Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 1:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Tokea kwenye muguu mpaka kwenye kichwa hakuna chenye kuwa kizima; ni machubuko, alama za mapigo na vidonda vinavyovuja damu, vilivyokosa kusafishwa, kufungwa wala kutulizwa kwa mafuta.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 1:6
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Katika inchi yote ya Israeli, hakuna mutu yeyote aliyesifiwa kwa uzuri wa umbo kama Abusaloma. Tangia kwenye miguu mpaka kwenye kichwa, Abusaloma hakukuwa na kilema chochote.


Maana yeye anaumiza na tena anatunza, anatia kidonda na kwa mukono wake anaponyesha.


Ninamulilia Mungu kwa sauti. Kwa sauti ninamulilia Mungu, anisikie.


Tena mwezi utawaka kama jua, nao mwangaza wa jua utakuwa mara saba ya mwangaza wake wa kawaida, sawa vile kwamba mwangaza wa siku saba umeangaza katika siku moja. Mambo haya yote yatatukia wakati Yawe atakapofunga vidonda na kuponyesha mapigo aliyowaletea watu wake.


Moyo wa mutu ni mudanganyifu kuliko vitu vyote; hauwezi kuponyeshwa, hakuna anayeweza kuuelewa!


Yawe anasema hivi: Mapigo yako hayaponi, vidonda vyako haviwezi kutunzwa.


Kwa nini unalia kwa ajili ya kidonda chako? Maumivu yako hayawezi kupona. Nimekutendea hayo yote, kwa sababu kosa lako ni kubwa, zambi zako ni nyingi sana.


Hata hivyo, mimi nitauponyesha muji huu na kuwapa watu wake afya; nitawajalia ustawi mwingi na usalama.


Wanatunza vidonda vya watu wangu juujuu, wakisema: “Kuna amani, kuna amani”, ingawa hakuna amani yoyote!


Kama vile maji yanavyotiririka toka ndani ya kisima, ndivyo maovu yanavyotiririka katika Yerusalema. Mateso makali na maangamizi yanasikilika ndani yake. Ninaona magonjwa na vidonda mbele yangu kila siku.


Hakuna wa kutunza mapigo yako, vidonda vyako ni vya kifo. Wote wanaosikia habari zako wanashangilia. Maana ni nani aliyeponyoka kila mara uovu wako?


Lakini Yesu alisikia vile walivyosema, na kwa hiyo akawaambia: “Wenye afya nzuri hawahitaji muganga lakini wale wanaokuwa wagonjwa.


Akajongea karibu naye, akamutunza vidonda, akivimwangia divai na kuvimimia mafuta na kuvifunga na vitambaa. Kisha akamupandisha juu ya punda wake, na kumupeleka kwenye nyumba ya kupangisha wageni na kumuchunga.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ