Kwa hiyo, nitawafukuza toka katika inchi hii na kuwapeleka mpaka kwenye inchi ambayo ninyi wenyewe wala babu zenu hawakuijua. Kule mutaitumikia miungu mingine usiku na muchana, wala sitawasikilia ninyi huruma. –Ni ujumbe wa Yawe.
Zambi ya watu wa Yuda, haiwezi kufutikana, imeandikwa kwa kalamu ya chuma; kwa chongo ya almasi. Imechorwa ndani ya mioyo yao na kwenye pembe za mazabahu yao.
Pahali pa kutambikia juu ya vilima pa Aweni, pahali Waisraeli walipofanyia zambi, pataharibiwa. Miiba na michongoma vitaota katika mazabahu zao. Nao wataiambia milima: Mutufunike na vilima: Mutuangukie!