Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 10:24 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

24 Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe wa majeshi anasema hivi: Enyi watu wangu munaokaa Sayuni, musiwaogope Waasuria ambao wanawapiga kwa fimbo, wakiinua gongo zao juu yenu kama walivyofanya Wamisri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 10:24
28 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

aliwaambia: “Mumwambie bwana wenu kwamba Yawe anasema hivi: ‘Usiogope kwa sababu ya maneno uliyoyasikia, ambayo watumishi wa mufalme wa Asuria wameyasema kwa kunitusi.


Wamisri pamoja na farasi wao wote, magari ya vita na wapanda-farasi wake waliwafuata Waisraeli. Wakawakuta wamepiga kambi kando ya bahari, karibu na Pi-Hahiroti, mbele ya Bali-Sefoni.


Wakubwa wa Wamisri wakawapiga wasimamizi wa Waisraeli waliochaguliwa kusimamia kazi wakisema: “Kwa nini hamutimizi kazi yenu na kufikisha hesabu ileile ya matofali kama mbele?”


Ole kwake Asuria, yeye ni kama fimbo ya hasira yangu, yeye anayeshika kiboko cha hasira yangu!


Mungu ndiye mwenye kuniokoa, nitamutegemea yeye, wala sitaogopa; Yawe ananijalia nguvu; yeye mwenyewe ndiye anayeniokoa.


Mupige vigelegele na kuimba kwa furaha, enyi wakaaji wa Sayuni, maana Mutakatifu wa Israeli ni makubwa kati yenu.


Musishangilie, enyi Wafilistini wote, kwamba Asuria, fimbo iliyowapiga, imevunjika; maana, nyoka wa kawaida atazaa nyoka mwenye sumu, na nyoka mwenye sumu atazaa nyoka mukubwa mwenye kuruka.


Mungu hakuwaazibu Waisraeli vikali kama alivyowaazibu waadui zao; Waisraeli waliouawa ni wachache kuliko wale waliokuwa wanawaua.


Enyi watu wa Sayuni, enyi watu wa Yerusalema, hakika ninyi hamutaomboleza tena. Kweli Mungu atawahurumia; mara tu atakaposikia kilio chenu atawaitikia.


Kila pigo la azabu ya Yawe juu ya Waasuria litaandamana na mudundo wa ngoma na zeze. Yeye mwenyewe atapigana na Waasuria.


Muwaambie waliovunjika moyo: Mujipe moyo, musiogope! Muangalie Mungu wenu atakuja kulipiza kisasi, atakuja kuwaazibu waadui zenu; atakuja yeye mwenyewe kuwaokoa ninyi.


basi huu ndio ujumbe wa Yawe juu ya huyo mufalme: Watu wa Sayuni wanakuzarau kabisa, Watu wa Yerusalema wanakutikisia kichwa kwa kukuchekelea.


aliwaambia: “Mumwambie bwana wenu kwamba Yawe anasema hivi: Usiogope kwa sababu ya maneno uliyoyasikia, ambayo watumishi wa mufalme wa Asuria wameyasema kwa kunitusi.


Wale watakaobaki wazima katika Yerusalema, huko Sayuni, wataitwa Wachaguliwa wa Mungu; hao ndio wale wote watakaokuwa wameandikwa katika kitabu chake waishi huko Yerusalema.


Siku ya kuwakomboa inakaribia, haiko mbali tena; siku ya kuwaokoa ninyi haitachelewa. Nitauokoa Sayuni, nitaleta utukufu kwa Israeli.


Wewe umenisahau mimi Yawe Muumba wako, niliyezitandaza mbingu, na kuiweka misingi ya dunia! Kwa sababu ya kasirani ya yule anayekutesa, unaendelea kuogopa siku zote kwamba yuko tayari kukuangamiza! Lakini hasira yake itafikia wapi?


na kuwapa wale wanaoomboleza katika Sayuni taji la maua pahali pa majivu juu ya kichwa, mafuta ya kuangarisha kwa furaha pahali pa maombolezo, nguo ya sifa pahali pa moyo muzito. Nao wataitwa miti ya mialo ya haki, Yawe aliyopanda kuonyesha utukufu wake.


Umwambie akuwe macho, atulie na asiogope wala asivunjike moyo, kwa sababu ya hasira kali ya mufalme Resini wa Aramu, na ya mwana wa Remalia. Hao wawili ni kama tu moshi wa kuni zinazozimika.


Viatu vyote vya washambulizi katika vita na nguo zote zenye kujaa damu vitateketezwa kama kuni za kuwasha moto.


Kwa silaha zao wataitawala inchi ya Asuria, na kuirizi inchi ya Nimurodi. Watatuokoa toka katika mikono ya Waasuria, watakapoingia katika inchi yetu na kuanza kuishambulia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ