Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 4:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Watu wangu wanaomba shauri kutoka kwa muti; kijiti chao cha kuaguza ndicho kinachowapa shauri. Nia ya kufanya uzinzi imewapotosha; wamefanya uzinzi kwa kufuata miungu mingine, wakaniacha mimi Mungu wao.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 4:12
25 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Haya yote yalitendeka kwa sababu watu wa Israeli walimwasi Yawe, Mungu wao, ambaye aliwatoa kutoka mikono ya mufalme wa Misri, vilevile waliabudu miungu mingine,


Lakini umeifuata mienendo ya wafalme wa Israeli na kuwaongoza watu wa Yuda na wa Yerusalema katika kukosa uaminifu kama vile Ahabu, na wafalme wa jamaa yake waliomufuata walivyoongoza Israeli kukosa uaminifu. Vilevile umewaua wandugu zako, wandugu za baba mumoja waliokuwa watu wema zaidi kuliko wewe.


Hivyo wakajichafua kwa matendo yao, wakakosa uaminifu kwa Mungu kama wazini.


Anayejitenga nawe, hakika ataangamia. Anayekukana, utamwangamiza.


Wote ni wajinga na wapumbafu, fundisho la sanamu hizi ni mazarau matupu!


Wao wanauambia muti: “Wewe ni baba yetu”, nalo jiwe: “Wewe ndiwe uliyetuzaa”; kwa maana unanigeuzia mugongo, wala hawakunielekezea uso. Lakini wakati wa shida wanasema: Simama utuokoe!


Kati ya manabii wa Samaria, nimeona jambo la kuchukiza sana: nao walitabiri kwa jina la mungu Bali na kupotosha watu wangu Waisraeli.


Ninyi munasema ndani ya mioyo yenu: Tutakuwa kama mataifa mengine, kama makabila ya inchi ingine na kuabudu miti na mawe. Hayo munayofikiri ndani ya mioyo yenu hayatafanikiwa hata kidogo.


Ewe upanga, shambulia upande wa kuume, shambulia upande wa kushoto; elekeza chongo yako pande zote.


Muombe huruma kwake, mumurudilie na kumwambia: Utusamehe uovu wote, upokee zawadi zetu, nasi tutakusifu kwa moyo.


Matendo yao yanawazuia wasimurudilie Mungu wao. Wamejaa uzinzi ndani ya mioyo yao; hawanijui mimi Yawe.


Nimeona jambo la kuchukiza sana kati ya Waisraeli: watu wa Efuraimu wanakimbilia miungu mingine, Waisraeli wamejichafua.


Musifurahi enyi Waisraeli! Musishangilie kama watu wa mataifa mengine; maana, mumekuwa wazinzi kwa kumwacha Mungu wenu. Mumefurahia malipo ya uzinzi, kwa kila nafasi ya kupepetea ngano.


Kwa hiyo Waisraeli watakoma kabisa kuwatambikia miungu ya uongo wenye umbo la beberu, jambo ambalo limewafanya wakose uaminifu kwangu. Hili ni sharti la kufuata siku zote katika vizazi vyao vyote.


mimi mwenyewe nitamukasirikia mutu huyu na jamaa yake. Nitawatenga kutoka watu wao, yeye mwenyewe pamoja na wote waliokosa uaminifu kwangu kwa kumwendea mungu Moleki.


Kama mutu angetokea akitangaza maneno matupu ya uongo na kusema “Ninawatabiria divai na pombe kwa wingi”, muhubiri wa namna hiyo angependwa na watu hawa!


Ole wake mutu anayeambia kipande cha muti: Amuka! au jiwe bubu: Simama! Sanamu inaweza kumufundisha mutu? Angalia imepakwa zahabu na feza, lakini haina uzima wowote.


Vishada hivyo vitakuwa ukumbusho kwenu. Kila mara mutakapoviona, mutakumbuka amri zangu zote na kuzifuata, kusudi musifuate mapenzi yenu na yale munayoona kwa macho yenu wenyewe.


Yawe akamwambia Musa: “Umekaribia sasa kuaga dunia, na kisha kufa kwako, watu wataanza kuniacha na kuendea miungu mingine ya inchi hiyo ambamo watakwenda kuishi. Wataniacha na kuvunja agano nililoagana nao.


Nao wakamwambia: “Tafazali utuulizie kwa Yawe kama tutafanikiwa katika safari yetu.”


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ