Umewatuma watumishi wako kuchekelea Yawe; wewe umesema: Kwa magari yangu mengi ya vita, nimefika juu kwenye vichwa vya milima, mpaka kwenye vichwa vya milima ya Lebanoni. Nimeangusha mierezi yake mirefu, na misunobari mizurimizuri. Nimevifikia vichwa vyake na ndani ya pori zake kubwa.
Kwa vile umefanya mipango juu yangu na nimesikia majivuno yako, nitatia ndoana yangu ndani ya pua yako, na lijamu yangu ndani ya kinywa chako. Nitakurudisha katika njia ileile uliyokuja ndani yake.
Umewatuma watumishi wako kumuchekelea Bwana wenu; wewe umesema: Kwa magari yangu mengi ya vita, nimefika juu kwenye vichwa vya milima, mpaka kwenye vichwa vya milima ya Lebanoni. Nimeangusha mierezi yake mirefu, na misunobari mizurimizuri. Nimevifikia vichwa vyake na ndani ya pori zake kubwa.
Siku hiyo, nitawafanya wakubwa wa Yuda kuwa kama chungu chenye moto mukali katika pori, kama mwenge wa moto unaowaka kati ya miganda. Watayateketeza mataifa yote yanayokuwa kandokando yao. Lakini watu wa Yerusalema wataendelea kuishi salama katika muji wao.