yatimie.
Wewe si ndiwe Yawe, tangu zamani sana? Wewe ndiwe Mungu wangu, Mutakatifu wangu, usiyekufa. Ee Yawe, umewachagua Wakaldea watuhukumu! Ewe kimbilio letu, umewaimarisha kusudi watuazibu!
Yawe atanyoosha mukono wake kwa kuazibu inchi ya upande wa kaskazini, na kuiangamiza inchi ya Asuria. Ataufanya muji wa Ninawe kuwa ukiwa, kuwa pahali penye kukauka kama jangwa.