Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 1:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Ole kwako wewe taifa lenye zambi, watu waliolemewa na uovu, kizazi cha watenda mabaya, watoto wanaoishi kwa udanganyifu! Ninyi mumemwacha Yawe, mumemuzarau Mutakatifu wa Israeli, mumerudi nyuma.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 1:4
69 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu wa Sodoma walikuwa waovu na watenda zambi wakubwa mbele ya Yawe.


Alimwacha Yawe, Mungu wa babu zake. Hakushika njia ya Yawe.


Wakati Rehoboamu alipoimarisha utawala wake, yeye pamoja na watu wake wote waliacha kutii Sheria ya Yawe.


Alitenda kwa usawa mbele ya Yawe kama vile Uzia baba yake alivyotenda. Hakuingia katika hekalu la Yawe. Watu waliendelea kufanya maovu.


Tumetenda mabaya mbele yako, hatujashika amri zako, masharti na maagizo yako uliyomwagiza mutumishi wako Musa.


Hapana. Ninyi munafikiria tu kutenda maovu; ninyi wenyewe munaeneza mateso makali katika inchi.


Nami nitakusifu kwa kinubi, kwa sababu ya uaminifu wako, ee Mungu wangu; nitakuimbia sifa kwa zeze, ewe Mutakatifu wa Israeli.


Mara ngapi walimwasi kule katika jangwa, na kumuchukiza huko kwenye ukiwa!


Walimujaribu Mungu tena na tena, wakamukasirikisha huyo Mutakatifu wa Israeli.


Lakini waligeuka na kufanya mabaya kama babu zao; wakayumbayumba kama upinde usiokuwa imara.


wasikuwe kama vile babu zao walivyokuwa, watu wagumu na waasi, kizazi ambacho hakikuwa na musimamo kamili, ambacho hakikuwa na uaminifu kwa Mungu.


Wewe ndiwe utukufu na nguvu yao; kwa upendo wako tunapata ushindi.


Yawe akamwambia Musa: Teremuka chini kwa maana watu wako uliowaleta kutoka inchi ya Misri wamejipotosha wenyewe.


Wakubwa wako ni waasi; wanashirikiana na wizi. Kila mumoja anapenda kituliro, na kukimbilia zawadi. Hawamupatii yatima haki yake, haki za wajane si kitu kwao.


Lakini waasi na wenye zambi wote wataangamizwa pamoja; wanaomwacha Yawe watateketezwa.


Nilimutuma kuliazibu taifa ovu, nilimwamuru kuwaazibu watu niliowakasirikia, kuwanyanganya na kuteka vitu vyao, na kuwakanyaga chini kama matope katika njia.


Mupige vigelegele na kuimba kwa furaha, enyi wakaaji wa Sayuni, maana Mutakatifu wa Israeli ni makubwa kati yenu.


Lakini wewe hautaunganishwa nao katika mazishi, maana uliiharibu inchi yako, uliwaua watu wako. Wazao wa waovu wasahauliwe kabisa!


Wanyenyekevu watapata furaha mupya kwa Yawe, na wamasikini kati ya watu watashangilia kwa furaha, kwa sababu ya Mungu, Mutakatifu wa Israeli.


Watu wa Yerusalema wamejikwaa, watu wa Yuda wameanguka, kwa sababu wanamupinga Yawe kwa maneno na matendo, wakizarau utukufu wake kati yao.


Ole watoto waasi, wanaotimiza mipango yao na si mipango yangu, wanaofanya mapatano kinyume cha mapenzi yangu! –Ni ujumbe wa Yawe.– Kweli, wanalundika zambi juu ya zambi.


Bwana wetu Yawe, Mutakatifu wa Israeli anasema hivi: Mukinirudilia na kutulia mutaokolewa; kwa utulivu na kunitumainia mutapata nguvu. Lakini ninyi hamukutaka.


Watu hawa ni waasi, watoto wasioaminiwa; watu wasiopenda kusikia mafundisho ya Yawe.


Mungu ni mwenye hekima na analeta maangamizi. Habadilishi masemi yake; lakini yuko tayari kuwaazibu watu waovu vilevile na wasaidizi wa watenda mabaya.


Wewe umemutukana nani? Umemutusi nani? Umesubutu kumufokea nani kwa majivuno? Ni Mungu, Mutakatifu wa Israeli!


Enyi watu wa Yakobo zaifu kama mududu, enyi Waisraeli, musiogope! Nitawasaidia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Mukombozi wenu ni yule Mutakatifu wa Israeli.


Mutaipepeta milima hiyo, nao upepo utaipeperushia mbali, zoruba itaitawanya huko na huko. Nanyi mutafurahi kwa sababu yangu Yawe; mutaona utukufu kwa sababu yangu Mungu Mutakatifu wa Israeli.


Watu wataona jambo hilo, nao watatambua na kuelewa kwamba mimi Yawe nimetenda hayo, mimi Mutakatifu wa Israeli nimefanya jambo hilo.


Wanasema: Muache Yawe afanye haraka, tunataka kuona yale aliyosema atayafanya! Mutakatifu wa Israeli atimize basi kusudi lake kusudi tuone ana mipango gani!


Kwa hiyo, kama vile moto unavyoteketeza nyasi, kama vile majani yanavyotoweka ndani ya moto, ndivyo mizizi yao itakavyooza, na maua yao yatakavyopeperushwa juu kama mavumbi. Maana wameacha sheria ya Yawe wa majeshi, wamezarau neno la yule Mutakatifu wa Israeli.


Niliwakasirikia kwa sababu ya uovu na tamaa zao; niliwaazibu, nikauficha uso wangu na kukasirika. Lakini wao waliendelea kufuata njia zao wenyewe.


Kila siku wananitafuta, wanatamani kujua njia zangu, kama vile wao ni taifa linalotenda haki, taifa lisilosahau agizo la Mungu wao. Wanataka niamue kwa haki, na kutamani kuikaa karibu na Mungu.


Lakini nitafanya nini na ninyi munaoniacha mimi Yawe, musioujali Sayuni, mulima wangu mutakatifu, munaotolea miungu chakula na divai kusudi iwapatie bahati zuri.


Ni watu ambao wananichokoza waziwazi siku zote; wanatambikia miungu yao katika bustani, na kuifukizia ubani juu ya matofali.


Uovu unawaka kama moto unaoteketeza michongoma na miiba; unawaka kama moto katika pori, na kutoa moshi muzito unaopanda juu katika anga.


Ninyi mumenikataa mimi. –Ni ujumbe wa Yawe.– Ninyi mumeniacha na kurudi nyuma. Kwa hiyo nimenyoosha mukono kwa kuwaangamiza. Nimechoka na kuwahurumia.


Watu wangu wametenda maovu mawili; wameniacha mimi ninayekuwa chemichemi ya maji ya uzima, wakajichimbia visima vyao wenyewe, visima vyenye nyufa, visivyoweza kuchunga maji.


Israeli, si wewe mwenyewe uliyejiletea hayo yote, kwa kuniacha mimi Yawe, Mungu wako, niliyekuwa ninakuongoza katika njia?


Uovu wako utakuazibu; na uasi wako utakuhukumu. Ujue na kutambua kwamba ni vibaya sana kuacha Bwana wako Yawe, Mungu wako, na kutokuwa na woga wangu ndani yako. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi.–


Enyi watu! Musikilize vile mimi Yawe ninavyosema: Nimekuwa kama vile jangwa au inchi yenye giza kubwa? Kwa nini basi watu wangu wanasema: Sisi tuko watu huru; hatutakurudilia!


Kweli wewe ni bingwa wa kutafuta wapenzi! Hata wanawake waovu unawafundisha njia zako.


Yawe anasema hivi: Babu zenu waliona kosa gani kwangu hata wakanigeuka na kuniacha, wakakimbilia miungu ya bure, hata nao wakakuwa watu bure?


kwa sababu ya uovu wote watu wa Israeli na Wayuda waliotenda, pamoja na wafalme na wakubwa wao, makuhani na manabii wao, na wakaaji wa Yerusalema.


Muwaite wapiga mishale waishambulie Babeli. Mupeleke kila mutu anayejua kuvuta upinde. Muuzunguke muji kusikuwe mutu yeyote atakayetoroka. Muulipize kadiri ya matendo yake yote; muutendee kama ulivyowatendea wengine, maana kwa kiburi ulinizarau mimi Yawe, Mutakatifu wa Israeli.


Lakini Israeli na Yuda hawakuachiliwa na Mungu wao, Yawe wa majeshi, ingawa inchi yao imejaa makosa mbele ya Mutakatifu wa Israeli.


Lakini ni nani wanayemukasirikisha? Mimi? Hata kidogo! Wanajikasirikisha wao wenyewe na kujifezehesha! –Ni ujumbe wa Yawe.


Lakini hawakunisikiliza wala kunitegea sikio, lakini wakazidi kufanya vichwa vyao kuwa vigumu na kuasi kuliko hata babu zenu.


Mimi Yawe nitaigusa mioyo ya Waisraeli kusudi wanirudilie, maana wamejitenga mbali nami kwa kuabudu sanamu zao za miungu.


Kwa kawaida wanaume wanawalipa makahaba, lakini wewe umewalipa wapenzi wako wote, ukiwahonga wakuje kwako toka pande zote upate kuzini nao.


Kweli wewe ni mutoto wa mama aliyemuchukia mume wake na watoto wake; wewe ni sawa na dada zako waliowachukia waume wao na watoto wao. Mama yako alikuwa Muhiti na baba yako alikuwa Mwamori.


Waisraeli wote wameiasi sheria yako, wamekuacha wakakataa kukutii. Kwa sababu tumekukosea, tumemwangiwa laana na viapo vilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, mutumishi wako.


Nitawaangamiza wote walioniacha mimi Yawe, wote walioacha kunitafuta na kuniuliza shauri.


Na sasa, enyi kizazi cha wenye zambi, mumesimama kwa pahali pa wazee wenu, kuongeza tena hasira kali ya Yawe juu ya Waisraeli.


“Mukuje kwangu ninyi wote munaosumbuka na kulemewa na mizigo mizito, nami nitawapumzisha.


Ninyi kikundi cha nyoka! Namna gani mutaweza kuepuka azabu ya jehenamu?


Yoane alipoona Wafarisayo wengi na Wasadukayo wakimufikia kwa kubatizwa, aliwaambia: “Ninyi kikundi cha nyoka! Ni nani aliyewaambia kwamba munaweza kuponyoka azabu ya Mungu inayokaribia?


Kwa maana wale wanaoshugulika na hali ya kimwili ni waadui za Mungu; hawatii sheria ya Mungu wala hawawezi kuitii.


Au tunataka kumuchokoza Bwana hata asikie wivu? Munafikiri kuwa sisi tuko na nguvu kuliko yeye?


Wakaenda kutumikia na kuabudu miungu mingine, ambayo hawakuijua mbele, wala Yawe hakukuwa amewapa.


Yawe akamwambia Musa: “Umekaribia sasa kuaga dunia, na kisha kufa kwako, watu wataanza kuniacha na kuendea miungu mingine ya inchi hiyo ambamo watakwenda kuishi. Wataniacha na kuvunja agano nililoagana nao.


Yawe aliona jambo hilo akawaacha; aliwakataa watoto wake, wanaume na wanawake.


Lakini ninyi mumekosa uaminifu kwake, ninyi sio watoto wake tena kwa sababu ya uovu, ninyi ni kizazi kiovu na kipotovu.


Sasa ninafurahi kwa ajili ya mateso ninayopata juu yenu. Kwa njia ya kuteseka kwangu kimwili, ninatimiza mateso yaliyomubakilia Kristo kwa ajili ya mwili wake, maana yake kanisa.


Kwa maana zambi zake zinazidi sana hata zimefika mbinguni na Mungu hakusahau mabaya yake.


Basi wakamulilia Yawe, wakisema: “Tumetenda zambi mbele yako, maana tumekuacha wewe Mungu wetu, tukatumikia Mabali.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ