Isaya 1:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
21 Namna gani muji uliokuwa mwaminifu sasa umegeuka kuwa kahaba! Wakati mumoja sheria ya Mungu ilifuatwa kabisa, haki ilikaa ndani yake. Sasa, ni muji wa wauaji.
Kisha, viongozi wa watu wakakaa katika Yerusalema; watu wengine wote, wakapiga kura kati ya kila jamaa kumi kwa kuchagua jamaa moja itakayokaa katika Yerusalema, muji mutakatifu. Jamaa zingine tisa zikakaa katika miji yao mingine.
Lakini waovu hata wakipewa rehema, hawawezi kujifunza kutenda haki. Hata katika inchi ya usawa, wao bado wanatenda maovu, wala hawajali ukubwa wako wewe Yawe.
Shamba la mizabibu la Yawe wa majeshi ni taifa la Waisraeli, na mizabibu mizuri aliyoipanda ni watu wa Yuda. Yeye alitazamia watu wafuate sheria yake, akaona mauaji; alitazamia haki, alisikia kilio!
Mume akiachana na muke wake, naye muke akijiendea, na kuolewa na mwingine, mume yule anaweza kumurudilia muke huyo? Kufanya hivyo hakutaichafua inchi kabisa? Wewe Israeli, umefanya ukahaba na wapenzi wengi, sasa unataka kunirudilia mimi? –Ni ujumbe wa Yawe.–
Kama sivyo, nitamuvua nguo abaki uchi, nitamufanya akuwe sawa vile alivyozaliwa. Nitamufanya akuwe utupu sawa jangwa, akauke sawa inchi kavu. Nitamwua kwa kiu.
Yawe wa majeshi anasema hivi: Nitaurudilia Sayuni na kufanya makao yangu katika Yerusalema. Muji Yerusalema utaitwa “Muji Mwaminifu”, na mulima wa Yawe wa majeshi utaitwa “Mulima Mutakatifu”.
“Ewe Yerusalema, Ewe Yerusalema, wewe unayewaua manabii na wajumbe ambao Mungu anakutumia kwa kuwatupia mawe. Mara nyingi nilitaka kuwakusanya wakaaji wako kama vile kuku anavyokusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake, lakini ninyi hamukutaka!
Ni nani kati ya manabii ambaye babu zenu walikosa kumutesa? Waliwaua wale waliotabiri zamani habari za kuja kwa Mwenye Haki. Na sasa mumemutoa na kumwua.
Lakini ninyi mumefikia kwenye mulima Sayuni na kwenye muji wa Mungu Mwenye Uzima, ndio muji Yerusalema wa mbinguni, kunakokuwa maelfu na maelfu ya wamalaika.
Lakini uache kiwanja kinachokuwa inje ya hekalu, usikipime kwa maana kimetolewa kwa watu wa mataifa mengine watakaokanyaga muji mutakatifu kwa muda wa miezi makumi ine na miwili.
Halafu mumoja wa wale wamalaika saba walioshika vile vikombe saba akajongea na kuniambia: “Kuja nitakuonyesha namna gani yule kahaba mukubwa atakavyohukumiwa, ndio ule muji uliojengwa katikati ya mito mingi.