Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 7:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Wanamufurahisha mufalme, lakini ni waovu; wanawafurahisha wakubwa, lakini ni wanafiki.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 7:3
16 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati ule, yule mutumishi aliyetumwa kwenda kwa Mikaya, akamwambia: “Manabii wengine wote kwa pamoja, wamemutabiria mufalme ushindi. Tafazali, nawe vilevile ufanye kama wao, umutabirie mazuri.”


Basi, Ahabu akakusanya manabii yapata mia ine, akawauliza: “Niende au nisiende kushambulia Ramoti-Gileadi?” Nao wakamujibu: “Kwenda! Yawe atakupatia ushindi.”


Wako wapi manabii waliokutabiria wakisema: Mufalme wa Babeli hatakushambulia wewe wala inchi hii?


manabii wanatabiri mambo ya uongo, nao makuhani wanatafuta faida yao wenyewe; nao watu wangu wanaona jambo hilo kuwa sawa. Lakini mwisho wake utakapofika mutafanya nini?


Ndimi zao ni hatari kama pinde; wameimarika kwa ajili ya uongo na si kwa ajili ya haki. Wanaendelea kutenda uovu kisha uovu, wala hawanitambui mimi. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Lakini ninyi mumepanda uovu, ninyi mumevuna ubaya; mumekula matunda ya uongo wenu. Wewe Israeli ulitegemea nguvu zako mwenyewe, na wingi wa waaskari wako.


Kuapa, uongo, mauaji, wizi na uzinzi vinatokea humo. Umwangaji wa damu unafuatana kwa mufululizo.


Efuraimu ameteswa, haki zake zimetwaliwa; maana alikusudia kufuata mambo isiyokuwa na maana.


Kwenye sikukuu ya mufalme, waliwalewesha sana wakubwa wake; naye mufalme akashirikiana na watu wa ovyoovyo.


Ninyi munafuata mufano mubaya wa mufalme Omuri na mufano mubaya wa jamaa ya mwana wake, Ahabu, na mumefuata mashauri yao. Kwa hiyo nitawaletea maangamizi, na kila mutu atawazarau. Watu watawachekelea kila pahali.


Wote ni wafundi wa kutenda maovu; waongozi na waamuzi wanaomba kituliro. Wakubwa wanaonyesha wazi nia zao mbaya, nao wanashirikiana pamoja kwa kuzitimiza.


Nao wanajua kwamba Sheria ya Mungu inasema kwamba watu wanaotenda maneno haya wanastahili kufa. Lakini hata hivi wanaendelea, si kuyafanya tu, lakini kukubaliana na wale wanaoyatenda.


Manabii wa uongo ni watu wa dunia, ndiyo maana wanasema mambo ya kidunia nao watu wa dunia wanawasikiliza.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ