Solomono alipomaliza kusema maombi hayo yote na ombi lake kwa Yawe, alisimama kutoka pale mbele ya mazabahu ya Yawe, pahali alipokuwa amepiga magoti akiinua mikono yake juu.
Magaribi, wakati wa kutoa sadaka ulipofika, nikasimama pahali pale nilipokuwa nimeikaa kwa huzuni nazo nguo zangu zimepasuka pamoja na koti, nikapiga magoti na kunyoosha mikono yangu kwa Yawe, Mungu wangu, na kuomba,
Musa akamwambia: “Mara tu nitakapotoka inje ya muji nitainua mikono na kumwomba Yawe. Ngurumo itakoma na hakutakuwa mvua ya mawe tena kusudi utambue kwamba dunia ni ya Yawe.
Mafungo ya kweli ni kugawanya chakula chako pamoja na wenye njaa, kuwakaribisha katika nyumba yako wamasikini wasiokuwa na makao, kuwavalisha wasiokuwa na nguo, bila kusahau kuwasaidia wandugu zenu.
Hata wakifunga, sitayasikiliza maombi yao, na hata wakinitolea sadaka za kuteketeza kwa moto na sadaka zingine, mimi sitazikubali. Lakini nitawaangamiza kwa vita, njaa na ugonjwa mukali.
Nilisikia sauti kama ya mwanamuke anayezaa, malalamiko kama ya mwenye kuzaa mutoto wa kwanza. Ilikuwa sauti ya Yerusalema akipumuapumua kwa uchungu, na kuinyooshanyoosha mikono yake, akisema: Ole wangu! Wanakuja kuniua!
Mataifa yatajua kwamba Waisraeli walikwenda katika uhamisho kutokana na makosa yao wenyewe waliyonikosea. Waliniasi, nami nikageuka wasipate kuniona, nikawatoa katika mikono ya waadui zao wakauawa.
“Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munawafungia watu wengine njia ya kuingia katika Ufalme wa mbinguni. Ninyi wenyewe hamwingii mule na zaidi ya hii munawazuiza wale wanaotaka kuingia. [
“Tena munapoomba, musitumie maneno mengi yasiokuwa na maana kama vile wapagani wanavyofanya, kwa sababu wanawaza kama Mungu atawasikia kama wakisema maneno mengi.