Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 1:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Munapoinua mikono yenu kwa kuomba, nitauficha uso wangu nisiwaone. Hata mukiomba sana sitawasikia, maana mikono yenu imejaa damu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 1:15
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kisha Solomono alisimama kwenye mazabahu ya Yawe, mbele ya Waisraeli wote, aliinua mikono yake juu,


Solomono alipomaliza kusema maombi hayo yote na ombi lake kwa Yawe, alisimama kutoka pale mbele ya mazabahu ya Yawe, pahali alipokuwa amepiga magoti akiinua mikono yake juu.


Magaribi, wakati wa kutoa sadaka ulipofika, nikasimama pahali pale nilipokuwa nimeikaa kwa huzuni nazo nguo zangu zimepasuka pamoja na koti, nikapiga magoti na kunyoosha mikono yangu kwa Yawe, Mungu wangu, na kuomba,


Vitisho vinamufikia kama vile mafuriko; usiku anapatwa na zoruba.


Kweli Mungu hasikilizi kilio cha bure; Mungu Mwenye Uwezo hajali kilio kile.


Muinue mikono kuelekea pahali patakatifu, na kumutukuza Yawe!


Kutoka kwa mukubwa wa waimbaji: kwa vyombo vyenye nyuzi. Mashairi ya Daudi.


Kama ningalikusudia maovu ndani ya moyo, Yawe hangalinisikiliza.


Musa akamwambia: “Mara tu nitakapotoka inje ya muji nitainua mikono na kumwomba Yawe. Ngurumo itakoma na hakutakuwa mvua ya mawe tena kusudi utambue kwamba dunia ni ya Yawe.


Halafu mutaniita lakini sitaitika; mutanitafuta kwa bidii lakini hamutanipata.


Macho ya kiburi, ulimi mudanganyifu, mikono inayoua wasiokuwa na kosa,


Bwana atawatakasa wanawake wa Sayuni toka uchafu wao na kusafisha damu iliyomwangika katika Yerusalema, kwa njia ya upepo wa hukumu na wa kuunguza.


Kweli wewe ni Mungu mwenye kufichama, Mungu wa Israeli, Mungu mwokozi.


Munafunga kula lakini munagombana na kupigana mangumi vikali. Mukifunga namna hiyo, maombi yenu hayatafika kwangu juu.


Mafungo ya kweli ni kugawanya chakula chako pamoja na wenye njaa, kuwakaribisha katika nyumba yako wamasikini wasiokuwa na makao, kuwavalisha wasiokuwa na nguo, bila kusahau kuwasaidia wandugu zenu.


Hata hivyo, ee Yawe, wewe ni Baba yetu. Sisi ni kama udongo, wewe ni mufinyanzi. Sisi wote ni kazi ya mikono yako.


Nitamungojea Yawe ambaye amejificha mbali na wazao wa Yakobo; nitamutumainia.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Nitaleta hasara juu yao ambayo hawataweza kuiepuka. Hata kama wakinililia namna gani, sitawasikiliza.


Hata wakifunga, sitayasikiliza maombi yao, na hata wakinitolea sadaka za kuteketeza kwa moto na sadaka zingine, mimi sitazikubali. Lakini nitawaangamiza kwa vita, njaa na ugonjwa mukali.


Nilisikia sauti kama ya mwanamuke anayezaa, malalamiko kama ya mwenye kuzaa mutoto wa kwanza. Ilikuwa sauti ya Yerusalema akipumuapumua kwa uchungu, na kuinyooshanyoosha mikono yake, akisema: Ole wangu! Wanakuja kuniua!


Ninyi mumewaua watu wengi katika muji huu, na kujaza barabara zake na watu waliouawa.


Wewe mwanadamu, watu hawa wamekubali mioyo yao itawaliwe na sanamu za miungu; miungu hiyo inawasukuma kutenda zambi. Nitakubali kuulizwa shauri nao?


Mataifa yatajua kwamba Waisraeli walikwenda katika uhamisho kutokana na makosa yao wenyewe waliyonikosea. Waliniasi, nami nikageuka wasipate kuniona, nikawatoa katika mikono ya waadui zao wakauawa.


Watakwenda na makundi yao ya kondoo na ngombe, kumutafuta Yawe; lakini hawataweza kumupata, kwa sababu amejitenga nao.


Wakati unakuja ambapo mutamulilia Yawe, lakini yeye hatawajibu. Atauficha uso wake wakati huo, kwa sababu mumetenda mambo maovu.


nikasema: Kwa sababu niliwaita nao hawakunisikiliza, basi, nao waliponiita, sikuwasikiliza.


“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munawafungia watu wengine njia ya kuingia katika Ufalme wa mbinguni. Ninyi wenyewe hamwingii mule na zaidi ya hii munawazuiza wale wanaotaka kuingia. [


“Tena munapoomba, musitumie maneno mengi yasiokuwa na maana kama vile wapagani wanavyofanya, kwa sababu wanawaza kama Mungu atawasikia kama wakisema maneno mengi.


Tunajua kwamba Mungu hasikilizi maombi ya wenye zambi, lakini anamusikiliza mutu yule anayemuheshimu na kufanya sawa anavyotaka.


Basi, ninataka watu waombe Mungu wakiinua mikono juu, ikiwa imetakaswa, nao wafanye vile bila kasirani wala ubishi.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ