Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 1:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Niwapige wapi tena, ninyi munaoendelea kuasi? Kichwa chote kinajaa vidonda, na moyo unaumia kabisa!

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 1:5
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa mara ingine tena, mufalme akatuma kiongozi mwingine na watu wake makumi tano. Kiongozi wa tatu akapanda kwenye mulima, akapiga magoti mbele ya Elia na kumusihi akisema: “Ewe mutu wa Mungu, ninakusihi uyahesabu maisha yangu na maisha ya hawa watumishi wako makumi tano yakuwe ya bei kali mbele yako.


Wakati alipokuwa katika taabu zaidi, mufalme huyu Ahazi alizidi kumwasi Yawe.


Wafalme wetu, wakubwa wetu, makuhani wetu na babu zetu hawakushika Sheria yako wala kujali amri zako na maonyo yako uliyowapa.


Wakubwa wako ni waasi; wanashirikiana na wizi. Kila mumoja anapenda kituliro, na kukimbilia zawadi. Hawamupatii yatima haki yake, haki za wajane si kitu kwao.


Enyi Waisraeli, mumurudilie yule muliyemwacha kabisa.


Hakuna atakayesema tena ni mugonjwa; watu watasamehewa uovu wao wote.


Yawe atakata katika Israeli kichwa na mukia, tawi la mingazi na nyasi, kwa muda wa siku moja tu.


Mwetiopia anaweza kubadilisha rangi yake, au chui madoadoa yake? Nanyi muliozoea kufanya mabaya, munaweza namna gani kutenda mema?


Moyo wa mutu ni mudanganyifu kuliko vitu vyote; hauwezi kuponyeshwa, hakuna anayeweza kuuelewa!


Niliwaazibu ninyi lakini ilikuwa bure, ninyi munakataa maonyo. Muliwateketeza manabii wenu kwa upanga kama simba mwenye uchu.


Kisha, wanaume wote waliojua kwamba wake wao walikuwa wameifukizia miungu mingine ubani, na wanawake wote waliokuwa hapo, kusanyiko kubwa la watu pamoja na Waisraeli waliokuwa wanakaa Patro katika inchi ya Misri walimujibu Yeremia:


Ee Yawe, wewe unatafuta uaminifu siku zote. Umewatwanga, lakini hawakuona uchungu; umewateketeza, lakini walikataa maonyo. Wamevifanya vichwa vyao kuwa vigumu kuliko jiwe; wamekataa kabisa kurudi kwako.


manabii wanatabiri mambo ya uongo, nao makuhani wanatafuta faida yao wenyewe; nao watu wangu wanaona jambo hilo kuwa sawa. Lakini mwisho wake utakapofika mutafanya nini?


Nitawaendea wakubwa niongee nao; bila shaka, wao wanajua mapenzi ya Yawe; wanajua sheria ya Mungu wao. Lakini wote ni sawa. Wamevunja nira yao, wamekata minyororo yao.


Kila mutu ajiepushe na jirani yake, wala asimwaminie ndugu yake! Maana ndugu ni mudanganyifu na kila jirani ni musingiziaji.


Kwa ajili ya hiyo tumeugua ndani ya moyo, kwa ajili ya hiyo macho yetu yamefifia.


Ewe Yerusalema, matendo yako machafu yamekuchafua. Ingawa nilijaribu kukutakasa, mwenyewe ulibaki muchafu. Basi, hautatakasika tena mpaka nitakapotuliza hasira yangu juu yako.


Nitawatafuta kondoo waliopotea na waliotangatanga nitawarudisha kwa nyumba. Waliovunjika nitawatunza, na wale wanaokuwa zaifu nitawapatia nguvu. Lakini kondoo wanono na wenye nguvu nitawaangamiza. Mimi nitawachunga kondoo kama inavyostahili.


Wanaokuwa zaifu hamukuwatia nguvu, wagonjwa hamukuwatunza, waliovunjika hamukuwafunga kwa kitambaa, waliotangatanga hamukuwarudisha na waliopotea hamukuwatafuta. Lakini mukawatawala kwa kinguvu na kuwatesa.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ