Hivi ndivyo uovu wa wazao wa Yakobo utakavyoondolewa, hivi ndivyo zambi yake itakavyofutwa kabisa: ataziharibu mazabahu za miungu; mawe yake yatasagwasagwa kama chokaa. Sanamu za Ashera wala mazabahu za kufukizia ubani hazitabaki.
Moto wa kufua vyuma unawaka kwa nguvu, risasi inayeyukia humohumo katika moto; ni bure kuendelea kuwatakasa watu wangu, waovu hawawezi kuondolewa uchafu wao.
Ndimi zao ni kama mishale yenye sumu, hawachoki kudanganya; kila mutu anaongea vema na jirani yake, lakini anafanya mipango ya kumushambulia ndani ya moyo wake.
Nitaondoa kati yenu waasi na wale wanaonikosea; nitawaondoa katika inchi walikokaa kama wakimbizi, lakini hawataingia hata kidogo katika inchi ya Waisraeli. Halafu mutatambua kwamba mimi ni Yawe.
Kama vile watu wanavyokusanya feza, shaba, chuma, risasi na bati katika furu wapate kuzisafisha kwa moto, ndivyo kasirani na hasira yangu vitakavyowakusanya huko na kuwayeyusha.
Siku hiyo, hautapata haya kutokana na matendo yako ya kuniasi, maana nitawaondoa kati yako wale wanaojivuna na kujitukuza, nawe hautakuwa na kiburi tena kwenye mulima wangu mutakatifu.
Yeye atakuja kuhukumu kama mutu anayesafisha na kutakasa feza. Atawasafisha wazao wa Lawi, kama mutu anavyofua zahabu au feza, mpaka wamutolee Yawe sadaka zinazokubalika.
Yeye anashika lungo katika mikono yake kwa kupepeta ngano. Atakusanya ngano na kuitia katika gala yake, lakini atateketeza maganda katika moto usiozimika.”
Enyi mataifa, mushangilie watu wake, maana yeye analipiza kisasi damu ya watumishi wake, anawalipiza kisasi wapinzani wake, na kuitakasa inchi ya watu wake.