Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 7:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Wote wamewaka hasira kama furu, na wanawaangamiza watawala wao. Wafalme wao wote wameanguka, wala hakuna anayeniomba musaada.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 7:7
27 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

akatawala kwa pahali pake. Huo ulikuwa mwaka wa tatu wa utawala wa mufalme Asa wa Yuda.


Simuri alipoona kwamba muji umekamatwa, akaingia katika munara, ndani ya nyumba ya kifalme, akaichoma kwa moto, naye akakufia mule.


Watu wa kundi lililomutambua Omuri, wakawazidia nguvu wale waliomutambua Tibuni mwana wa Ginati. Tibuni akakufa na Omuri akakuwa mufalme.


Kisha akaamuru: “Muwakamate wakiwa wazima.” Wakawakamata watu makumi ine na wawili wakawaua karibu na kisima cha “Kambi ya Wachungaji”. Hakuna aliyebaki hata mumoja.


Basi, barua ilipowafikia, waliwatwaa hao wana wa mufalme na kuwakata vichwa wote makumi saba. Waliweka vichwa vyao katika vikapu na kumupelekea Yehu kule Yezereheli.


Salumu mwana wa Yabesi alimwasi, akamupiga mbele ya watu na kumwua, kisha akatawala kwa pahali pake.


Menahemu mwana wa Gadi aliondoka Tirza kwenda Samaria, na kule akamupiga Salumu mwana wa Yabesi, kisha akatawala kwa pahali pake.


Peka mwana wa Remalia, ambaye alikuwa mukubwa wa waaskari wa Pekahia, alishirikiana na watu wengine makumi tano kutoka Gileadi, akamwua Pekahia katika chumba cha ndani cha nyumba ya mufalme kule Samaria na kuwa mufalme kwa pahali pake.


Katika mwaka wa makumi mbili wa utawala wa Yotamu mwana wa Uzia mufalme wa Yuda, Hoshea mwana wa Ela alimwasi Peka mwana wa Remalia na kumwua, kisha akatawala kwa pahali pake.


Yehu akatwaa upinde wake na kutupa mushale ambao ulipenya mabega ya Yoramu na kuchoma moyo wake, naye akakufa palepale ndani ya gari lake.


naye Yehu akawaambia: “Mumutupe chini!” Wakamutupa chini na damu yake ikasambaa juu ya ukuta na kwenye farasi. Yehu akapitisha farasi na gari lake juu ya maiti yake


Waovu wanapenda kukasirika; hawamwombi musaada anapowafunga.


Hao wanaotenda maovu hawajui kitu? Wanatafuna watu wangu kama mikate, wala hawajali Yawe.


Lakini ewe taifa la Yakobo, haukuniabudu mimi; enyi watu wa Israeli, mulichoka nami!


Wewe unakuja kuwasaidia wanaotenda haki kwa furaha, wanaokukumbuka na kufuata njia zako. Ulitukasirikia tulipokuwa wenye zambi; sisi tumeasi kwa muda murefu.


Hakuna hata mumoja anayekuja kukuomba; hakuna anayejishugulisha kukutafuta. Wewe unauficha uso wako mbali nasi, umetuacha tufungwe na maovu yetu.


Hata hivyo, ee Yawe, wewe ni Baba yetu. Sisi ni kama udongo, wewe ni mufinyanzi. Sisi wote ni kazi ya mikono yako.


Yawe atakata katika Israeli kichwa na mukia, tawi la mingazi na nyasi, kwa muda wa siku moja tu.


Nilitafuta kati yao mutu mumoja atengeneze ukuta na kusimama juu ya nafasi iliyobomoka mbele yangu, kusudi ailinde inchi na kunizuia nisiiharibu, lakini sikumupata hata mumoja.


Umetuazibu kama ilivyoandikwa katika Sheria ya Musa, lakini mpaka sasa, ee Yawe, Mungu wetu, hatukuomba musamaha wako kwa kuziacha zambi zetu na kutambua uaminifu wako.


Yuko wapi sasa mufalme wenu awaokoe? Wako wapi wale wakubwa wenu wawalinde? Ninyi ndio mulioomba: Utupatie mufalme na wakubwa watutawale.


Nitarudi mahali pangu na kujitenga nao mpaka watambue kosa lao na kunirudilia. Taabu zao zitawafundisha wanitafute.


Kiburi cha Waisraeli kinawashuhudia wao wenyewe, hawanirudilii mimi Yawe, Mungu wao; wala hawanitafuti kwa ajili ya matukio hayo yote.


Wananililia, lakini si kwa moyo. Wanagaagaa na kujikatakata juu ya vitanda vyao, kusudi nisikilize maombi yao kwa kupata ngano na divai; lakini wanaendelea kuniasi.


Walijiwekea wafalme bila ruhusa yangu, walijichagulia wakubwa ambao sikuwatambua. Wamejitengenezea miungu ya feza na zahabu, jambo ambalo litawaangamiza.


Ole wao wanaopanga kutenda maovu, wanaolala usiku wakikusudia mabaya! Mara tu kunapopambazuka, wanayatimiza maana wako na uwezo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ