Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 1:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Mujisafishe, mujitakase; muondoe matendo yenu maovu mbele yangu. Muache kutenda mabaya,

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 1:16
31 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe alituma manabii na waonaji kuionya inchi ya Israeli na ya Yuda akisema: “Mwache njia zenu mbaya mutii amri zangu na masharti yangu kufuatana na sheria nilizowapa babu zenu, na ambazo niliwapa ninyi kupitia kwa watumishi wangu manabii.”


Ninanawa mikono yangu kuonyesha kama sina kosa, na kuizunguka mazabahu yako, ee Yawe,


Basi, uache kusema mabaya, na kuepuka kusema uongo.


Achana na uovu, utende mazuri, nawe utaishi katika inchi siku zote;


Kutenda mambo ya haki na kufuata sheria ya Mungu kunamupendeza Yawe kuliko sadaka.


Usigeukie kuume wala kushoto; epusha muguu wako mbali na uovu.


Muondoke! Muondoke! Mutoke pale! Musiguse kitu chochote kichafu! Muondoke kule Babeli! Mujitakase, enyi munaobeba vyombo vya Yawe.


Basi Sasa, uende kuwaambia watu wa Yuda na wakaaji wa Yerusalema kwamba: Yawe anasema hivi: Mimi nimekwisha kukamata mipango juu yenu, na nimekusudia kuleta hasara juu yenu. Basi kila mumoja arudi kutoka katika njia mbaya, abadilishe mwenendo wake na matendo yake.


Wao waliwaambia hivi: Kila mumoja wenu aachane na mwenendo wake mwovu na matendo yake mabaya, kusudi mupate kuishi katika inchi ambayo Yawe amewapa ninyi na babu zenu tangu zamani kuwa urizi wenu milele.


Labda watayasikiliza na kila mumoja wao ataacha njia yake mbaya. Wakifanya hivyo, nitabadilisha nia yangu juu ya hasara niliyokusudia kuleta juu yao kwa sababu ya matendo yao maovu.


Niliwapelekea tena na tena watumishi wangu wote, ni kusema manabii wawaambie kila mumoja wenu aachane na mwenendo wake mwovu, abadilishe matendo yake na kuacha kuifuata na kuitumikia miungu mingine. Na kwamba mukifanya hivyo mutakaa katika inchi niliyowapa ninyi na babu zenu. Lakini ninyi hamukunitegea sikio wala hamukunisikiliza.


Wewe Yerusalema, usafishe maovu ya moyo wako, kusudi upate kuokolewa. Mpaka wakati gani utaendelea kuchunga maovu?


Muchukie mabaya, mupende mazuri, na kudumisha sheria ya Mungu katika tribinali. Labda Yawe wa majeshi atawarehemu watu wa kabila la Yosefu waliobaki.


Watu wote na nyama wavae gunia. Kila mutu amwombe Mungu na kumusihi kwa moyo. Kila mumoja aache uovu wake, aache kutenda kwa ukali.


Siku hiyo, kutatokea chemichemi ya kutakasa zambi na uchafu wa wazao wa Daudi na wakaaji wote wa Yerusalema.


Haya ndiyo mambo ambayo mimi Yawe niliyowaambia kupitia kwa manabii wa zamani, wakati Yerusalema ulikuwa umestawi na wenye wakaaji tele, na wakati ambapo kulikuwa wakaaji wengi katika miji ya kandokando yake na katika eneo la Negebu na mabonde ya Sefela.


Basi muonyeshe kwa njia ya matendo kwamba mumegeuka toka zambi zenu.


Basi sasa, unangojea nini? Simama ubatizwe na kuondolewa zambi zako, ukiomba kwa jina la Bwana.’ ”


Upendo wenu ukuwe pasipo udanganyifu. Muchukie chochote kinachokuwa kibaya, mushikamane na kinachokuwa chema.


Basi wapendwa wangu, kwa kuwa tumepewa ahadi hizi zote, tujitakase toka uchafu wote unaochafua mwili na roho na tujikaze kuwa watakatifu kabisa tukiishi katika kumuheshimu Mungu.


Mumukaribie Mungu, naye atawakaribia. Musafishe mikono yenu, ninyi wenye zambi! Mutakase mioyo yenu, ninyi wenye nia mbili!


Basi, mutupilie mbali matendo yote maovu na ya udanganyifu pamoja na wivu na masingizio ya kila namna.


Aepuke mabaya, atende mema, atafute amani na kuifuatilia.


Nami nikamujibu: “Bwana wangu wewe ndiwe unayejua.” Naye akaniambia: “Hawa ndio wanaotoka katika mateso makubwa. Wamesafisha kanzu zao na kuzifanya kuwa nyeupe katika damu ya Mwana-Kondoo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ