Nyuma ya matendo hayo ya uaminifu ya mufalme Hezekia, mufalme Saniharibu wa Asuria akashambulia inchi ya Yuda. Akakuja kupiga makambi kwenye miji yenye kuta akitumaini kwamba ataishinda ikuwe mali yake.
Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe wa majeshi anasema hivi: Enyi watu wangu munaokaa Sayuni, musiwaogope Waasuria ambao wanawapiga kwa fimbo, wakiinua gongo zao juu yenu kama walivyofanya Wamisri.
Yawe atakausha guba ya bahari ya Misri, kwa pumzi yake inayochoma atakausha muto Furati, nao utagawanyika katika vijito saba, watu wavuke humo miguu mikavu.
Mungu anasema: Musimike bendera juu ya mulima usiokuwa na miti, muwapigie waaskari kelele, muwapepee watu kwa mukono, mukiwaita waingie kwenye milango ya muji wa wakubwa.
Katika siku zinazokuja, itatukia kwamba mulima wa nyumba ya Yawe utaimarishwa kupita milima yote, utainuliwa juu ya vilima vyote. Mataifa yote yatajaa kule,
Wameshika pinde zao na mikuki; ni watu wakali wasiokuwa na huruma. Vishindo vyao ni kama uvumi wa bahari. Wamepanda juu ya farasi, wamejipanga tayari kwa vita na wewe Sayuni!
Kisha aliwaua kwa makali ya upanga wakaaji wote wa Noba, muji wa makuhani, wanaume na wanawake, watoto wadogo na wenye kunyonya, ngombe, punda na kondoo.
Kwa hiyo Doegi Mwedomu, ambaye alikuwa amesimama karibu na watumishi wa Saulo akasema: “Nilimwona mwana wa Yese alipofika Noba kwa kuhani Ahimeleki mwana wa Ahitubu.