Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 1:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Yawe wa majeshi asingetuachia watu wachache, tungekwisha kuwa kama watu wa Sodoma tungekuwa na hali ileile ya Gomora.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 1:9
37 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akamwambia: “Nikikuta watu wa haki makumi tano kule katika muji wa Sodoma, basi nitaacha muji wote salama kwa ajili yao.”


Kisha Abrahamu akasema: “Ee Bwana, ninakuomba usikasirike, lakini nitasema tena mara moja tu. Labda kutapatikana watu wema kumi.” Yawe akamujibu: “Kwa ajili ya hao watu wema kumi, sitaangamiza muji ule.”


Halafu Yawe akateremusha moto mukali wa kiberiti kutoka mbinguni juu ya Sodoma na Gomora,


Lakini, nitawaacha wazima watu elfu saba katika inchi ya Israeli, ambao hawajainama mbele ya Bali, wala kuibusu sanamu yake.”


Labda Yawe, Mungu wako, alisikia maneno ya yule jemadari ambaye ametumwa na bwana wake mufalme wa Asuria, kwa kumutukana Mungu Mwenye Uzima, naye Yawe, Mungu wako atamwazibu kwa ajili ya maneno aliyosikia. Uwaombee watu wanaobaki.’ ”


Sayuni umeachwa kama kibanda katika shamba la mizabibu, kama kibanda cha mulinzi katika shamba la maboga, kama muji uliozungukwa kwa vita.


Siku hiyo, Bwana ataunyoosha mukono wake tena kuwarudisha watu wake waliobaki kule Asuria, Misri, Patirosi, Etiopia, Elamu, Sinari, Hamati na sehemu za visanga vya bahari.


Tena, kutakuwa barabara kubwa toka Asuria kwa ajili ya watu wake waliobaki humo kama ilivyokuwa kwa Waisraeli wakati walipotoka katika inchi ya Misri.


Watabaki wachache kama vile kisha kuangusha matunda ya mizeituni: matunda mawili au matatu katika tawi la juu; mane, matano katika matawi yanayozaa sana. –Ni ujumbe wa Yawe, Mungu wa Israeli.


Kama vile zeituni chache tu juu ya mizeituni au tini chache tu juu ya muti wa tini, kisha kumaliza mavuno, ndivyo inavyokuwa katika inchi zote.


Kwa sababu hiyo laana inaiteketeza dunia, wakaaji wake wanateseka kwa ajili ya makosa yao. Wakaaji wa dunia wamepunguka, ni watu wachache tu waliobaki.


Labda Yawe, Mungu wako, alisikia maneno ya yule jemadari ambaye ametumwa na bwana wake mufalme wa Asuria, kwa kumutukana Mungu Mwenye Uzima, naye Yawe, Mungu wako atamwazibu kwa ajili ya maneno aliyoyasikia. Uwaombee watu wanaobaki.”


Musikilize, enyi wazao wa Yakobo, munisikilize, enyi mabaki ya watu wangu wa Israeli. Mimi niliwatunza ninyi tangu mulipozaliwa; niliwabeba ninyi tangu katika tumbo la mama yenu.


Hata kukibaki sehemu moja ya kumi ya watu, nao vilevile watateketezwa. Hao watakuwa kama muti wa muvinje au wa mwalo ambao shina lake limebaki kisha kukatwa. Shina hilo ni mbegu takatifu ya mwanzo mupya.


Yawe anasema hivi: Mutu akikuta kishada cha mizabibu mizuri, watu wanasema: Tusikiharibu; kina baraka. Ndivyo nitakavyofanya kwa ajili ya watumishi wangu; sitawaangamiza wote.


Lakini kati ya manabii wa Yerusalema, nimeona mambo ya kutisha zaidi: wao wanafanya uzinzi na kusema uongo; wanawaunga mukono wanaotenda maovu hata kusikuwe mutu anayeachana na uovu. Kwangu wote wamekuwa kama watu wa Sodoma; wakaaji wake wamekuwa kama watu wa Gomora.


wakamwendea Yeremia, wakamwambia: Tafazali sikiliza maombi yetu na kutuombea kwa Yawe, Mungu wako, sisi wote tuliobaki, kwa maana tulikuwa wengi, lakini sasa tumebaki wachache tu, kama unavyoona.


Siku hizo na wakati huo, uovu utatafutiwa katika inchi ya Israeli, lakini hautapatikana; zambi itatafutiwa katika inchi ya Yuda, lakini haitapatikana; maana mimi nitawasamehe wale ambao nimewaponyesha. –Ni ujumbe wa Yawe.


Wema wa Yawe haukomi, huruma zake hazina mwisho.


Kosa la watu wangu lilikuwa kubwa kuliko zambi za watu wa Sodoma, muji ambao uliteketezwa kwa rafla bila kuwa na muda wa kunyoosha mukono.


Hata hivyo, kutabaki wazima watu watakaoponyoka na kuwaleta wana na wabinti zao kwako, wewe Ezekieli. Utaona jinsi wanavyokuwa waovu sana; nawe utakubali kwamba azabu yangu juu ya Yerusalema ni ya haki.


Hata hivyo, nitawaacha wengine wabaki wazima; wamoja kati yenu wataponyoka upanga nao watasambazwa katika inchi mbalimbali.


Niliwaangusha wamoja kati yenu kwa maangamizi kama nilivyoangamiza Sodoma na Gomora. Wale waliobaki kati yenu, walikuwa kama kijiti kilichookolewa katika moto. Hata hivyo hamukunirudilia. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Ee Yawe, nimesikia juu ya utukufu wako, juu ya matendo yako, nami ninaogopa. Uyafanye tena mambo yale wakati wetu; uyafanye yajulikane wakati huu wetu. Unapokasirika tafazali ukumbuke huruma yako!


Kwa hiyo, kama vile ninavyoishi, –ni ujumbe wa Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli– inchi ya Moabu itakuwa kama Sodoma na ya Amoni itakuwa kama Gomora. Inchi zake zitakuwa shamba la miiba na mashimo ya chumvi, zitakuwa ukiwa milele. Watu wangu watakaobaki wataziteka, watu wa taifa langu waliobaki watazirizi.


Lakini njia inayoongoza kufikia kwenye uzima ni yenye kusongamana na mulango unaoiingilia ni mwembamba, nao watu wanaoifuata ni wachache tu.


Isaya alisema kwa sauti juu ya Waisraeli: “Ijapokuwa Waisraeli ni wengi kama muchanga wa bahari, ni wachache tu watakaookolewa.


Ni kama vile Isaya alivyokuwa ametangulia kusema: “Kama Bwana wa Majeshi hangetuponyeshea wamoja wa wazao wetu, ingetutokea sawa Sodoma, ingegeuka kwetu sawa Gomora.”


Hata mataifa yote yatasema: ‘Kwa nini Yawe ameitendea hivyo inchi hii? Hasira hii kubwa ina maana gani?’


Vilevile Mungu alihukumu muji wa Sodoma na Gomora na kuiteketeza kwa moto. Kwa njia hiyo, alionyesha mufano wa mambo yatakayotokea kwa watu waovu.


Maiti zao zitabaki katika barabara ya muji ule mukubwa unaoitwa kwa fumbo Sodoma au Misri. Ni ndani ya muji ule Bwana wao alitundikwa juu ya musalaba.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ