Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 10:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Maana mufalme wa Asuria alisema: Kwa nguvu zangu mwenyewe nimetenda hayo, na kwa hekima yangu, maana mimi ni mwerevu! Nimeondoa mipaka kati ya mataifa, nikanyanganya akiba zao; kama ngombe dume nimewaporomosha walioikaa juu ya viti vya kifalme.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 10:13
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati wa utawala wa Peka mufalme wa Israeli, Tigilati-Pileseri, mufalme wa Asuria, aliteka miji ya Iyoni, Abeli-Beti-Maka, Yanoa, Kadesi na Hazori, pamoja na inchi za Gileadi, Galilaya na Nafutali na kuwahamisha wakaaji wake kwenda Asuria.


Ahazi akatwaa feza na zahabu iliyokuwa katika nyumba ya Yawe na hazina iliyokuwa katika nyumba ya mufalme na kumupelekea kama zawadi mufalme wa Asuria.


Kisha mufalme wa Asuria akapeleka watu kutoka Babeli, Kuta, Awa, Hamati na Sefarwaimu na kuwaweka katika miji ya Samaria kwa pahali pa watu wa Israeli waliopelekwa katika uhamisho. Wakaitwaa miji hiyo na kukaa mule.


Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea, mufalme wa Asuria aliuteka muji wa Samaria na kuwapeleka watu wa Israeli katika uhamisho mpaka Asuria. Wamoja kati yao akawaweka katika muji wa Hala, wengine karibu na muto Habori, muto Gozani na wengine katika miji ya Wamedi.


Mufalme wa Asuria akakamata watu wa Israeli na kuwapeleka mpaka Asuria na kuwaweka wengine wao katika muji wa Hala, na karibu ya Habori, muji wa Gozani, vilevile na wengine katika miji ya Wamedi,


Hezekia akamupelekea feza yote iliyokuwa katika nyumba ya Yawe na katika hazina za nyumba ya mufalme.


mpaka nitakapokuja na kuwapeleka katika inchi kama hii yenu, inchi yenye ngano na divai, inchi yenye mukate na mashamba ya mizabibu, inchi yenye mizeituni na asali, kusudi mupate kuishi, nanyi hamutakufa. Musimusikilize Hezekia anapowadanganya akisema: Yawe atatuokoa.


Basi, Mungu wa Israeli akasukuma roho ya Puli, mufalme wa Asuria, (ambaye alijulikana vilevile kwa jina la Tiglati-Pileseri), akashambulia inchi yao na kuwapeleka watu wa kabila la Rubeni, la Gadi na nusu ya kabila la Manase kwa upande wa mashariki mpaka uhamisho kule Hala, Habori na Hara, pembeni ya muto Gozani, ambako wamekaa mpaka leo.


Tajiri anajiona mwenyewe kuwa mwenye hekima, lakini masikini mwenye akili atamufichua.


Maana alisema: Si kweli majemadari wangu ni wafalme?


Ole kwao wanaojiona kuwa wenye hekima na akili.


Misri ni kama muto Nili uliofurika, kama mito inayovumisha mawimbi. Ilisema: Nitajaa, nitaifunika inchi, nitaiharibu miji na wakaaji wake.


Namna gani munaweza kusema: Sisi ni mashujaa, na watu wenye nguvu nyingi za vita?


Uwaambie Waamoni hivi: Musikilize neno la Bwana wetu Yawe: Ninyi mulifurahia kuona hekalu langu likichafuliwa, inchi ya Waisraeli ikiangamizwa na watu wa Yuda wakipelekwa katika uhamisho.


Wewe mwanadamu! Watu wa muji wa Tiro wameuchekelea Yerusalema na kusema: Aha! Yerusalema muji ambao watu wote walipitia, umeangamizwa! Sasa umetuachia nafasi; utajiri wake umeharibika!


Umwambie kwamba Bwana wetu Yawe anasema hivi: Mimi nitapingana na wewe mufalme wa Misri, wewe mamba unayelala ndani ya muto Nili! Wewe unafikiri kwamba muto Nili ni wako, kwamba wewe ndiwe uliyeufanya!


Nimesikia jinsi unavyojivuna na kusema maneno mengi juu yangu.


Basi, akasema kwa sauti: Angalia Babeli, muji mukubwa nilioujenga kwa nguvu zangu ukuwe makao yangu ya kifalme na kwa ajili ya utukufu wangu!


Mara moja jambo hilo juu ya mufalme Nebukadneza likatimizwa. Alifukuzwa mbali na wanadamu, akakuwa anakula majani kama ngombe. Alilowanishwa na umande wa mbinguni, na nywele zake zikakuwa ndefu kama manyoya ya tai, na kucha zake kama za ndege.


Kwa hiyo nitawapeleka katika uhamisho, mbali kuliko Damasiki! –Ni Yawe anayesema, ambaye jina lake ni Mungu wa majeshi.


Ninyi munashangilia juu ya muji wa Bure na kusema mumeuteka muji wa Nguvu kwa nguvu zenu wenyewe.


Kisha wanasonga mbele kama upepo, wanapita na kufanya makosa. Nguvu zao ndio mungu wao!


Kwa hiyo, wanazitambikia nyavu zao, na kuzifukizia ubani; maana kwa njia ya vitu hivyo mapato yao yanaongezeka, na wanakuwa na chakula kingi.


Kila mutu atamuchekelea mutu wa namna hiyo na kumutungia misemo ya kitambi: Ole wako unayejilundikia visivyokuwa vyako, na kutwaa rehani mali za watu lakini haulipi! Utaendelea kufanya hivyo mpaka wakati gani?


Hivyo mufanye angalisho kusudi musijisemeshe ndani ya mioyo yenu: ‘Tumejitajirisha kwa uwezo na nguvu zetu wenyewe’.


Yawe akamwambia Gideoni: “Watu unaokuwa nao ni wengi sana kwangu mimi kwa kuwatia Wamidiani katika mikono yao. Waisraeli wasipate kujisifu mbele yangu na kusema kwamba wamejiokoa kwa nguvu zao wenyewe.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ