Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 8:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Enyi watu wa Samaria, ninaichukia sanamu yenu ya mwana-ngombe. Hasira yangu inawaka juu yenu. Mutaendelea kuwa na makosa mpaka wakati gani?

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 8:5
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Sasa ninyi munazani munaweza kupinga ufalme wa Yawe ambao Daudi na wazao wake walipewa kwa sababu muko na jeshi kubwa na sanamu za zahabu za wana-ngombe, Yeroboamu alizowatengenezea kuwa miungu yenu!


Lakini nani anayeona makosa yake mwenyewe? Ee Mungu, unisamehe makosa nisiyoyajua.


“Enyi wajinga! Mpaka wakati gani mutapenda kuwa wajinga? Mpaka wakati gani wenye kuzarau watafurahia mazarau yao, na wapumbafu kuchukia maarifa?


Enyi watu wa mataifa muliobaki, mukusanyike pamoja mukuje! Ninyi mumekosa akili: ninyi munabeba sanamu za miti na kumwomba mungu asiyeweza kuokoa watu.


Nimeyaona machukizo yako: nimeona uzinzi wako na utongozaji wako, na uasherati wako usiousikilia haya, unaoufanya juu ya milima na katika mashamba. Ole kwako wewe Yerusalema! Mpaka wakati gani utabaki bila kutakaswa?


Wewe Yerusalema, usafishe maovu ya moyo wako, kusudi upate kuokolewa. Mpaka wakati gani utaendelea kuchunga maovu?


Halafu Wamoabu watapata haya kwa ajili ya mungu wao Kemosi, kama vile watu wa Israeli walivyopata haya kwa ajili ya kutegemea Beteli.


Wakaaji wa Samaria watatetemeka kwa sababu ya sanamu ya mwana-ngombe wa kule Beteli. Watu wake watamwombolezea mwana-ngombe yule, hata makuhani wanaomwabudu watamulilia; maana utukufu wa mwana-ngombe yule umeondolewa.


Pahali pa kutambikia juu ya vilima pa Aweni, pahali Waisraeli walipofanyia zambi, pataharibiwa. Miiba na michongoma vitaota katika mazabahu zao. Nao wataiambia milima: Mutufunike na vilima: Mutuangukie!


Waefuraimu wanaendelea kutenda zambi, wanajitengenezea sanamu za feza yenye kuyeyushwa, sanamu zinazotengenezwa kwa ufundi wao, zote zikiwa kazi ya wafundi. Wanasema: Muzitambikie! Wanaume wanabusu sanamu ya mwana-ngombe!


Ile sanamu inatoka Israeli, ni fundi ndiye aliyeitengeneza. Yenyewe si Mungu hata kidogo. Kweli! Sanamu ya mwana-ngombe ya Samaria itavunjwavunjwa!


Wale wanaoapa kwa mungu wa uongo wa Samaria na kusema “Kwa nafsi ya mungu wako ee Dani” au “Kwa nafsi ya mungu wa Beri-Seba”, wote wataanguka na hawatasimama tena hata kidogo.


Sanamu zake zote zitavunjwavunjwa, kila kitu kilichochumwa kitateketezwa kwa moto. Nitaharibu sanamu za miungu yake yote. Zililundikwa kutokana na mushahara wa ukahaba, nazo zitatumiwa tena kuwa mushahara wa ukahaba.


Katika siku zile wakajitengenezea sanamu ya mwana-ngombe, wakaitambikia na kufurahia kitu hicho walichojifanyia wao wenyewe.


Hasira yangu imewaka moto, inachoma mpaka chini kuzimu, itateketeza dunia na vinavyokuwa ndani yake, itaunguza misingi ya milima.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ