Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 1:20 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

20 Lakini mukikataa na kuniasi, mutaangamizwa kwa upanga. Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 1:20
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini wasipomutii, wanaangamia kwa upanga, na kufa kwa kukosa akili.


Kama ukikataa kuwaacha waondoke na ukiendelea kuwashikilia,


Lakini ole kwao watu waovu! Mambo yatawaendekea vibaya, maana yale waliyotenda yatawapata wao wenyewe.


Wanaume wenu wataangamia kwa upanga, watu wenu wenye nguvu watakufa katika vita.


Musome katika kitabu cha Yawe: Hakuna hata kiumbe kimoja kitakachokosekana, kila kimoja kitakuwa na mwenzake. Maana kinywa cha Yawe kimeamuru hivyo. Roho yake itawakusanya hao wote.


Kisha utukufu wa Yawe utafunuliwa, na watu wote pamoja watauona. Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe.


utapata furaha yako kwangu mimi Yawe, nitakupatia ushindi katika kila upinzani katika inchi, nitakulisha mali ya Yakobo, babu yako. Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe.


Nimewapangia kifo kwa upanga, ninyi wote mutanaswa kwa kuchinjwa! Maana, nilipowaita, hamukuniitikia; niliposema, hamukunisikiliza. Mulitenda maovu mbele yangu, mukachagua yale nisiyoyapenda.


Kwa sababu watu hawa wameyakataa maji ya Siloa yanayotiririka polepole, wakatetemeka mbele ya mufalme Resini na mufalme Peka mwana wa Remalia,


Lakini musiponisikiliza na mukiacha kuihesabu siku ya Sabato kama siku takatifu, musipoacha kubeba mizigo na kuingia nayo kupitia milango ya Yerusalema siku ya Sabato, basi nitawakisha moto katika milango yake, nao utateketeza nyumba zote nzuri za Yerusalema, wala hautazimika. –Ni ujumbe wa Yawe.


Nawe Yeremia utawaambia watu hawa kwamba: Yawe anasema hivi: Musikilize! Mimi ninaweka mbele yenu njia ya uzima na njia ya kifo.


Utawaambia kwamba: Yawe anasema hivi: Kama hamutanisikiliza na kufuata sheria zangu nilizowawekea,


wanauzunguka Yerusalema kama walinzi wanavyozunguka mashamba, kwa sababu watu wake wameniasi. –Ni ujumbe wa Yawe.


Tangaza katika inchi ya Misri, uijulishe huko Migidoli, uijulishe huko Nofi na Tapanesi. Uwaambie: Mukae tayari kabisa maana upanga utawaangamiza kila nafasi.


Nitawaletea upanga ambao utalipiza kisasi juu ya agano mulilovunja. Ninyi mutakimbilia katika miji yenu, lakini nitawaletea ugonjwa mukali na kuwatia katika mikono ya waadui zenu.


Nitawatawanya ninyi kati ya watu wa mataifa na kuchomoa upanga juu yenu. Inchi yenu itakuwa ni ukiwa na miji yenu uharibifu.


Kila mutu atakaa kwa amani chini ya miti ya tini na mizabibu yake, bila kutishwa na mutu yeyote. –Maneno haya yanatoka katika kinywa cha Yawe wa majeshi.


Mungu si mutu, hata aseme uongo, wala si mwanadamu, hata abadilishe nia yake! Ataahidi kitu na asikifanye, au kusema kitu asikitimize?


Na kwa njia hiyo watapata tumaini la uzima wa milele, ambalo Mungu asiyesema uongo alituahidi mbele ya mwanzo wa nyakati.


Lakini kama hamutasikiliza sauti ya Yawe, mukiasi amri yake, basi yeye atapambana nanyi pamoja na mufalme wenu.


Lakini kama mukiendelea kutenda maovu, mutaangamia ninyi wenyewe pamoja na mufalme wenu.”


Na Mungu ambaye ni utukufu wa Israeli hadanganyi, wala habadilishi wazo lake. Yeye si mwanadamu hata apate kubadilisha mawazo.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ