Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 7:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Hawafikiri hata kidogo kwamba mimi ninayakumbuka maovu yao yote. Sasa maovu yao yamewabana. Yote waliyotenda yako mbele yangu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 7:2
33 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Macho ya Mungu yanachunguza mienendo ya watu; yeye anaziona hatua zao zote.


Mwovu anawaza ndani ya moyo wake: “Mungu amesahau; ameficha uso wake, haoni kitu!”


Usikumbuke zambi na makosa ya ujana wangu; unikumbuke kwa kadiri ya wema wako, kwa ajili ya uzuri wako, ee Yawe.


“Mufikiri vizuri jambo hili, enyi musionijali, kama sivyo nitawaangamiza, wala hakuna atakayewaokoa.


Mataifa yameanguka katika shimo walilochimba, miguu yao imenaswa kwenye wavu waliotega.


Maovu yetu umeyaweka mbele yako; zambi zetu za siri ziko wazi mbele yako.


Ngombe anamufahamu mwenye naye, punda anajua kibanda cha bwana wake; lakini Waisraeli hawajui, watu wangu, hawaelewi!


Ee Yawe, walipotaabika walikutafuta, walikuomba musaada ulipowaazibu.


Hakuna anayeweza kuwaza au kuwa na akili na kufikiri na kusema: Kipande cha muti huo nilikikonga moto; tena nikachoma mikate juu ya makaa yake, nikachoma nyama, nikakula. Basi, sehemu iliyobaki namna gani nitatengeneza nayo sanamu ambayo ni chukizo na kuabudu hicho kipande cha muti?


Katika karamu zao, hapakosekani vinubi, zeze, ngoma, filimbi na divai. Lakini hawajali matendo ya Yawe, wala kutambua kazi za mikono yake.


Yawe anasema hivi juu ya watu hawa: Kweli wamependa sana kutangatanga, wala hawakujizuia; kwa hiyo mimi Yawe sipendezwi nao. Sasa nitayakumbuka makosa yao, na kuwaazibu kwa ajili ya zambi zao.


Maana, mimi ninayaona matendo yao yote, hakuna hata moja linalofichama mbele yangu. Maovu yao yote ni wazi mbele yangu.


Zambi ya watu wa Yuda, haiwezi kufutikana, imeandikwa kwa kalamu ya chuma; kwa chongo ya almasi. Imechorwa ndani ya mioyo yao na kwenye pembe za mazabahu yao.


Uovu wako utakuazibu; na uasi wako utakuhukumu. Ujue na kutambua kwamba ni vibaya sana kuacha Bwana wako Yawe, Mungu wako, na kutokuwa na woga wangu ndani yako. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi.–


Wewe unapanga kwa hekima na unafanya maajabu; njia za watu wote ziko wazi mbele yako, unamulipa kila mumoja kadiri ya njia zake na matendo yake.


Wewe Yuda, hayo yote yamekupata kwa ajili ya mwenendo na matendo yako. Hiyo ndiyo hasara inayokufikia, tena ni yenye uchungu; yamepenya mpaka ndani ya moyo wako.


Juu ya matambiko ambayo ninyi na babu zenu, wafalme wenu na wakubwa wenu, pamoja na wanainchi wote, mulitoa katika miji ya Yuda na katika barabara za Yerusalema, munazani Yawe amesahau au hakumbuki?


Kwa hiyo, Bwana wetu Yawe anasema hivi: Wote wataweza kuziona zambi zenu. Kila mutu atajua jinsi munavyokuwa na makosa. Kila kitendo munachotenda kinaonyesha zambi zenu. Ninyi mutapata azabu nami nitawatia katika mikono ya waadui zenu.


Watu wa Efuraimu wanachunga upepo, muchana kutwa wanafukuza upepo wa mashariki. Wanazidisha uongo na mateso, wanafanya mapatano na Asuria na kupeleka mafuta Misri.


Lakini yatakayowapata watu yatawapata makuhani; nitawaazibu kwa sababu ya mwenendo wao, nitawalipiza matendo yao wenyewe.


Nyuma ya siku mbili atatupatia tena uzima. Nyuma ya siku tatu atatufufua kusudi tuweze kuishi pamoja naye.


Wanapenda kutoa sadaka za nyama, kwa kusudi la kula nyama yake; lakini mimi Yawe sipendezwi hata kidogo. Mimi ninayakumbuka makosa yao; nitawaazibu kwa ajili ya zambi zao; nitawarudisha katika utumwa kule Misri.


Yawe anasema hivi: Uovu wao wote ulianzia Gilgali; kule ndiko nilipoanza kuwachukia. Kwa sababu ya uovu wa matendo yao, nitawafukuza toka katika nyumba yangu. Sitawapenda tena. Wakubwa wao wote ni waasi.


Ninyi mumezama katika uovu, kama ilivyokuwa kule Gibea. Mungu atayakumbuka makosa yao, na kuwaazibu kwa ajili ya zambi zao.


Yawe, utukufu wa Yakobo, ameapa: Hakika, sitayasahau matendo yao maovu.


Simama, uende Ninawe, ule muji mukubwa, uukaripie. Maana uovu wake umenifikia.


Lakini ninawaonya kwamba musipotimiza ahadi yenu, mutakuwa mumemutendea Yawe zambi; mujue kwa hakika kwamba mutaazibiwa.


Hakuna kitu chochote kinachofichwa kitakachokosa kuvumbulikana wala hakuna siri itakayokosa kujulikana.


Kwa hiyo musihukumu mutu mbele ya wakati uliopangwa; mungojee mpaka Bwana atakaporudia. Yeye ndiye atakayeonyesha wazi katika mwangaza mambo yote yaliyofichwa katika giza na kufunua nia za siri za watu. Halafu kila mutu atapokea sifa anayostahili toka kwa Mungu.


Wangekuwa na hekima wangejua kwa nini walishindwa, wangeweza kuelewa mwisho wao utakuwa namna gani.


Hakuna kitu kinachoweza kufichwa mbele ya Mungu, lakini vitu vyote vinafunuliwa na viko wazi mbele ya macho yake, yeye tutakayemutolea hesabu ya maneno yetu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ