Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 5:5 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

5 Kiburi cha Waisraeli kinaonekana wazi; watu wa Efuraimu watajikwaa katika makosa yao, nao watu wa Yuda watajikwaa pamoja nao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 5:5
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Hakika mwovu hataepuka kuazibiwa, lakini wenye haki wataokolewa.


Haki ya watu wakamilifu inanyoosha njia yao, lakini waovu wanaanguka kwa uovu wao wenyewe.


Mwovu anaangamizwa kwa matendo yake maovu, lakini mwenye haki atapata usalama kwa uaminifu wake.


maana mutu wa haki anaanguka mara nyingi naye anainuka tena, lakini mutu mwovu anaangamizwa na hasara.


Kuna watu ambao macho yao yanajaa kiburi. Wanazarau kila kitu wanachoona.


Watu wa Yerusalema wamejikwaa, watu wa Yuda wameanguka, kwa sababu wanamupinga Yawe kwa maneno na matendo, wakizarau utukufu wake kati yao.


Ubaguzi wao unashuhudia juu yao; wanatangaza zambi yao kama vile watu wa Sodoma, wala hawaifichi. Ole kwao watu hao, kwa sababu wamejiletea maangamizi wenyewe.


Watu wote wanaotengeneza sanamu za miungu ni bure kabisa; na vitu hivyo wanavyovifurahia haviwafalii kitu chochote. Wanaoshuhudia hiyo miungu ya uongo ni vipofu na wajinga. Kwa hiyo hao watafezeheshwa!


Makosa yetu mbele yako ni mengi sana, zambi zetu zinashuhudia juu yetu. Kweli, makosa yetu yanaandamana nasi, tunayajua maovu yetu.


Nao watu wanasema: Ingawa zambi zetu zinatoa ushuhuda juu yetu, utusaidie ee Yawe kwa ajili ya heshima ya jina lako. Maasi yetu ni mengi, tumetenda zambi mbele yako.


Uovu wako utakuazibu; na uasi wako utakuhukumu. Ujue na kutambua kwamba ni vibaya sana kuacha Bwana wako Yawe, Mungu wako, na kutokuwa na woga wangu ndani yako. –Ni ujumbe wa Bwana wetu Yawe wa majeshi.–


Watu wa Samaria wataazibiwa kwa ajili ya kosa lao; wamemwasi Mungu wao. Watauawa kwa upanga, watoto wao watapondwapondwa, na wamama wenye mimba watapasuliwa tumbo.


Enyi Waisraeli, mumurudilie Yawe, Mungu wenu. Mumejikwaa kwa sababu ya uovu wenu.


Wewe utajikwaa muchana, naye nabii atajikwaa pamoja nawe usiku. Nitamwangamiza mama yako Israeli.


Maana mimi nitakuwa kama simba kwa Efuraimu, kama simba mukali kwa watu wa Yuda. Mimi mwenyewe nitawararua na kuondoka, nitawakamata na hakuna atakayewaokoa.


Kiburi cha Waisraeli kinawashuhudia wao wenyewe, hawanirudilii mimi Yawe, Mungu wao; wala hawanitafuti kwa ajili ya matukio hayo yote.


Waisraeli wamemusahau Muumba wao, wakajijengea nyumba kubwa; watu wa Yuda wamejiongezea miji yenye kuzungukwa na kuta, lakini mimi nitatuma moto katika miji hiyo, na kuziteketeza kuta zao.


Umeanguka na hautainuka tena ewe binti Israeli! Umeachwa ukiwa katika inchi yako, hakuna hata mutu wa kukuinua.


Hivi munajishuhudia ninyi wenyewe kuwa ninyi ni ukoo wa watu waliowaua manabii.


Yule bwana akamujibu: ‘Wewe mutumishi mubaya! Nitakuhukumu kufuatana na maneno yako. Ulijua kama mimi ni mutu mugumu, ninayetafutia nafasi nisipowekea na kuvuna nafasi nisipopanda.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ