Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 9:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Musifurahi enyi Waisraeli! Musishangilie kama watu wa mataifa mengine; maana, mumekuwa wazinzi kwa kumwacha Mungu wenu. Mumefurahia malipo ya uzinzi, kwa kila nafasi ya kupepetea ngano.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 9:1
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Anayejitenga nawe, hakika ataangamia. Anayekukana, utamwangamiza.


hata mukiifanya ikomae siku hiyohiyo muliyoipanda na kuifanya ichanue asubui hiyohiyo, mavuno yenu yatatoweka siku hiyo ya hasara na maumivu yasiyoweza kuponyeshwa.


Uovu wako utakuazibu; na uasi wako utakuhukumu. Ujue na kutambua kwamba ni vibaya sana kuacha Bwana wako Yawe, Mungu wako, na kutokuwa na woga wangu ndani yako. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi.–


Yawe anasema: Tangu zamani wewe ulivunja nira yako, ulikata minyororo yako, ukasema: “Sitakutumikia”. Juu ya kila kilima kirefu na chini ya kila muti wa majani mabichi, ukalala machali kama kahaba.


Lakini kila kitu tulichoapa kufanya tutafanya: Tutamufukizia ubani malkia wa mbinguni na kumutolea sadaka ya kinywaji kama tulivyokuwa tunafanya sisi wenyewe na babu zetu, wafalme wetu na wakubwa wetu, katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalema. Kwa wakati huo tulikuwa na chakula tele, tulistawi na hatukuona hasara yoyote.


Wakaaji wa Edomu, ile inchi ya Uzi, mushangilie na kufurahi kwa sasa. Lakini kikombe hiki cha azabu kitawafikia vilevile. Mutakikunywa na kulewa, hata mutavaa uchi!


Lakini, ulitegemea uzuri wako, ukatumia sifa yako kwa kufanya uzinzi, ukifanya ukahaba na mutu yeyote anayepita.


Kweli wewe ni mugonjwa wa mapenzi. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Unafanya uzinzi bila kuona haya hata kidogo.


Ninyi munasema ndani ya mioyo yenu: Tutakuwa kama mataifa mengine, kama makabila ya inchi ingine na kuabudu miti na mawe. Hayo munayofikiri ndani ya mioyo yenu hayatafanikiwa hata kidogo.


Watu wote watajua kwamba mimi Yawe ndiye niliyeuchomoa upanga ndani ya mufuko wake na wala hautarudishwa tena ndani.


Wakaaji wa Samaria watatetemeka kwa sababu ya sanamu ya mwana-ngombe wa kule Beteli. Watu wake watamwombolezea mwana-ngombe yule, hata makuhani wanaomwabudu watamulilia; maana utukufu wa mwana-ngombe yule umeondolewa.


Nitamuvua nguo abaki uchi mbele ya wapenzi wake, wala hakuna mutu atakayeweza kunizuia.


Watu wangu wanaomba shauri kutoka kwa muti; kijiti chao cha kuaguza ndicho kinachowapa shauri. Nia ya kufanya uzinzi imewapotosha; wamefanya uzinzi kwa kufuata miungu mingine, wakaniacha mimi Mungu wao.


Matendo yao yanawazuia wasimurudilie Mungu wao. Wamejaa uzinzi ndani ya mioyo yao; hawanijui mimi Yawe.


Wamevunja uaminifu kwa Yawe, wamezaa watoto wa haramu. Mwezi mumoja utatosha kwa kuwaangamiza, pamoja na mashamba yao.


Kati ya mataifa yote katika ulimwengu, ni ninyi tu niliowachagua. Kwa hiyo nitawaazibu ninyi, kwa sababu ya uovu wenu wote.


Mutoe sadaka ya shukrani ya mikate isiyotiwa chachu. Mutangaze popote kwamba mumetoa kwa mapenzi; maana ndivyo munavyopenda kufanya! –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.–


Ninyi munashangilia juu ya muji wa Bure na kusema mumeuteka muji wa Nguvu kwa nguvu zenu wenyewe.


Nitazigeuza sikukuu zenu kuwa kilio, na nyimbo zenu za furaha kuwa maombolezo. Nitawavalisha ninyi wote magunia kwa huzuni na kunyoa vichwa vyenu upaa, kama kuomboleza kifo cha mutoto wa pekee. Na siku ya mwisho itakuwa ya uchungu mukubwa.


Lakini sasa munajivuna na kujisifu. Majivuno yote ya namna hii ni mabaya.


Basi, munisikilize sasa ninyi watajiri! Mulie na kuomboleza kwa sababu ya taabu itakayowapata.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ