Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 1:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Sipendezwi na sikukuu zenu za mwandamo wa mwezi, pamoja na sikukuu zenu zingine. Zimekuwa muzigo muzito kwangu, nami nimechoka kuzivumilia.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 1:14
13 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

na wakati wa siku za Sabato, mwandamo wa mwezi na sikukuu zingine, pale sadaka za kuteketezwa kwa moto zilipotolewa kwa Yawe. Sheria ziliwekwa kuelekea hesabu ya Walawi walioagizwa kufanya kazi zile siku zote mbele ya Yawe.


Ole kwako Yerusalema, mazabahu ya Mungu, muji ambamo Daudi alipiga kambi yake! Miaka inakuja na kupita, na sikukuu zako zinaendelea kufanyika;


lakini mimi Mungu nitahuzunisha Yerusalema, ndani yake kutakuwa vilio na maombolezo, muji wenyewe utakuwa kama mazabahu.


Hamukuninunulia marasi kwa mali yenu, wala kunishibisha kwa mafuta za sadaka. Pahali pake zambi zenu zimekuwa muzigo kwangu, mumenichokesha kabisa kwa makosa yenu.


Mimi Yawe ninapenda watu wafuate sheria yangu; ninachukia unyanganyi na uovu. Nitawatunza watu wangu kwa uaminifu, nitafanya nao agano la milele.


Katika kila sikukuu ya mwandamo wa mwezi, na katika kila siku ya Sabato, wanadamu wote watakuja kuniabudu. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Basi, Isaya akamujibu: Musikilize basi, enyi watu wa ukoo wa Daudi! Haitoshi kuwachokesha watu hata sasa munataka kumuchokesha Mungu wangu vilevile?


Kwa hiyo wakati wa mavuno nitaitwaa ngano yangu, nitaiondoa divai yangu kwa wakati wake. Nitamunyanganya nguo zangu za sufu na kitani, ambazo zilitumika kuufunika uchi wake.


Wamevunja uaminifu kwa Yawe, wamezaa watoto wa haramu. Mwezi mumoja utatosha kwa kuwaangamiza, pamoja na mashamba yao.


Sasa basi, nitawagandamizia chini, kama gari lililojaa ngano.


Yawe anasema hivi: Ninachukia na kuzarau sikukuu zenu; siifurahii mikutano yenu ya kidini.


Kwa muda wa mwezi mumoja, nikaua wachungaji watatu wabaya. Tena uvumilivu wangu kwa kondoo ukaniishia, nao kwa upande wao, wakanichukia.


Mumemuchokesha Yawe kwa maneno yenu matupu. Hata hivyo, munasema: Tumemuchokesha namna gani? Mumemuchokesha munaposema: Yawe anawaona kuwa wazuri watu wanaotenda mabaya; tena anawapenda. Au munapouliza: Yuko wapi yule Mungu mwenye haki?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ