Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 9:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Yawe anasema: Nilipowakuta Waisraeli walikuwa kama zabibu katika jangwa. Nilipowaona babu zenu, walikuwa bora kama matunda ya tini za kwanza. Lakini walipofika kule Bali-Peori, wakajitolea kwa kuabudu chukizo Bali, wakakuwa chukizo kama kile walichokipenda.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 9:10
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Tena, zaidi ya kufuata mwenendo mubaya wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Ahabu alimwoa Yezebeli binti ya Etibali mufalme wa Wasidoni. Akamutumikia na kumwabudu Bali.


na wakafukiza ubani kwenye mazabahu yote ya miungu ya uongo kwa kufuata desturi za mataifa ambayo yalifukuzwa na Yawe. Walimukasirikisha Yawe na matendo yao maovu,


Wote wanaoitengeneza wanafanana nayo, na hata vilevile wote wanaoitumainia.


“Lakini watu wangu hawakunisikiliza; Israeli hakunitaka kabisa.


Ni kitu gani kile kinachotoka katika jangwa kama munara wa moshi, kinachotoa harufu ya manemane na ubani, manukato yanayouzishwa na wachuuzi?


utukufu wake unatoweka kama ua linalonyauka; utukufu uliotawala katika bonde kwenye udongo muzuri utakuwa kama tini za mwanzo mbele ya wakati wa mavuno; mutu akiziona anazichuma na kuzikula mara moja.


Enyi watu wa Yuda, hesabu ya miji yenu ni sawasawa na hesabu ya miungu yenu. Na kama vile barabara zenu za Yerusalema zinavyokuwa nyingi, ndivyo mulivyojenga mazabahu ya haya, ni kusema ya kufukizia ubani kwa mungu Bali.


Ndani ya kikapu cha kwanza kulikuwa tini nzuri sana, kama vile tini za mavuno ya kwanzakwanza. Lakini ndani ya kikapu cha pili kulikuwa tini mbaya sana, mbaya hata hazifai kukuliwa.


Tangu ujana wetu, tendo hili la haya limeangamiza kila kitu babu zetu walichokitoshea jasho: makundi yao ya kondoo na ngombe, wana wao na wabinti zao.


Sherti tujilaze chini kwa ajili ya haya, na kujiachilia kufunikiwa na haya yetu. Tangu ujana wetu mpaka leo hii, sisi wenyewe, kama vile babu zetu, tumetenda zambi mbele ya Yawe, Mungu wetu, wala hatukumutii Yawe, Mungu wetu.


Yawe anasema hivi: Watu walioponyoka kuuawa, nilionyesha neema yangu kwao katika jangwa. Wakati Israeli alipotafuta kwenda kupumzika,


manabii wanatabiri mambo ya uongo, nao makuhani wanatafuta faida yao wenyewe; nao watu wangu wanaona jambo hilo kuwa sawa. Lakini mwisho wake utakapofika mutafanya nini?


Lakini waliniasi, hawakutaka kunisikiliza. Hakuna hata mumoja kati yao aliyetupilia mbali machukizo yale waliyoyapenda, wala hawakuachana na sanamu za miungu ya Misri. Basi, nikafikiri kwamba nitawamwangia kasirani yangu na kuitimiza hasira yangu juu yao wakiwa kulekule katika inchi ya Misri.


Israeli alipokuwa mutoto, nilimupenda. Kutoka Misri nilimwita mwana wangu.


Ni mimi niliyewachunga mulipokuwa katika jangwa, katika inchi iliyokuwa yenye kukauka.


Nitamulipiza kwa ajili ya siku alizoabudu sanamu za mungu Bali, kwa ajili ya muda alioutumia kuzifukizia ubani, akajipamba kwa pete zake na ushanga, na kuwaendea wapenzi wake, akanisahau mimi. –Ni ujumbe wa Yawe.


Lakini sitawaazibu wabinti zenu wanapofanya uzinzi, wala bibi-arusi wenu wanapofanya uasherati, maana, wanaume wenyewe ndio wanaofuatana na wazinzi, na kutambikia pamoja nao katika ibada za uzinzi. Watu hawa wenye kukosa akili hakika wataangamia!


Kama vile kundi la walevi, wanajizamisha wenyewe katika uzinzi; wanapendelea mambo ya haya kuliko heshima yao.


Mutoe sadaka ya shukrani ya mikate isiyotiwa chachu. Mutangaze popote kwamba mumetoa kwa mapenzi; maana ndivyo munavyopenda kufanya! –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Ole wangu! Mimi ninakuwa kama muvunaji kisha wakati wa mavuno; hakuna tini za kwanzakwanza ninazotamani. Ni kama wakati wa kuchuma zabibu: hakuna hata fungu moja la zabibu la kula!


Vishada hivyo vitakuwa ukumbusho kwenu. Kila mara mutakapoviona, mutakumbuka amri zangu zote na kuzifuata, kusudi musifuate mapenzi yenu na yale munayoona kwa macho yenu wenyewe.


Mazao yote ya kwanza ya matunda mabichi ya mashamba yao ambayo wataniletea mimi, yatakuwa yako. Kila mutu asiyekuwa muchafu katika jamaa yako anaweza kula.


Basi mulipata faida gani kwa kufanya mambo yale munayopata haya juu yake sasa? Maana mwisho yao ni kifo!


Yawe alikuta Waisraeli katika inchi ya jangwa, jangwa tupu zenye upepo mukali. Aliwalinda na kuwatunza. Aliwakinga kama mboni ya jicho lake.


Wakatambikia pepo ambazo hazikukuwa miungu, wakaendea miungu ambayo hawakuijua hata kidogo, miungu mipya iliyotokea kwa siku za karibu, ambayo wazee wao hawakuiheshimu hata kidogo.


Ninyi muliona kwa macho yenu mambo ambayo Yawe aliyafanya juu ya Bali-Peori. Yawe, Mungu wenu, aliwaangamiza watu wote kati yenu waliomwabudu huyo mungu Bali-Peori.


Siku hiyo wakamwita Gideoni “Yerubali” maana yake “Bali ajitetee”, maana aliibomoa mazabahu ya mungu Bali.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ