Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 8:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Wanapanda upepo, watavuna zoruba! Mimea yao ya ngano inayokuwa katika mashamba haitatoa ngano yoyote. Na hata kama ikizaa, mazao yake yatakuliwa na wageni.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 8:7
22 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Halafu yakafuatwa na masuke mengine saba matupu, membamba na yaliyokaushwa na upepo mukali wa jangwa.


Basi, Puli mufalme wa Asuria akashambulia inchi ya Israeli, naye Menahemu akamupa kilo elfu makumi tatu na ine za feza kusudi amusaidie kuimarisha mamlaka yake juu ya inchi ya Israeli.


Wakati wa utawala wa Peka mufalme wa Israeli, Tigilati-Pileseri, mufalme wa Asuria, aliteka miji ya Iyoni, Abeli-Beti-Maka, Yanoa, Kadesi na Hazori, pamoja na inchi za Gileadi, Galilaya na Nafutali na kuwahamisha wakaaji wake kwenda Asuria.


Mimi nimeona kwamba wanaopanda uovu na ubaya wanavuna yaleyale.


Anayepanda ubaya atavuna hasara. Uwezo wake wa kutenda mabaya utavunjwa.


Aliishi maisha yake yote katika giza na huzuni, katika mahangaiko, magonjwa na hasira.


hata mukiifanya ikomae siku hiyohiyo muliyoipanda na kuifanya ichanue asubui hiyohiyo, mavuno yenu yatatoweka siku hiyo ya hasara na maumivu yasiyoweza kuponyeshwa.


Mbona munatumia feza zenu kwa ajili ya kitu kisichokuwa chakula? Kwa nini kutoa jasho lenu kwa kitu kisichoshibisha? Munisikilize mimi kwa uangalifu, nanyi mutakula vinavyokuwa vitamu, na kufurahia vinavyokuwa bora.


Yawe atakuja kama moto, na magari yake ya vita ni kama zoruba. Ataiacha hasira yake ifanye kazi yake kwa ukali, na maonyo yake yatimizwe kwa ndimi za moto.


Walipanda ngano, lakini walivuna magugu; wamejichokesha kwa bure. Kwa sababu ya hasira kali ya Yawe, watasikia haya juu ya mavuno yao.


Inchi yetu imepewa kwa wageni, nyumba zetu kwa watu wengine.


Atawafuata wapenzi wake, lakini hatawapata; atawatafuta, lakini hatawaona. Kwa hiyo atasema: Nitarudi kwa mume wangu wa kwanza; maana zamani nilikuwa na raha kuliko sasa.


Wageni wamenyonya nguvu zake, wala yeye mwenyewe hajui; imvi zimejaa juu ya kichwa chake, lakini yeye mwenyewe hana habari.


Watu wa Efuraimu wamepigwa, wamekuwa kama muti wenye muzizi wenye kukauka, hawatazaa watoto wowote. Hata kama wakizaa watoto, nitawaua watoto wao wanaowapenda.


Yawe hakasiriki upesi, lakini amejaa nguvu, Yawe hatawaachilia wenye makosa hata kidogo. Yawe anapopita, upepo mukali na zoruba vinatokea; mawingu ni mavumbi yanayonyanyuliwa na miguu yake.


Munapanda mbegu kwa wingi, lakini munavuna kidogo. Munakula, lakini hamushibi. Munakunywa divai, lakini hamutosheki. Munavaa nguo, lakini bado munasikia baridi. Mushahara wa mutumishi unakuwa kama umetumbukizwa katika mufuko uliotoboka.


Musidanganyike: Mungu hachekelewi. Chochote mutu atakachopanda, ndicho atakachovuna.


Anayepanda kwa kupendeza hali yake ya kimwili, atavuna matunda yanayotokana na hali ile, nayo ni lufu. Lakini anayepanda kwa kupendeza Roho Mutakatifu, atavuna matunda yanayotokana na Roho yule, nayo ni uzima wa milele.


“Taifa musilolijua litatwaa mazao yote ya inchi yenu na matunda ya jasho lenu, nanyi mutapondwa na kuteswa siku zote,


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ