Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 7:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Wanaigeukia miungu ya bure, wako kama upinde ulioregea. Waongozi wao watakufa kwa upanga, kwa sababu ya maneno yao ya kiburi. Kwa hiyo, watazarauliwa katika inchi ya Misri.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 7:16
32 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kila mumoja anamudanganya mwenzake; anabembeleza lakini ni kwa moyo wa unafiki.


Ee Yawe, ukomeshe midomo hiyo ya kudanganya, na ndimi hizo zinazojigamba.


Wao wanasema: “Kwa ndimi zetu tutashinda; tuko na midomo, nani anayeweza kututawala?”


Hao hawana huruma yoyote ndani ya moyo; wamejaa maneno ya kujivuna.


Atanipelekea musaada toka mbinguni na kuniokoa, atawafezehesha hao wanaonishambulia. Mungu atanionyesha wema na uaminifu wake!


Kwa vinywa vyao wanatukana mbingu; kwa ndimi zao wanajitapa katika dunia.


Hawakuambatana naye kwa moyo, hawakukuwa waaminifu kwa agano lake.


Lakini waligeuka na kufanya mabaya kama babu zao; wakayumbayumba kama upinde usiokuwa imara.


Watu wa Yerusalema wamejikwaa, watu wa Yuda wameanguka, kwa sababu wanamupinga Yawe kwa maneno na matendo, wakizarau utukufu wake kati yao.


Kisha, watu wakasema: Tuende tufanye shauri baya juu ya Yeremia, maana hatukosi makuhani wa kutufundisha. Vilevile hatukosi watu wenye hekima wa kutushauria na manabii wa kututangazia ujumbe wa Mungu! Mukuje tumushitaki kufuatana na maneno yake mwenyewe, wala tusiyatilie maana mambo yote anayosema.


Pamoja na hayo yote, Yuda, dada mudanganyifu wa Israeli hakunirudilia kwa moyo wote, lakini kwa unafiki tu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Maana Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kama vile hasira yangu na kasirani yangu ilivyowapata wakaaji wa Yerusalema, ndivyo kasirani yangu itakavyowapata ninyi, kama mutakwenda Misri. Mutakuwa kitu cha kutukaniwa, kitisho, laana na haya. Hamutaona tena nafasi hii.


Bwana wetu Yawe anasema hivi: Utakunywa toka kikombe cha dada yako; kikombe kikubwa na kirefu. Watu watakuchekelea na kukuzarau; na kikombe chenyewe kimejaa.


Hata walipokuwa kati ya mataifa walilikufuru jina langu takatifu, hata watu wakasema hivi juu yao: Hawa ndio wale watu wa Yawe, lakini wamelazimishwa kuondoka katika inchi yake!


Huyo atasema maneno ya kujivuna mbele ya Mungu Mukubwa na kuwatesa watakatifu wake. Atajaribu kubadilisha sikukuu na sheria zao, na watakatifu watatiwa katika mikono yake kwa muda wa miaka mitatu na nusu.


Basi, watarudi katika inchi ya Misri; watatawaliwa na mufalme wa Asuria, kwa sababu wamekataa kunirudilia.


Watu wangu wamekusudia kuniacha mimi, wakiitwa kusimama wapande juu, hakuna hata mumoja anayeweza.


Lakini Yawe anasema hivi: Nitakutendea nini, ee Efuraimu? Nikufanyie nini, ee Yuda? Upendo wenu kwangu ni kama ukungu wa asubui, kama umande unaotoweka upesi.


Ole kwao kwa sababu wameniacha! Maangamizi yawapate, maana wameniasi. Nilitaka kuwakomboa, lakini wanasema uongo juu yangu.


Hawatakaa katika inchi ya Yawe. Watu wa Efuraimu watarudi katika utumwa kule Misri. Watakula vyakula vichafu kule Asuria.


Hawatamutolea Yawe sadaka ya divai, wala hawatamufurahisha kwa sadaka zao. Chakula chao kitakuwa kama cha kilio, wote watakaokikula watajichafua. Kitakuwa chakula cha kuwashibisha tu, hakitafaa kuletwa katika nyumba kwa Yawe.


Mutakapoyakimbia maangamizi ya inchi yenu, Misri itawakaribisha ninyi kwake, lakini makaburi yenu yanawangoja kule Memufisi. Michongoma itaota katika vyombo vyenu vya feza, miiba itajaa katika mahema yenu.


Yawe anasema hivi: Maneno yenu yamekuwa muzigo kwangu. Hata hivyo munasema: Tumesema nini juu yako?


Ninyi mumesema: Kumutumikia Mungu hakuna faida. Kuna faida gani kuyatii maagizo ya Yawe wa majeshi, au kujaribu kumwonyesha kwamba tumekosa mbele yake kwa kutembea kama watu wanaoomboleza?


“Ninawaambia wazi kwamba kwa Siku ya hukumu, watu watasamba kila neno lisilokuwa na maana walilosema.


Udongo wenye mawe pahali mbegu zilipoanguka ni mufano wa watu wanaosikia neno na kulipokea kwa furaha, lakini halizami ndani yao kama mizizi. Wanaliaminia kwa muda mufupi tu, nayo majaribu yanapowafikia, wanaliacha.


Hivi vilevile ulimi ni kiungo kidogo cha mwili, lakini unaweza kujivunia mambo makubwa sana. Muangalie, moto kidogo inaweza kuchoma pori kubwa sana!


Kwa maana mutu yule mwenye haki aliishi kati ya watu wabaya, akiona na kusikia kila siku mambo yaliyochukiza roho yake ya haki.


Yule nyama akapewa uwezo wa kusema maneno ya kiburi ya kumutukana Mungu. Naye akapewa mamlaka ya kufanya kazi yake kwa muda wa miezi makumi ine na miwili.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ