Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 7:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Ole kwao kwa sababu wameniacha! Maangamizi yawapate, maana wameniasi. Nilitaka kuwakomboa, lakini wanasema uongo juu yangu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 7:13
42 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Watu wa Israeli ni watumishi wako na watu wako uliwakomboa kwa uwezo wako na mukono wako wenye nguvu.


Hao ndio waliomwambia Mungu: “Achana nasi!” Na “Wewe Mungu Mwenye Uwezo unaweza nini juu yetu?”


Aliwaokoa katika mikono ya waliowachukia; aliwaokoa kutoka nguvu za waadui zao.


Ole watoto waasi, wanaotimiza mipango yao na si mipango yangu, wanaofanya mapatano kinyume cha mapenzi yangu! –Ni ujumbe wa Yawe.– Kweli, wanalundika zambi juu ya zambi.


Bila kutaka shauri langu, wanafunga safari kwenda Misri, kukimbilia ulinzi kwa mufalme wa Misri, kupata pahali pa kujificha katika inchi yake.


Ole kwao wale wanaokwenda Misri kuomba musaada! Wanategemea farasi, wanategemea wingi wa magari ya vita na nguvu za waaskari wao wapanda-farasi. Lakini hawamutegemei Mutakatifu wa Israeli, wala hawamwombi Yawe shauri!


Enyi watu wa Yakobo zaifu kama mududu, enyi Waisraeli, musiogope! Nitawasaidia. –Ni ujumbe wa Yawe.– Mukombozi wenu ni yule Mutakatifu wa Israeli.


Yawe aliyewaumba enyi watu wa Yakobo, yeye aliyewafanya enyi watu wa Israeli, anasema hivi: Musiogope, maana mimi nimewakomboa; nimewaita kwa jina lenu nanyi ni wangu.


Tumekuasi na kukukana, ee Yawe, tumekataa kukufuata, ewe Mungu wetu. Tunasema maneno ya kutesa na uasi, katika mioyo yetu tunatunga na kutoa maneno ya uongo.


Maana alisema juu yao: Hakika, hawa ni watu wangu; watoto wangu ambao hawatanidanganya. Basi yeye akakuwa Mwokozi wao.


Yawe anasema hivi juu ya watu hawa: Kweli wamependa sana kutangatanga, wala hawakujizuia; kwa hiyo mimi Yawe sipendezwi nao. Sasa nitayakumbuka makosa yao, na kuwaazibu kwa ajili ya zambi zao.


mumepotoka, mumeyahatarisha maisha yenu. Maana mulinituma kwa Yawe, Mungu wenu, mukiniambia: Utuombee kwa Yawe, Mungu wetu kwamba kitu chochote Yawe, Mungu wetu, atakachosema, utuambie, nasi tutatimiza.


Tulijaribu kuuponyesha Babeli, lakini hauwezi kupona. Muuache, tujiendee, kila mumoja katika inchi yake. Hukumu yake ni kubwa sana inafika mpaka katika mawingu.


Nitawafukuza ninyi mbali nami kama nilivyowatupilia mbali wandugu zenu, wote wa uzao wa Efuraimu.


Taji tuliojivunia imeanguka. Ole kwetu maana tumetenda zambi!


Ole kwako, ole kwako Yerusalema! –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe.– Kisha kufanya hayo yote


Kwa nini munarudiliarudilia mezali hii katika inchi ya Waisraeli: Wababa wamekula matunda mabichi ya mizabibu, lakini ni meno ya watoto wao ndiyo yanaumizwa!


Lakini ninyi munasema: Matendo ya Yawe si sawa! Musikilize sasa, enyi Waisraeli: Ninachofanya mimi si sawa? Munachofanya ninyi ndicho kisichokuwa sawa.


Kweli, kondoo walisambazwa, wakatangatanga juu ya milima na vilima. Kondoo walisambazwa katika dunia yote, na hakukukuwa mutu aliyejali juu yao wala kuwatafuta.


Lakini kadiri nilivyozidi kuwaita, ndivyo walivyozidi kwenda mbali nami; waliendelea kuyatambikia Mabali, na kuvifukizia ubani sanamu za miungu.


Wamevunja uaminifu kwa Yawe, wamezaa watoto wa haramu. Mwezi mumoja utatosha kwa kuwaangamiza, pamoja na mashamba yao.


Kila mara nikitaka kurudishia watu wangu hali yao ya mbele, ninapotaka kuwaponyesha Waisraeli, uovu wa watu wa Efuraimu unafunuliwa, matendo mabaya ya Samaria yanajitokeza. Wao wanaongozwa na udanganyifu, mwizi anabomoa nyumba; inje katika barabara wanyanganyi wanashambulia.


Wanamufurahisha mufalme, lakini ni waovu; wanawafurahisha wakubwa, lakini ni wanafiki.


Hata kama wakilea watoto, sitamwacha hata mumoja wao muzima. Ole kwao, nitakapowaacha peke yao!


Kwa vile wamekataa kumusikiliza, Mungu wangu atawatupilia; wao watatangatanga kati ya mataifa.


Kisha Yona akawaelezea kwamba alikuwa anamukimbia Yawe. Kusikia hayo, watu hao wakazidi kuogopa, wakamwambia: Kwa sababu gani umefanya vile?


Basi, Yona akasimama kwa kukimbilia Tarsisi, mbali na uso wa Yawe. Akaenda mpaka katika muji wa Yofa ambapo alikuta mashua moja iko tayari kwenda Tarsisi. Alilipa bei ya safari, akapanda ndani ya mashua, akasafiri pamoja na watu wengine kwenda Tarsisi, mbali na uso wa Yawe.


Watajiri wa miji ni watesaji wakali kabisa, wakaaji wake wanasema uongo, kila neno wanalosema ni udanganyifu.


Mimi niliwatoa katika inchi ya Misri, niliwakomboa kutoka katika utumwa, niliwapatia Musa, Haruni na Miriamu kwa kuwaongoza.


“Ewe Yerusalema, Ewe Yerusalema. Wewe unaua manabii na kuwatupia mawe wale ambao Mungu anakutumia. Mara nyingi nilitaka kuwakusanya wakaaji wako kama vile kuku anavyokusanya vitoto vyake chini ya mabawa yake, lakini ninyi hamukutaka!


Mukumbuke kwamba ninyi mulikuwa watumwa huko Misri na Yawe, Mungu wenu, aliwakomboa; ndiyo maana leo ninawaamuru hivyo.


Tukisema kwamba hatukutenda zambi, tunamugeuza Mungu kuwa mwongo, na ukweli wa neno lake si ndani yetu.


Kisha nikaangalia tena, nami nikasikia tai mumoja akiruka juu sana katika anga akisema hivi kwa sauti kubwa: “Ole! Ole! Ole kwa wakaaji wa dunia, kutakaposikilika mulio wa zile baragumu zingine ambazo wamalaika watatu wanatayarisha kupiga!”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ