Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 1:18 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

18 Yawe anasema hivi: Mukuje basi, tukate shauri. Zambi zenu zikionekana kuwa nyekundu, zitakuwa nyeupe kama teluji; zikionekana kuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama sufu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 1:18
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hakuna mwamuzi kati yetu ambaye angetuamua sisi wawili.


Mimi ni mukosaji tangia kuzaliwa kwangu, mwenye zambi tangia tumbo la mama yangu.


Unitakase kwa hisopo, nikuwe safi, unisafishe, nikuwe mweupe pee.


Wakubwa wako ni waasi; wanashirikiana na wizi. Kila mumoja anapenda kituliro, na kukimbilia zawadi. Hawamupatii yatima haki yake, haki za wajane si kitu kwao.


Yawe yuko tayari kuanza mashitaki, anasimama kwa kuwahukumu watu wake.


Mungu anasema hivi: Enyi wakaaji wa mbali munyamaze munisikilize! Enyi mataifa mujitie moyo; mujitokeze na mujisemee, na mukuje tuende pamoja kwa hukumu.


Yawe, Mufalme wa Yakobo, anasema: Enyi miungu ya mataifa, mulete maneno yenu, mukuje mujitetee!


Nimezimisha makosa yako nayo yametoweka kama mawingu, nimefuta zambi zako, nazo zimepotea kama kunguku. Urudi kwangu maana mimi nimekukomboa.


Muteteaji wangu yuko karibu. Ni nani atakayepingana nami? Akuje tusambe naye. Adui yangu ni nani? Ajitokeze mbele basi.


Waovu waache njia zao mbaya, watu wabaya waachane na mawazo yao mabaya; wamurudilie Yawe apate kuwahurumia, wamwendee Mungu wetu maana atawasamehe.


Yawe anasema hivi: Babu zenu waliona kosa gani kwangu hata wakanigeuka na kuniacha, wakakimbilia miungu ya bure, hata nao wakakuwa watu bure?


Lakini mutu mwovu akiachana na uovu aliofanya, na kutenda mambo ya haki na ya ukweli, huyo atayaokoa maisha yake.


Zambi zake zote alizotenda hapo mbele hazitakumbukwa; yeye ametenda mambo yanayokuwa ya haki na mema, kwa hiyo hakika ataishi.


Musikilize mashitaki ya Yawe, enyi milima, musikilize enyi misingi imara ya dunia! Yawe yuko na maneno juu ya watu wake. Yeye atatoa mashitaki juu ya Waisraeli.


Na sawa ilivyokuwa desturi, Paulo akaingia katika nyumba ile. Kwa muda wa siku tatu za Sabato zilizofuatana juma kwa juma, akabishana na watu waliokuwa mule, akitumia Maandiko Matakatifu.


Na kila siku ya Sabato, Paulo alibishana na Wayuda na Wagriki katika nyumba ya kuabudia na kuwashinda.


Lakini Paulo alipokuwa akihubiri juu ya haki, juu ya kujizuiza na juu ya siku ya hukumu ya Mungu itakayokuja, Feliki akaogopa na kumwambia: “Kwa sasa unaweza kujiendea. Nitakuita tena nitakapopata wakati.”


Sheria ilitokea na kusababisha kuongezeka kwa makosa, lakini nafasi yoyote palipozidi zambi, neema ilizidi sana.


Nami nikamujibu: “Bwana wangu wewe ndiwe unayejua.” Naye akaniambia: “Hawa ndio wanaotoka katika mateso makubwa. Wamesafisha kanzu zao na kuzifanya kuwa nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo.


Sasa musimame palepale munapokuwa kusudi mimi na ninyi tuhukumiwe mbele ya Yawe, nami nitawahutubia juu ya matendo yake ya ajabu ambayo aliyatenda kwa kuwaokoa ninyi na babu zenu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ