Lakini Yawe aliwarehemu na kuwaonea huruma. Aliwaangalia kwa wema kwa sababu ya agano lake na Abrahamu, Isaka na Yakobo. Hakuwaangamiza wala hajawaachilia hata kidogo mpaka leo.
Ni wewe uliyesema maneno haya kwa njia ya Roho Mutakatifu kwa kinywa cha mutumishi wako babu yetu mukubwa Daudi: ‘Kwa nini mataifa wanafanya fujo, na kwa nini watu wanafanya mipango ya ovyo?
Ijapokuwa wanamujua Mungu, hawamutukuzi wala kumushukuru kama vile anavyostahili. Lakini mawazo yao yaligeukia mambo ya ovyo ovyo, na mioyo yao isiyokuwa na ufahamu ilibaki katika giza.