Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 6:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Ndiyo maana ninawashambulia kwa njia ya manabii, nimewaangamiza kwa maneno yangu, hukumu yangu inajitokeza kama mapambazuko.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 6:5
35 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Sizani kama utafanya hivyo, kuwaua watu wa haki pamoja na waovu, kutendea watu wa haki sawa na waovu. Hapana, haiwezekani! Mwamuzi wa dunia yote hataacha kutenda mambo yanayokuwa sawa!”


Lakini Ahiya alipomusikia anaingia kwenye mulango, alisema: “Karibu ndani muke wa Yeroboamu. Lakini mbona unajigeuza kuwa mutu mwingine? Niko na ujumbe usiokuwa muzuri kwako!


Basi Elia wa kijiji cha Tisibe katika jimbo la Gileadi akamwambia mufalme Ahabu: “Kama vile Yawe, Mungu wa Israeli, ambaye ninamutumikia, anavyoishi, hakutakuwa umande wala mvua mpaka nitakapotoa amri.”


Ahabu alipomwona Elia, alisema: “Hakika ni wewe unayetaabisha Waisraeli?”


Basi, mutu yeyote atakayepona kuuawa kwa upanga wa Hazaeli, Yehu atamwua, na yeyote atakayepona kuuawa kwa upanga wa Yehu, Elisha atamwua.


Akamwambia mufalme: “Yawe anasema hivi: ‘Kwa sababu ulituma wajumbe kuomba shauri kwa Bali-Zabubu mungu wa Ekuroni sawa vile hakuna Mungu katika Israeli ambaye ungemwomba shauri, basi, hautashuka katika kitanda ambacho umepanda juu yake. Hakika utakufa.’ ”


Nabii Elia akamupelekea mufalme Yoramu barua hii: “Yawe, Mungu wa Daudi babu yako, anakulaani kwa sababu haukufuata mwenendo wa Yosafati baba yako, au wa Asa mufalme wa Yuda.


Hataponyoka giza la kifo. Ndimi za moto zitakausha vichipukizi vyake, maua yake yatapeperushwa na upepo.


Kwa hiyo munisikilize, enyi wenye ujuzi. Mungu hawezi kufanya uovu hata kidogo; Mungu Mwenye Uwezo hawezi kufanya kosa.


Ninatetemeka kwa kukuogopa wewe; nimejaa hofu kwa sababu ya maamuzi yako.


Ataifanya haki yako iangae kama mwangaza wa jua muchana kati.


Atawaamulia wamasikini kwa haki na kutetea haki za wakosefu katika inchi. Kwa neno lake dunia itaazibiwa, kwa pumzi yake waovu watauawa.


Yawe anasema: Piga kelele, wala usijizuize; ulalamike kwa sauti kubwa kama baragumu. Uwatangazie watu wangu makosa yao, uwaambie wazao wa Yakobo zambi zao.


Leo nimekupa mamlaka juu ya mataifa na falme, ukuwe na mamlaka ya kuongoa na kubomoa, mamlaka ya kuharibu na kuangamiza, mamlaka ya kujenga na ya kupanda mbegu.


Na tangu leo, ninakufanya kuwa imara kama muji unaozungukwa na kuta, kama munara wa chuma na kama ukuta mugumu sana wa shaba. Utakuwa na nguvu juu ya inchi yote, juu ya wafalme wa Yuda, wakubwa wake, makuhani wake na watu wake wote.


Nawe utawajibia hivi: Yawe anasema hivi: Nitawalewesha wakaaji wote wa inchi hii; wafalme wanaotawala kwa kiti cha kifalme cha Daudi, makuhani, manabii na wakaaji wote wa Yerusalema.


Neno langu ni kama moto. –Ni ujumbe wa Yawe!– Neno langu ni kama nyundo inayovunja mawe vipandevipande.


Yawe wa majeshi anasema hivi: Kwa sababu wao wamesema jambo hilo, sasa nitayafanya maneno niliyokupa wewe Yeremia kuwa moto. Nao watu hawa watakuwa kuni, na moto huo utawateketeza.


Kwa hiyo, utoe unabii juu yao! Tabiri ewe mwanadamu!


Kama vile almasi inavyokuwa ngumu kuliko mawe mengine, ndivyo nilivyokufanya ukuwe na kichwa kigumu. Usiwaogope wala usitishwe na nyuso zao, maana hao ni watu waasi.


Wewe mwanadamu! Uwaombolezee watu wengi wa Misri. Uwapeleke chini kwenye inchi ya wafu pamoja na mataifa mengine yenye nguvu, waende huko pamoja na wanaoshuka chini kwa wafu.


Maono hayo yalikuwa kama maono niliyoyaona wakati Mungu alipokuja kuuangamiza Yerusalema. Vilevile yalifanana na maono niliyoyaona karibu na muto Kebari. Nikaanguka uso mpaka chini.


Lakini Yawe anayekuwa katika muji ule ni mwenye haki, yeye hatendi jambo lolote baya. Kila siku asubui anatangaza hukumu yake, kila kunapopambazuka anaitimiza. Lakini waovu hawana haya hata kidogo.


Musa alipoona jambo hilo akashangaa sana, naye aliposogea karibu kusudi aangalie, akasikia sauti ya Bwana ikisema:


Lakini wewe ni mugumu na mwenye moyo usiotaka kugeuka. Kwa hiyo unajiwekea azabu kubwa siku Mungu atakapoonyesha kasirani yake na hukumu yake ya haki.


Mupokee wokovu kama vile kofia ya chuma ya kuwalinda, na Neno la Mungu kama upanga munaopewa na Roho.


Kwa maana Neno la Mungu ni lenye uzima, na lina nguvu; ni kali kupita upanga unaokata ngambo mbili. Linapenya hata linatenga moyo na roho na hata viungo na ubongo. Nalo linatambua nia na mawazo ya mutu.


Alikuwa ameshika nyota saba katika mukono wake wa kuume. Ndani ya kinywa chake mulitoka upanga wenye makali ngambo zote mbili, uso wake ulingaa sana kama jua wakati linapopiga vikali sana.


Basi ugeuke toka zambi zako, kwa maana kama si vile nitakuja kwako upesi, nami nitapigana na watu wale kwa upanga unaotoka ndani ya kinywa changu.


Wale wamalaika wane wakafunguliwa, nao walikuwa wamewekwa tayari kwa saa ile, siku, mwezi na mwaka ule, wapate kuua sehemu moja ya tatu ya wanadamu.


Watu wale hawakuacha hata matendo yao ya uuaji, ya uchawi, ya uasherati na ya wizi.


Samweli akamujibu Saulo: “Umefanya kipumbafu. Haukutii mambo Yawe, Mungu wako, aliyokuamuru. Kama ungetii, Yawe angeudumisha milele ufalme wako juu ya Israeli.


Halafu Samweli akamwambia: “Unazani kwamba Yawe anapendelea zaidi sadaka za kuteketezwa kwa moto na matoleo mengine, kuliko kuitii sauti yake? Hapana. Kumutii yeye ni bora kuliko matoleo na kumusikiliza kuliko kumutolea mafuta ya beberu.


Kisha Samweli akasema: “Muniletee hapa Agagi mufalme wa Waamaleki.” Agagi akamwendea Samweli akiwa mwenye furaha maana alifikiri: “Uchungu wa kifo umepita.”


Samweli akasema: “Kwa sababu upanga wako umewafanya wamama wengi wasikuwe na watoto, ndivyo na mama yako atakavyokuwa bila mutoto kati ya wamama.” Akamukatakata Agagi vipandevipande mbele ya Yawe kule Gilgali.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ