Isaya 10:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
20 Siku ile wazao wa Yakobo watakaobaki, ni kusema Waisraeli watakaopona hawatalitegemea tena taifa lililowaazibu, lakini watamutegemea kabisa Yawe, Mutakatifu wa Israeli.
Basi Ahazi akatuma watu kwa mufalme Tigilati-Pileseri wa Asuria wakiwa na ujumbe huu: “Mimi ni mutumishi wako mwaminifu. Ukuje uniokoe kutoka kwa wafalme wa Aramu na Israeli ambao wananishambulia.”
Maana kutakuwa watu watakaobaki kule Yerusalema; kule kwenye mulima Sayuni kutakuwa watu wachache watakaobakia. Yawe wa majeshi amekusudia kukamilisha hayo.
Tutavunja amri zako tena na kuoana na watu hawa wanaotenda maovu haya? Hautatukasirikia na kutuangamiza kabisa, na kusibaki hata mumoja wetu muzima wala yeyote wa kutoroka?
Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari.
Labda Yawe, Mungu wako, alisikia maneno ya yule jemadari ambaye ametumwa na bwana wake mufalme wa Asuria, kwa kumutukana Mungu Mwenye Uzima, naye Yawe, Mungu wako atamwazibu kwa ajili ya maneno aliyoyasikia. Uwaombee watu wanaobaki.”
Musikilize, enyi wazao wa Yakobo, munisikilize, enyi mabaki ya watu wangu wa Israeli. Mimi niliwatunza ninyi tangu mulipozaliwa; niliwabeba ninyi tangu katika tumbo la mama yenu.
Nani kati yenu anayemwogopa Yawe? Nani anayetii maneno ya mutumishi wake? Kama kuna mutu anayetembea katika giza bila taa, amutumainie Yawe, na kumutegemea Mungu wake.
Hata kukibaki sehemu moja ya kumi ya watu, nao vilevile watateketezwa. Hao watakuwa kama muti wa muvinje au wa mwalo ambao shina lake limebaki kisha kukatwa. Shina hilo ni mbegu takatifu ya mwanzo mupya.
Kwa hiyo hakutakuwa mutu hata mumoja kati ya watu wa Yuda waliobaki na kwenda kukaa katika inchi ya Misri ambaye ataponyoka au kuishi au kurudi katika inchi ya Yuda ambayo wanatamani kurudi na kuishi humo. Hawatarudi, isipokuwa tu wakimbizi wachache.
Watu wa Efuraimu walipogundua ugonjwa wao, watu wa Yuda walipogundua kidonda chao, watu wa Efuraimu walikwenda Asuria kuomba musaada kwa mufalme mukubwa; lakini yeye hakuweza kuwatunza, hakuweza kuponyesha kidonda chao.
Huyo mutawala atawachunga watu wake kwa nguvu ya Yawe, kwa utukufu wa Yawe, Mungu wake. Watu wake wataishi kwa usalama, maana atakuwa mukubwa mpaka kwa miisho ya dunia.