basi, nitawahamisha watu wangu, Waisraeli, kutoka inchi hii ambayo nimewapa; vilevile na nyumba hii ambayo niliyoitakasa kwa ajili ya jina langu, nitaitupilia mbali nami, na kuifanya kitu cha kuchekelewa na kuzarauliwa kati ya watu wa mataifa yote.
Katika mwaka wa tisa wa utawala wa Hoshea, mufalme wa Asuria aliuteka muji wa Samaria na kuwapeleka watu wa Israeli katika uhamisho mpaka Asuria. Wamoja kati yao akawaweka katika muji wa Hala, wengine karibu na muto Habori, muto Gozani na wengine katika miji ya Wamedi.
Nitalipiza kisasi mara mbili zaidi juu ya zambi zao na makosa yao, kwa sababu wameichafua inchi yangu na mizoga ya miungu yao yenye kuchukiza, wameijaza inchi yangu na hayo machukizo yao. –Ni ujumbe wa Yawe.
Niliwaleta katika inchi yenye mboleo, muyafurahie mazao yake na mema yake mengine. Lakini mulipofika tu, muliichafua inchi yangu; inchi niliyowapa ikuwe yenu, mukaifanya chukizo.
Lakini Danieli aliamua kutojichafua kwa kula chakula bora cha mufalme na kunywa divai yake. Kwa hiyo, alimwomba yule mukubwa amuruhusu asikule vitu hivyo na kujichafua.
Wanaigeukia miungu ya bure, wako kama upinde ulioregea. Waongozi wao watakufa kwa upanga, kwa sababu ya maneno yao ya kiburi. Kwa hiyo, watazarauliwa katika inchi ya Misri.
Wanapenda kutoa sadaka za nyama, kwa kusudi la kula nyama yake; lakini mimi Yawe sipendezwi hata kidogo. Mimi ninayakumbuka makosa yao; nitawaazibu kwa ajili ya zambi zao; nitawarudisha katika utumwa kule Misri.
Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Muke wako atakuwa kahaba katika muji, na wana wako na wabinti zako watauawa katika vita. Inchi yako itagawanywa na kupewa wengine, nawe mwenyewe utakufia katika inchi inayohesabiwa kuwa chafu; nao Waisraeli hakika watapelekwa katika uhamisho, mbali kabisa na inchi yao.
Lakini Petro akajibu: “Hapana, hata kidogo Ee Bwana! Mimi sijakula bado kitu chochote kisichoruhusiwa kukuliwa, wala chochote kinachohesabiwa kuwa kichafu.”
Kama vile Yawe alivyopendezwa kuwafanikisha na kuwafanya kuwa wengi, ni vile vile Yawe atapendezwa kuwaletea hasara na kuwaangamiza. Nanyi mutaondolewa katika inchi hiyo ambayo munakwenda kuirizi.
Yawe atawarudisha Misri kwa mashua, safari ambayo aliahidi kwamba hamungeifanya tena. Huko mutajaribu kujiuzisha kwa waadui zenu kuwa watumwa, lakini hakuna mutu atakayewanunua.”
Lakini kama vile Yawe, Mungu wenu, alivyotimiza mambo yote mema aliyowaahidi, ni vile vile anavyoweza kuwaletea maovu yote mpaka awaangamize wote kutoka inchi hii nzuri ambayo amewapa.