Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 8:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Walijiwekea wafalme bila ruhusa yangu, walijichagulia wakubwa ambao sikuwatambua. Wamejitengenezea miungu ya feza na zahabu, jambo ambalo litawaangamiza.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 8:4
20 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Basi, kisha kushauriana na wengine, akatengeneza sanamu mbili za zahabu. Kisha akawaambia watu: “Enyi watu wa Israeli, hii ndiyo miungu yenu iliyowatoa katika inchi ya Misri! Hakuna sababu ya kwenda Yerusalema kutoa sadaka kule.”


Tendo hili likakuwa zambi ambayo ilisababisha ukoo wa Yeroboamu ufutiliwe mbali na kuangamizwa.


Tena, zaidi ya kufuata mwenendo mubaya wa Yeroboamu mwana wa Nebati, Ahabu alimwoa Yezebeli binti ya Etibali mufalme wa Wasidoni. Akamutumikia na kumwabudu Bali.


Mwanadamu anaweza kujitengenezea miungu? Kweli hiyo si miungu hata kidogo!


Mutupilie mbali zambi mulizonitendea; mujipatie moyo na roho mupya. Enyi Waisraeli, mutakufa kwa sababu gani?


Mufalme Nebukadneza alitengeneza sanamu ya zahabu, yenye urefu wa metre makumi mbili na nane na upana wa metre tatu. Akaisimamisha katika bonde la Dura katika jimbo la Babeli.


Waefuraimu waliposema, watu wote walitetemeka; Waefuraimu walikuwa na uwezo mukubwa katika inchi ya Israeli, lakini walianza kumwabudu mungu Bali, wakajiletea kifo.


Kwa hasira yangu mimi nikawapa mufalme, kisha nikamwondoa kwa kasirani yangu.


Waefuraimu wanaendelea kutenda zambi, wanajitengenezea sanamu za feza yenye kuyeyushwa, sanamu zinazotengenezwa kwa ufundi wao, zote zikiwa kazi ya wafundi. Wanasema: Muzitambikie! Wanaume wanabusu sanamu ya mwana-ngombe!


Basi, nitafunga njia yake kwa miiba, nitamuzungushia ukuta, asipate njia ya kutokea inje.


Lakini Waisraeli wametupilia mambo mazuri. Kwa hiyo, sasa waadui watawafuatilia.


Lakini bwana akajibu: ‘Kweli ninawaambia: mimi siwajui ninyi.’ ”


“Mwenye nyumba atakapokwisha kusimama na kufunga mulango, ninyi mutabaki inje na kuanza kupiga hodi na kusema: ‘Bwana, utufungulie.’ Naye atawajibu: ‘Sijui munatokea wapi.’


Lakini atawaambia tena: ‘Sijui munatokea wapi. Mutoke karibu nami, ninyi wote watenda maovu!’


Mimi ni muchungaji mwema. Ninajua kondoo wangu na kondoo wangu wananijua,


Lakini sasa munamujua Mungu, au afazali tuseme kwamba sasa munajulikana naye. Basi namna gani mumerudilia tena vitu vinavyotawala dunia, visivyokuwa na uwezo na vikosefu, mukitaka kuwa watumwa tena?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ