Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Isaya 1:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Yawe anasema hivi: Uwingi wa sadaka zenu ni kitu gani kwangu? Nimechoka na sadaka zenu za kondoo wenye kuteketezwa na mafuta ya nyama wenu wenye kunona. Sipendezwi na damu ya ngombe dume, wala ya wana-kondoo, wala ya beberu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Isaya 1:11
23 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ee Yawe, Mungu wangu, umetufanyia maajabu mengi, na mipango yako juu yetu haihesabiki; hakuna yeyote anayekuwa kama wewe. Kama ningeweza kusimulia hayo yote, hesabu yake ingenishinda.


Sikukaripii kwa sababu ya sadaka zako; haujaacha kunitolea sadaka za kuteketezwa.


Uniokoe kutoka kosa la kumwanga damu, ee Mungu, Mungu mwokozi wangu, nami nitaimba kwa sauti kwamba umeniokoa.


Sadaka ya waovu ni chukizo kwa Yawe, lakini maombi ya watu wa usawa yanamufurahisha Mungu.


Sadaka ya mwovu ni kitu cha kuchukiza sana. Inachukiza zaidi akiitoa kwa nia mbaya.


Kutenda mambo ya haki na kufuata sheria ya Mungu kunamupendeza Yawe kuliko sadaka.


Kila siku wananitafuta, wanatamani kujua njia zangu, kama vile wao ni taifa linalotenda haki, taifa lisilosahau agizo la Mungu wao. Wanataka niamue kwa haki, na kutamani kuikaa karibu na Mungu.


Lakini watu hawa wanafanya wanavyotaka: wananitolea sadaka ya ngombe na tena wanaua watu kwa kutambikia. Wananitolea sadaka ya mwana-kondoo na vilevile wanaua imbwa. Wananitolea sadaka ya unga na vilevile wanatolea damu ya nguruwe. Wanachoma ubani mbele yangu na kwenda kuabudu miungu ya uongo. Hao wamechagua kufuata njia zao wenyewe.


Kwa nini kuniletea ubani kutoka Seba, na udi wa harufu nzuri kutoka inchi ya mbali? Sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto hazikubaliki, wala sadaka zenu zingine hazinipendezi.


Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Muongeze sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto juu ya sadaka zenu zingine, nanyi mujikulie nyama zile!


Maana kitu ninachotaka kwenu ni wema na si sadaka, kumujua Mungu na si kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto.


Wanapenda kutoa sadaka za nyama, kwa kusudi la kula nyama yake; lakini mimi Yawe sipendezwi hata kidogo. Mimi ninayakumbuka makosa yao; nitawaazibu kwa ajili ya zambi zao; nitawarudisha katika utumwa kule Misri.


Mutoe sadaka ya shukrani ya mikate isiyotiwa chachu. Mutangaze popote kwamba mumetoa kwa mapenzi; maana ndivyo munavyopenda kufanya! –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Yawe anasema hivi: Ninachukia na kuzarau sikukuu zenu; siifurahii mikutano yenu ya kidini.


Hata mukinitolea sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto na za vyakula, mimi sitakubali kuzipokea; na sadaka zenu za amani za nyama wanono mimi sitaziangalia kabisa.


Yawe atapendezwa nikimutolea maelfu ya kondoo dume, au mito elfu na elfu ya mafuta? Nimutolee muzaliwa wangu wa kwanza kwa ajili ya kosa langu, mutoto wangu wa kwanza kwa ajili ya zambi yangu?


Hagai akajibu na kusema hivi: Hivi ndivyo inavyokuwa kwa watu wa taifa hili mbele yangu –ni ujumbe wa Yawe– na kila kitu wanachofanya; hata vitu wanavyotoa kwenye mazabahu ni vichafu.


Uwaambie wakaaji wote wa inchi na makuhani hivi: Kwa muda wa miaka makumi saba iliyopita, ninyi mulikuwa mukifunga na kuomboleza katika mwezi wa tano na wa saba. Munazani mulifunga kwa ajili yangu?


Heri kungepatikana mutu mumoja kati yenu ambaye angefunga milango ya hekalu kusudi musiwashe moto usiokubaliwa kwenye mazabahu yangu! Sipendezwi nanyi na sitaikubali sadaka yoyote munayonitolea.


Kisha akawatuma watumishi wengine, akisema: ‘Mwende kuwaambia waalikwa kwamba karamu yangu iko sasa tayari. Nimechinja ngombe na nyama wenye kunona; vitu vyote viko tayari. Muwaambie wafike kwa karamu!’


Muende kujifunza maana ya Maandiko Matakatifu yanayosema: ‘Ninataka huruma, lakini si sadaka zenu.’ Kwa maana sikukuja kuwaita wenye haki kunifuata, lakini watenda mabaya.”


Halafu Samweli akamwambia: “Unazani kwamba Yawe anapendelea zaidi sadaka za kuteketezwa kwa moto na matoleo mengine, kuliko kuitii sauti yake? Hapana. Kumutii yeye ni bora kuliko matoleo na kumusikiliza kuliko kumutolea mafuta ya beberu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ