Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 6:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Lakini mulivunja agano langu kama mulivyofanya katika muji wa Adamu; kule walikosa uaminifu kwangu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 6:7
18 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Yawe akamwuliza: “Nani aliyekuambia kwamba uko uchi? Umekula tunda la muti nililokuamuru usikule?”


Basi, mwanamuke alipoona kwamba muti ule ni muzuri kwa chakula, unavutia macho, na kwamba unafaa kwa kupata hekima, akachuma tunda lake, akakula, akamupa mume wake aliyekuwa pamoja naye, naye vilevile akakula.


Walikataa kutii masharti yake; hawakushika agano alilofanya na babu zao, walizarau maonyo yake, waliabudu sanamu zisizokuwa na maana hata wao wenyewe hawakukuwa na maana tena, walifuata desturi za mataifa yaliyowazunguka: walizarau amri za Yawe; wala hawakuzishika.


Nimeficha makosa yangu kama wengine? Nimekataa kutambua zambi zangu?


Tunasikia nyimbo za sifa kutoka miisho ya dunia, nyimbo za kumusifu Mungu anayekuwa mwenye haki. Lakini mimi ninasema: Ninakonda, kweli ninakonda. Ole kwangu mimi! Wadanganyifu wanaendelea kuwa wadanganyifu, udanganyifu wao unazidi kuwa mubaya zaidi.


Watu wameichafua dunia maana wamezivunja sheria za Mungu, wamegeuka mbali na masharti yake, wamelivunja agano lake la milele.


Haujapata kuyasikia wala kuyajua hata kidogo; tangu zamani masikio yako hayakuyasikia. Nilijua kwamba wewe ni mudanganyifu, na kwamba wewe ni mwasi tangu kuzaliwa.


Mimi nilizani kwamba nyuma ya kufanya hayo yote, atanirudilia. Lakini hakunirudilia. Yuda, dada yake mudanganyifu, alishuhudia hayo yote.


Agano hili halitakuwa kama lile nililofanya na babu zao nilipowatoa kwa mukono wangu kutoka Misri; agano hilo walilivunja, ingawa mimi nilikuwa Bwana wao.


Watu waliovunja agano langu na kukataa kufuata masharti ya agano walilofanya mbele yangu, nitawafanya kama yule mwana-ngombe waliyemukata sehemu mbili na kupita katikati ya vipande vile.


Kweli, watu wa Israeli na watu wa Yuda, wamekosa kabisa uaminifu kwangu. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Kwa hiyo, Yawe wa majeshi anasema hivi: Nitawasafisha na kuwapima kwa moto kama vile chuma. Ni namna gani zaidi ya kuwatendea hawa watu wangu waovu?


Wamevunja uaminifu kwa Yawe, wamezaa watoto wa haramu. Mwezi mumoja utatosha kwa kuwaangamiza, pamoja na mashamba yao.


Mupige baragumu! Adui anakuja kama tai kuishambulia nyumba ya Yawe, kwa sababu wamelivunja agano langu na kuiasi sheria yangu.


Lakini kifo kilitawala tangia wakati wa Adamu mpaka wakati wa Musa, hata juu ya wale wasiofanya zambi kwa kuvunja amri, sawa vile Adamu alivyofanya. Naye ni mufano wa yule aliyengojewa kuja.


Nitakapowapeleka katika inchi inayotiririka maziwa na asali, kama vile nilivyowaapia babu zao, nao watakula, watashiba na kunenepa, halafu watageukia miungu mingine na kuitumikia. Watanizarau na kuvunja agano langu.


Agano lile halitakuwa sawa na lile nililofanya na babu zao siku nilipowakamatia kwenye mukono na kuwaondoa toka inchi ya Misri. Kwa sababu hawakushika lile agano, kwa hiyo vilevile sikuwashugulikia. Ni Bwana wetu Mungu anayesema hivyo.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ