Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 9:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 Kwa vile wamekataa kumusikiliza, Mungu wangu atawatupilia; wao watatangatanga kati ya mataifa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 9:17
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Lakini Mikaya akamujibu: “Kama vile Yawe anavyoishi, kile Mungu wangu atakachoniambia, ndicho nitakachosema.”


Lakini wao waliendelea kuwachekelea wajumbe wa Mungu, wakayazarau maneno yake na kuwachekelea manabii wake mpaka kwa mwisho kasirani ya Yawe ikawaka juu ya watu wake hata hakukukuwa wa kuwaponyesha.


Sasa, Ee Mungu wangu, kumbuka wema wangu wote niliowatendea watu hawa.


Ninasikia watu wakinongonezana; kuna vitisho kila upande. Wanafanya shauri baya juu yangu, wanafanya mipango ya kuniua.


Anayeonywa mara nyingi na kuwa mugumu, ataangamia kwa rafla wala hatapata kupona.


Ingekuwa heri ungalizitii amri zangu! Halafu baraka zingekutiririkia kama muto, ungefanikiwa kwa wingi kama mawimbi ya bahari.


Basi, Isaya akamujibu: Musikilize basi, enyi watu wa ukoo wa Daudi! Haitoshi kuwachokesha watu hata sasa munataka kumuchokesha Mungu wangu vilevile?


Basi wataitwa “takataka za feza”, maana mimi Yawe nimewakataa.


Ninyi mumefanya mambo hayo yote. –Ni ujumbe wa Yawe.– Na hata niliposema nanyi tena na tena hamukunisikiliza. Nilipowaita hamukuitika.


Nitawafukuza ninyi mbali nami kama nilivyowatupilia mbali wandugu zenu, wote wa uzao wa Efuraimu.


Watakula, lakini hawatashiba, watazini, lakini hawatapata watoto, kwa sababu wameniacha mimi Yawe, na kufuata miungu mingine.


Watu wangu wameangamia kwa kutonijua, maana wewe kuhani umekataa mafundisho. Nimekukataa kuwa kuhani wangu. Kwa maana umeisahau sheria ya Mungu wako, nami vilevile nitawasahau watoto wako.


Ole kwao kwa sababu wameniacha! Maangamizi yawapate, maana wameniasi. Nilitaka kuwakomboa, lakini wanasema uongo juu yangu.


Naye Yawe akaniuliza: Amosi, unaona nini? Nami nikamujibu: Ninaona kikapu cha matunda yenye kuivya. Kisha Yawe akaniambia: Mwisho umewafikia watu wangu wa Israeli. Sitavumilia tena maovu yao.


Nitatoa amri, na kuwapepeta Waisraeli kati ya mataifa kama mutu anavyopepeta ngano kusudi niwatoshe wote wasiofaa.


Lakini mimi ninamutumainia Yawe, ninamutazamia Mungu mwenye kuniokoa; Mungu wangu atanisikiliza.


Musikuwe kama babu zenu. Manabii waliwaambia: Yawe anasema hivi: muachane na mienendo yenu miovu na matendo yenu mabaya. Lakini wao hawakunisikiliza wala hawakunitii. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Yesu akamwambia: “Usinishike, kwa sababu sijapanda bado kwa Baba. Lakini kwenda kwa wandugu zangu na kuwaambia kwamba ninapanda kwa Baba yangu anayekuwa Baba yenu vilevile, anayekuwa Mungu wangu na Mungu wenu vilevile.”


Toma akamujibu: “Bwana wangu na Mungu wangu!”


Wayuda wakaulizana hivi wao kwa wao: “Mutu huyu atakwenda wapi sisi tusipoweza kumwona? Ataenda kwa Wayuda waliosambazwa kati ya Wagriki na kuwafundisha Wagriki?


Na mutu yeyote atakayekataa kumusikiliza nabii yule, atatengwa mbali na taifa la Mungu na kuuawa.’


Ningaliwaangamiza kabisa na kuwafanya wasikumbukwe tena na mutu yeyote,


“Mimi leo ninaita mbingu na dunia zishuhudie juu yenu. Mutakapokuwa mukikaa katika inchi hiyo, mukipata watoto na wajukuu na kuwa wazee, kama mukianza kupotoka na kujifanyia sanamu katika umbo la kitu chochote, mukifanya uovu mbele ya Yawe, Mungu wenu, na kumukasirikisha, mara moja mutaangamia kabisa katika inchi ambayo munaenda kurizi huko ngambo ya muto Yordani. Hamutaishi huko muda murefu, lakini mutaangamizwa kabisa.


Yawe atawatawanya kati ya mataifa mengine, na ni wachache tu wenu watakaobakia huko ambako Yawe atawafukuzia.


Basi, kwa njia ya Yesu Kristo, Mungu wangu atatimiza mahitaji yenu yote kufuatana na uwingi na utukufu wa utajiri wake.


Barua hii inatoka kwangu mimi Yakobo, mutumishi wa Mungu na wa Bwana Yesu Kristo. Ninawasalimia ninyi watu wa makabila kumi na mawili waliosambazwa katika dunia.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ