Yawe anasema hivi: Kama nimeachana na mama yako Yerusalema, barua ya kuachana iko wapi? Nilikuwa na deni ya nani kwa kuwauzisha? Mukumbuke kwamba muliuzishwa kwa ajili ya maovu yenu, mama yenu alifukuzwa kwa ajili ya makosa yenu.
Wajane wao wamekuwa wengi kuliko muchanga wa bahari. Nao wamama wenye watoto vijana nimewaletea mwangamizaji muchana kati. Nimesababisha uchungu na vitisho viwapate kwa rafla.
Ujumbe juu ya manabii wasiofaa. Nimevunjika moyo, mifupa yangu yote inatetemeka; nimekuwa kama mulevi, kama mutu anayetabanika na pombe, kwa sababu ya Yawe na maneno yake matakatifu.
lakini inchi yenu ya kuzaliwa itapatishwa haya; hiyo inchi mama yenu, itafezeheshwa. Babeli itakuwa ya mwisho kati ya mataifa, itakuwa mbuga yenye kukauka na jangwa.
Kama sivyo, nitamuvua nguo abaki uchi, nitamufanya akuwe sawa vile alivyozaliwa. Nitamufanya akuwe utupu sawa jangwa, akauke sawa inchi kavu. Nitamwua kwa kiu.
Wakati ule, nitaondoa majina ya sanamu za miungu katika inchi, wala hayatakumbukwa tena. –Ni ujumbe wa Yawe wa majeshi.– Na wanaojidai kuwa manabii nitawaondoa kabisa pamoja na tamaa zao za kuabudu sanamu.