Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 6:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Maana kitu ninachotaka kwenu ni wema na si sadaka, kumujua Mungu na si kutoa sadaka za kuteketezwa kwa moto.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 6:6
24 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

“Nawe Solomono mwana wangu, umujue Mungu wa baba yako, na umutumikie kwa moyo wako wote na kwa nia nzuri; yeye Yawe anachunguza mioyo na anafahamu mipango na mafikiri ya mwanadamu. Ukimutafuta yeye, utamwona; lakini ukimwacha, atakutupilia mbali milele.


Sikukaripii kwa sababu ya sadaka zako; haujaacha kunitolea sadaka za kuteketezwa.


Kutenda mambo ya haki na kufuata sheria ya Mungu kunamupendeza Yawe kuliko sadaka.


Fikiri mbele ya kusema, wala usikuwe mwepesi kwa kusema neno lolote mbele ya Mungu, kwa maana Mungu yuko mbinguni na wewe uko katika dunia. Kwa hiyo usiseme maneno mengi.


Yawe anasema hivi: Uwingi wa sadaka zenu ni kitu gani kwangu? Nimechoka na sadaka zenu za kondoo wenye kuteketezwa na mafuta ya nyama wenu wenye kunona. Sipendezwi na damu ya ngombe dume, wala ya wana-kondoo, wala ya beberu.


Mafungo ninayotaka mimi ni haya: kuwafungua waliofungwa bila haki, kuziondoa kamba za utumwa, kuwaacha huru wanaogandamizwa, na kuvunja kabisa mambo yote ya kitumwa!


Aliwapatia haki wamasikini na wakosefu, na mambo yake yaliendeka vizuri. Si hivi ndivyo kunijua mimi? –Ni ujumbe wa Yawe.–


Maana, siku nilipowaondoa babu zenu katika inchi ya Misri, sikuwaambia kitu wala kuwapa amri yoyote juu ya sadaka za kuteketezwa na sadaka zingine.


Basi, akasema kwa sauti: Angalia Babeli, muji mukubwa nilioujenga kwa nguvu zangu ukuwe makao yangu ya kifalme na kwa ajili ya utukufu wangu!


Enyi Waisraeli, mumurudilie Yawe, Mungu wenu. Mumejikwaa kwa sababu ya uovu wenu.


Nitafanya agano na nyama wa pori, ndege pamoja na vyote vinavyotambaa, kusudi wasikuumize. Nitaondoa upinde, upanga na silaha za vita katika inchi, na kukufanya uishi kwa usalama.


Musikilize maneno ya Yawe, enyi Waisraeli. Yawe anawashitaki wakaaji wa inchi hii. Hakuna tena uaminifu wala wema katika inchi; hakuna anayemujua Mungu katika inchi hii.


Wanapenda kutoa sadaka za nyama, kwa kusudi la kula nyama yake; lakini mimi Yawe sipendezwi hata kidogo. Mimi ninayakumbuka makosa yao; nitawaazibu kwa ajili ya zambi zao; nitawarudisha katika utumwa kule Misri.


Yawe anasema hivi: Ninachukia na kuzarau sikukuu zenu; siifurahii mikutano yenu ya kidini.


Nimwendee Yawe na kitu gani, nipate kumwabudu Mungu anayekuwa juu? Nimwendee na sadaka za kuteketezwa kwa moto, nimutolee mwana-ngombe wa mwaka mumoja?


Mungu amekuonyesha yanayokuwa mema, ewe mwanadamu; kitu Yawe anachotaka kwako ni hiki: kutenda mambo ya haki, kupenda kuwa na huruma, na kuishi kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wako.


Mungejua maana ya Maandiko haya Matakatifu, yanayosema: ‘Ninataka huruma, lakini si sadaka zenu,’ hamungehukumu watu hawa wasiokuwa na kosa.


Heri wale wanaokuwa na huruma, maana Mungu atawahurumia!


Muende kujifunza maana ya Maandiko Matakatifu yanayosema: ‘Ninataka huruma, lakini si sadaka zenu.’ Kwa maana sikukuja kuwaita wenye haki kunifuata, lakini watenda mabaya.”


Na mutu anapaswa kumupenda Mungu kwa moyo wake wote, kwa akili yake yote na kwa nguvu yake yote, naye anapaswa kumupenda mwenzake kama vile anavyojipenda mwenyewe. Mambo hayo ni bora zaidi kuliko kumutolea Mungu nyama za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine zote.”


Hao wote waliotoka Misri walikuwa wametahiriwa, lakini wale wote waliozaliwa katika safari kule katika jangwa kisha kutoka Misri, walikuwa bado hawajatahiriwa.


Sisi tunatambua kwamba tunamujua Mungu ikiwa tunashika amri zake.


Basi kila mutu anayeungana naye hafanyi tena zambi; lakini kila mutu anayefanya zambi hakumwona wala kumujua.


Halafu Samweli akamwambia: “Unazani kwamba Yawe anapendelea zaidi sadaka za kuteketezwa kwa moto na matoleo mengine, kuliko kuitii sauti yake? Hapana. Kumutii yeye ni bora kuliko matoleo na kumusikiliza kuliko kumutolea mafuta ya beberu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ