Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 10:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Yawe wa majeshi atainua fimbo yake kama vile alivyowapiga Wamidiani kwenye jiwe la Orebu. Atanyoosha fimbo yake juu ya bahari kama vile alivyowafanyia Wamisri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 10:26
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, malaika wa Yawe aliingia ndani ya kambi ya Waasuria na kuwaua watu elfu mia moja makumi nane na watano. Kesho yake, wakati watu walipoamuka, waliona yale maiti yote.


Uinuke, ee Yawe, unitetee; ukuje, ee Mungu wangu, uangalie maneno yangu.


watu uliowaangamiza kule Endori, wakakuwa takataka juu ya inchi.


Inua fimbo yako na kuielekeza juu ya bahari. Maji yatagawanyika na Waisraeli wataweza kuvuka katikati ya bahari pahali pakavu.


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe wa majeshi anasema hivi: Enyi watu wangu munaokaa Sayuni, musiwaogope Waasuria ambao wanawapiga kwa fimbo, wakiinua gongo zao juu yenu kama walivyofanya Wamisri.


Tena, kutakuwa barabara kubwa toka Asuria kwa ajili ya watu wake waliobaki humo kama ilivyokuwa kwa Waisraeli wakati walipotoka katika inchi ya Misri.


Yawe atawafanya watu wote waisikie sauti yake tukufu na pigo la nguvu yake lionekane kwa hasira nyingi. Kutakuwa ndimi za moto mukali, ngurumo, zoruba na mvua ya mawe.


Waasuria watajaa hofu watakaposikia sauti ya Yawe, wakati atakapowapiga na fimbo yake.


Kila pigo la azabu ya Yawe juu ya Waasuria litaandamana na mudundo wa ngoma na zeze. Yeye mwenyewe atapigana na Waasuria.


Maana miti mizito waliyobeba, nira walizokuwa wamefungwa, na fimbo ya wasimamizi, umezivunjavunja kama wakati wa Wamidiani.


Viatu vyote vya washambulizi katika vita na nguo zote zenye kujaa damu vitateketezwa kama kuni za kuwasha moto.


Watu wa mataifa mengine walikasirika, lakini kasirani yako imetokea. Sasa ni wakati wa kuhukumu waliokufa, nao wakati wa kuwapa waliokutumikia zawadi, ndio manabii wako, na wote wanaoheshimu jina lako, wakubwa na wadogo. Ni wakati wa kuangamiza wale wanaoharibu dunia!”


Ndani ya kinywa chake mulitoka upanga mukali kwa kushinda mataifa. Naye atatawala kwa fimbo ya chuma na kukamua zabibu ndani ya kikamulio cha divai kinachojaa kasirani kali ya Mungu Mwenye Uwezo.


Wakatwaa mateka viongozi wawili wa Midiani, majina yao ni Kibombobombo na Imbwa-wa-Pori. Wakamwua Kibombobombo juu ya jiwe la Kibombobombo, naye Imbwa-wa-Pori wakamwua katika kikamulio cha Imbwa-wa-Pori wakiwa wanawafuatilia Wamidiani. Wakamuletea Gideoni vichwa vya Kibombobombo na Imbwa-wa-Pori, ngambo ya muto Yordani.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ