Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 1:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Musiniletee tena matoleo yenu yasiyokuwa na maana; ninachukizwa na sadaka yenu ya ubani. Muache kufanya sikukuu za mwandamo wa mwezi, Sabato na mikutano ya ibada; sikubali ibada zilizochanganyika na maovu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 1:13
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Mume wake akamwuliza: “Kwa nini unataka kumwona leo? Leo si sikukuu ya mwandamo wa mwezi wala Sabato.” Akamujibu: “Si neno.”


na wakati wa siku za Sabato, mwandamo wa mwezi na sikukuu zingine, pale sadaka za kuteketezwa kwa moto zilipotolewa kwa Yawe. Sheria ziliwekwa kuelekea hesabu ya Walawi walioagizwa kufanya kazi zile siku zote mbele ya Yawe.


Mara ngapi walimwasi kule katika jangwa, na kumuchukiza huko kwenye ukiwa!


Siku ya kwanza na siku ya saba mutakuwa na mukutano mutakatifu. Katika siku hizo mbili hamutaruhusiwa kufanya kazi yoyote isipokuwa kazi ya lazima ya kutayarisha chakula.


Sadaka ya mwovu ni kitu cha kuchukiza sana. Inachukiza zaidi akiitoa kwa nia mbaya.


“Ilinipasa kutoa sadaka zangu; leo hii nimekamilisha naziri yangu.


Katika kila sikukuu ya mwandamo wa mwezi, na katika kila siku ya Sabato, wanadamu wote watakuja kuniabudu. –Ni Yawe anayesema hivyo.


Lakini watu hawa wanafanya wanavyotaka: wananitolea sadaka ya ngombe na tena wanaua watu kwa kutambikia. Wananitolea sadaka ya mwana-kondoo na vilevile wanaua imbwa. Wananitolea sadaka ya unga na vilevile wanatolea damu ya nguruwe. Wanachoma ubani mbele yangu na kwenda kuabudu miungu ya uongo. Hao wamechagua kufuata njia zao wenyewe.


Amelibomoa hekalu lake kama kibanda katika bustani, ameharibu pahali pake pa kusanyiko. Amefanya sikukuu na siku ya Sabato visahauliwe kule Sayuni, kwa hasira yake kubwa amewakataa mufalme na makuhani.


Na sasa, enyi Waisraeli, Bwana wenu Yawe anawaambia hivi: Muendelee kuziabudu sanamu zenu za miungu, kama hamunisikilizi; lakini mutalazimishwa kuacha kulikufuru jina langu takatifu kwa sadaka na sanamu zenu.


Kwa hiyo wakati wa mavuno nitaitwaa ngano yangu, nitaiondoa divai yangu kwa wakati wake. Nitamunyanganya nguo zangu za sufu na kitani, ambazo zilitumika kuufunika uchi wake.


Mutoe amri watu wafunge kula chakula; muwaalike watu kuja kwa mukutano wa kidini. Mukusanye wazee na wakaaji wote wa inchi, katika nyumba ya Yawe, Mungu wenu, na mule mumulilie Yawe.


Mupige baragumu kule Sayuni! Mutoe amri watu wafunge kula; muwaalike kuja kwa mukutano wa kidini.


Miji yenu nitaiteketeza, pahali penu patakatifu nitapafanya jangwa na harufu zenu nzuri za sadaka sitazikubali.


Heri kungepatikana mutu mumoja kati yenu ambaye angefunga milango ya hekalu kusudi musiwashe moto usiokubaliwa kwenye mazabahu yangu! Sipendezwi nanyi na sitaikubali sadaka yoyote munayonitolea.


Tengeneza baragumu mbili kwa feza iliyofuliwa. Utatumia baragumu hizo wakati wa kuwaita watu na wakati wa kuvunja kambi.


Ibada wanayonifanyia ni ya bure, sababu mafundisho yao yanalingana na kanuni za watu tu.’ ”


“Ole kwenu, ninyi Wafarisayo! Munatoa fungu moja la kumi la vijani vya kukoleza chakula na kila namna ya mboga; lakini mumezarau haki na upendo wa Mungu. Mambo hayo ndiyo mulipaswa kushika pasipo kuacha mengine.


Kuelekea maonyo yanayofuata, mimi siwasifu. Kwa maana munapokusanyika, mikutano yenu haiwafalii, lakini inawaletea hasara.


Musihuzunishe Roho Mutakatifu wa Mungu; kwa maana Roho ni kitambulisho kilichowekwa juu yenu kwa kuhakikisha kwamba ninyi ni watu wake mpaka siku Mungu atakapowakomboa.


Ni kweli kwamba wengi kati yao wanahubiri habari za Kristo kwa wivu na ugomvi, lakini wengine wanahubiri katika nia nzuri.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ