Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 6:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Halafu watasema: Tuende tumurudilie Yawe! Yeye mwenyewe ameturarua, lakini yeye mwenyewe atatuponyosha. Yeye mwenyewe ametuumiza, lakini yeye mwenyewe atatunza vidonda.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 6:1
36 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kwa hiyo wajumbe wakapita katika inchi yote ya Israeli na ya Yuda kwa kupeleka barua zile kufuatana na amri ya mufalme na wakubwa wake. Barua hizo zilikuwa na ujumbe huu: “Enyi watu wa Israeli muliobaki nyuma ya mashambulizi ya wafalme wa Asuria. Mumurudilie Yawe, Mungu wa Abrahamu, Isaka na Israeli, kusudi naye apate kuwarudilia.


Amenirarua kwa hasira na kunichukia, amenisagia meno, na adui yangu ananitonolea macho.


Ukimurudilia Mungu na kunyenyekea, ukiondoa uovu mbali na makao yako,


Kama Mungu akinyamaza, nani anayeweza kumuhukumu? Kama akificha uso wake, nani anayeweza kumwona, ikiwa ni taifa au mutu mumoja?


Maana yeye anaumiza na tena anatunza, anatia kidonda na kwa mukono wake anaponyesha.


Mimi nilipofanikiwa, nilisema: “Sitashindwa hata kidogo!


Ee Yawe, usiniazibu kwa hasira yako, usiniadibishe kwa kasirani yako.


Umeniletea taabu kubwa, lakini utanirudishia tena uzima, wewe utaniinua tena kutoka katika shimo.


wakati wa kuua na wakati wa kuponyesha, wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga,


Siku hiyo, watu watamwangalia Muumba wao, na kuelekeza macho yao kwa huyo Mutakatifu wa Israeli.


watu wengi wataenda kule na kusema, Mukuje tupandie kwenye mulima wa Yawe, tuende kwenye nyumba ya Mungu wa Yakobo, apate kutufundisha njia zake, nasi tutafuata mapito yake. Maana sheria itakuja kutoka Sayuni; neno la Yawe kutoka Yerusalema.


Mutazihesabu sanamu zenu za miungu zilizopakwa feza na zahabu kuwa uchafu. Mutazitupilia mbali kama takataka, mukisema: Mupotelee mbali!


Tena mwezi utawaka kama jua, nao mwangaza wa jua utakuwa mara saba ya mwangaza wake wa kawaida, sawa vile kwamba mwangaza wa siku saba umeangaza katika siku moja. Mambo haya yote yatatukia wakati Yawe atakapofunga vidonda na kuponyesha mapigo aliyowaletea watu wake.


Waovu waache njia zao mbaya, watu wabaya waachane na mawazo yao mabaya; wamurudilie Yawe apate kuwahurumia, wamwendee Mungu wetu maana atawasamehe.


Murudi, enyi watoto musiokuwa na uaminifu, mimi nitawaponyesha ukosefu wenu wa uaminifu. Nanyi munasema: Sisi tunarudi kwako, maana wewe ndiwe Yawe, Mungu wetu.


Yawe anasema hivi: Mapigo yako hayaponi, vidonda vyako haviwezi kutunzwa.


Sasa wanakuita wewe Sayuni: “Aliyetupiliwa”, “Muji usioshugulikiwa na mutu”. Lakini nitakurudishia afya yako, nitaponyesha vidonda vyako. –Ni ujumbe wa Yawe.


Watu watajaribu kupigana na Wakaldea lakini hiyo itakuwa bure, maana mifereji itajaa maiti za watu ambao nitawaua kwa hasira na kasirani yangu. Kwa vile wamefanya uovu huo wote, mimi nitauacha muji huu.


Hata hivyo, mimi nitauponyesha muji huu na kuwapa watu wake afya; nitawajalia ustawi mwingi na usalama.


Siku hizo na wakati huo, watu wa Israeli na watu wa Yuda watakusanyika pamoja na kuja wakilia na kutafuta Yawe, Mungu wao. –Ni ujumbe wa Yawe.


Watauliza njia ya kwenda Sayuni, na nyuso zao zikielekea huko, wakisema: Mukuje! Nao watajiunga na Yawe katika agano la milele ambalo halitasahauliwa hata kidogo.


Alinifukuza katika njia yangu, akanirarua na kuniacha ukiwa.


Watanifuata mimi Yawe ninayenguruma kama simba; nitakaponguruma watanifikia toka magaribi wakitetemeka.


Watu wa Samaria wataazibiwa kwa ajili ya kosa lao; wamemwasi Mungu wao. Watauawa kwa upanga, watoto wao watapondwapondwa, na wamama wenye mimba watapasuliwa tumbo.


Inchi ya Asuria haitatuokoa, hatutategemea tena farasi wa vita. Hatutaziita tena Mungu wetu hizo sanamu tulizochonga. Kwako, ee Mungu, yatima anapata huruma.


Nyuma, Waisraeli watarudi na kumutafuta Yawe, Mungu wao, na kumutafuta mufalme wao, wa uzao wa Daudi. Halafu watamutii Yawe, na kutazamia wema wake siku za mwisho.


Lakini ikiwa kisha kuchunguza nyumba hiyo, kuhani akiona kwamba taka halikuenea kisha kupigwa lipu, basi, kuhani atatangaza kwamba nyumba hiyo ni safi maana taka limekwisha.


Mukusanyike, mukusanyike, enyi taifa la watu wasiokuwa na haya,


Muone kwamba mimi ni Mungu na wala hakuna mwingine isipokuwa mimi. Mimi ninaua na kuweka uzima, ninaumiza na kuponya, na hakuna anayeweza kumwokoa yeyote toka katika mikono yangu.


Yawe anaua na kufufua, yeye anawashusha katika kuzimu naye anawarudisha tena.


Samweli akawaambia Waisraeli: “Kama munamurudilia Yawe kwa moyo wenu wote, basi mutupilie mbali miungu ya kigeni na sanamu za Astaroti. Muelekeze mioyo yenu kwa Yawe, na kumutumikia yeye peke yake; naye atawaokoa kutoka katika mikono ya Wafilistini.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ