Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 10:29 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

29 Amekwisha pita kwenye kivuko. Usiku huu analala Geba. Watu wa Rama wanatetemeka kwa hofu, wakaaji wa Gibea, muji wa Sauli, wamekimbia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 10:29
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Matendo mengine yote ya Asa, ushujaa wake na miji yote aliyoijenga, yote yameandikwa katika Kitabu cha Mambo ya Siku za Wafalme wa Yuda. Wakati wa uzee wake, Asa alishikwa na ugonjwa wa miguu.


Yawe anasema hivi: Sauti imesikilika katika muji wa Rama, maombolezo na kilio cha uchungu. Rakeli anawalilia watoto wake, wala hataki kufarijiwa kwa ajili yao, maana wote hawako tena.


Enyi Waisraeli, ninyi mumetenda zambi tangia kule Gibea, na mpaka sasa munaendelea. Hakika vita itawaangamizia kulekule Gibea.


Mupige baragumu kule Gibea, na ngunga kule Rama. Mupige kelele la kujulisha hatari kule Beti-Aweni. Enyi watu wa Benjamina, adui yenu yuko nyuma!


Ninyi mumezama katika uovu, kama ilivyokuwa kule Gibea. Mungu atayakumbuka makosa yao, na kuwaazibu kwa ajili ya zambi zao.


Katika eneo la kabila la Benjamina walipewa miji mingine: Gibeoni pamoja na mbuga zake za malisho,


Vilevile, Saulo pamoja na wapiganaji hodari ambao zamani Mungu aligusa mioyo yao, alikwenda kwake kule katika muji wa Gibea.


Wale wajumbe walipofika katika muji wa Gibea, ambako Saulo alikoishi, wakaeleza habari hizo na watu wote wakaanza kulia kwa sauti.


Saulo na mwana wake Yonatani pamoja na watu waliokuwa pamoja nao, walikaa kule Gibea katika inchi ya Benjamina na Wafilistini walipiga kambi kule Mikimasi.


Saulo aliwachagua Waisraeli elfu tatu. Kati yao, elfu mbili alikuwa nao kule Mikimasi na katika inchi ya milima ya Beteli. Elfu moja aliwaweka kule Gibea katika eneo la Benjamina. Hao aliwaweka chini ya uongozi wa mwana wake Yonatani. Watu wengine wote waliobakia, aliwarudisha, kila mutu kwake.


Wafilistini walipeleka kikundi cha waaskari kwenda kulinda njia ya Mikimasi.


Saulo alikuwa amepiga kambi chini ya muti wa mukomamanga kule Migroni, inje ya muji wa Gibea, akiwa pamoja na watu yapata mia sita.


Kwenye mapito ya mulima ambako Yonatani alipaswa kuvukia kusudi afike kwenye kambi ya Wafilistini, kulikuwa chongo mbili, upande mumoja na upande mwingine. Chongo moja iliitwa Bozezi na ingine iliitwa Sene.


Chongo moja ilikuwa upande wa kaskazini wa muji wa Mikimasi na ingine ilikuwa upande wa kusini kuelekea muji wa Gibea.


Kisha, Samweli akaenda Rama; na mufalme Saulo akarudi kwenye nyumba yake kule Gibea.


Kisha, alikuwa akirudi Rama, maana kule ndiko kulikuwa kwake. Aliwaamulia Waisraeli haki zao kule, na kumujengea Yawe mazabahu kule.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ