Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 8:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Wametafuta wapenzi kati ya watu wa mataifa, lakini mimi nitawakusanya. Na hapo watasikia uzito wa muzigo wa mufalme wa wakubwa.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 8:10
21 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Ni kwa sababu Yawe aliona taabu kubwa Waisraeli waliyopata maana hakukuwa mutu yeyote wa kuwasaidia.


Mufalme Salmanaseri wa Asuria alimushambulia; naye Hoshea akakuwa mutumishi wake na kumulipa kodi.


Lakini wakati mumoja Hoshea alituma wajumbe kwa mufalme wa Misri akiomba musaada; ndipo akaacha kulipa kodi kwa mufalme Salmanaseri wa Asuria kama vile alivyozoea kufanya kila mwaka. Salmanaseri alipoona hivi alimufunga Hoshea kwa minyororo na kumuweka katika kifungo.


Basi, Mungu wa Israeli akasukuma roho ya Puli, mufalme wa Asuria, (ambaye alijulikana vilevile kwa jina la Tiglati-Pileseri), akashambulia inchi yao na kuwapeleka watu wa kabila la Rubeni, la Gadi na nusu ya kabila la Manase kwa upande wa mashariki mpaka uhamisho kule Hala, Habori na Hara, pembeni ya muto Gozani, ambako wamekaa mpaka leo.


Maana alisema: Si kweli majemadari wangu ni wafalme?


Bila kutaka shauri langu, wanafunga safari kwenda Misri, kukimbilia ulinzi kwa mufalme wa Misri, kupata pahali pa kujificha katika inchi yake.


Kisha huyo jemadari akasimama, akalalamika na kusema kwa luga ya Kiebrania: “Musikilize maneno ya mufalme mukubwa, mufalme wa Asuria!


wakamwendea Yeremia, wakamwambia: Tafazali sikiliza maombi yetu na kutuombea kwa Yawe, Mungu wako, sisi wote tuliobaki, kwa maana tulikuwa wengi, lakini sasa tumebaki wachache tu, kama unavyoona.


Kwa kawaida wanaume wanawalipa makahaba, lakini wewe umewalipa wapenzi wako wote, ukiwahonga wakuje kwako toka pande zote upate kuzini nao.


Basi, mimi nitawakusanya wapenzi wako wote uliojifurahisha nao, wote uliowapenda na wote uliowachukia. Nitawakusanya toka pande zote wakushambulie. Nitawafunulia uchi wako wapate kuuona.


Kama vile watu wanavyokusanya feza, shaba, chuma, risasi na bati katika furu wapate kuzisafisha kwa moto, ndivyo kasirani na hasira yangu vitakavyowakusanya huko na kuwayeyusha.


Ingawa Ohola alikuwa muke wangu, lakini aliendelea kuwa muzinzi na kuwatamani wapenzi wake Waasuria.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Kutoka upande wa kaskazini nitamuleta Nebukadneza, mufalme wa Babeli, mufalme wa wafalme, akiwa na farasi, magari ya vita, waaskari wapanda-farasi na kundi kubwa, akuje kukushambulia.


Wewe, ee mufalme, mufalme wa wafalme! Mungu amekupa ufalme, uwezo, nguvu na utukufu!


Nitawaendea watu hawa wapotovu na kuwaazibu; watu wa mataifa watakusanyika kwa kuwashambulia, watakapoazibiwa kwa ajili ya zambi zao nyingi.


Watu wa Efuraimu wanachunga upepo, muchana kutwa wanafukuza upepo wa mashariki. Wanazidisha uongo na mateso, wanafanya mapatano na Asuria na kupeleka mafuta Misri.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Kisha muda kidogo nitazitikisa mbingu na dunia, bahari na inchi kavu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ