Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 3:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Yawe akaniambia: Kwenda tena umupende mwanamuke anayependwa na mwanaume mwingine na ambaye ni muzinzi. Umupende kama vile mimi Yawe ninavyowapenda Waisraeli, ingawa wao wanaigeukia miungu mingine na kupenda mikate ya zabibu.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 3:1
34 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

na akawagawanyia watu wote, kundi lote la Waisraeli, wanaume na wanawake, kila mumoja, mukate, kipande cha nyama na mukate wa sadaka. Kisha, watu wote waliondoka, kila mutu akarudi kwake.


Lakini Yawe aliwarehemu na kuwaonea huruma. Aliwaangalia kwa wema kwa sababu ya agano lake na Abrahamu, Isaka na Yakobo. Hakuwaangamiza wala hajawaachilia hata kidogo mpaka leo.


na akawagawanyia Waisraeli wote, wanaume na wanawake, kila mumoja akapewa mukate, kipande cha nyama na mukate wa zabibu.


Hata hivyo, kutokana na rehema zako nyingi, haukuwaachilia waangamie kabisa au kuwatupilia, maana wewe ni Mungu mwenye huruma na rehema.


Kama watumishi wanavyomutegemea bwana wao, kama mujakazi anavyomutegemea bibi mukubwa wake, ndivyo nasi tunavyokutegemea wewe, ee Yawe, Mungu wetu, mpaka hapo utakapotuonea huruma.


Kesho yake watu wakaamuka mapema wakatoa sadaka za kuteketezwa na sadaka za amani. Watu wakaikaa chini kwa kula na kunywa, kisha wakasimama na kucheza.


Munishibishe na zabibu kavu, munifurahishe kwa matunda, maana ninaugua kwa mapenzi!


Munigeukie mimi mupate kuokolewa, popote munapokuwa katika dunia. Maana mimi ni Mungu, wala hakuna mwingine.


Lakini kama muke asiyekuwa mwaminifu anavyomwacha mume wake, ndivyo ulivyokosa uaminifu kwangu. –Ni ujumbe wa Yawe.


Efuraimu ni mwana wangu mupendwa; yeye ni mutoto wangu ninayemupenda sana. Ndiyo maana kila mara ninapomutisha, ninaendelea kumukumbuka. Moyo wangu unamwelekea kwa wema; hakika nitamuhurumia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Ewe Efuraimu, ninaweza kukuacha namna gani? Ninaweza kukutupilia, ewe Israeli namna gani? Nitaweza namna gani kukufanya kama muji wa Adama? Nitaweza namna gani kukutendea kama Zeboimu! Ninazuizwa na moyo wangu; huruma yangu imezidi kuwa motomoto.


Kama sivyo, nitamuvua nguo abaki uchi, nitamufanya akuwe sawa vile alivyozaliwa. Nitamufanya akuwe utupu sawa jangwa, akauke sawa inchi kavu. Nitamwua kwa kiu.


Uasherati, divai mupya na ya zamani vinaondoa maarifa.


Kwenye sikukuu ya mufalme, waliwalewesha sana wakubwa wake; naye mufalme akashirikiana na watu wa ovyoovyo.


Juu ya kila mazabahu, watu wanalalia nguo walizozitwaa kwa masikini kama rehani ya madeni yao; na katika nyumba ya Mungu wao, wanakunywa divai waliyotwaa kwa wenye kuwa na madeni yao.


Munakunywa divai katika mabakuli, na kujipakaa marasi mazuri kabisa. Lakini hamuhuzuniki hata kidogo juu ya kuangamia kwa wazao wa Yosefu.


Lakini mimi ninamutumainia Yawe, ninamutazamia Mungu mwenye kuniokoa; Mungu wangu atanisikiliza.


Kwa hiyo, Yawe anasema hivi: Ninarudilia Yerusalema kwa huruma; humo itajengwa nyumba yangu, na ujenzi mupya wa muji utaanza. –Ni Yawe ya majeshi anayesema.


Lakini Yesu akamwambia: “Rafiki, ufanye lililokuleta.” Halafu watu wale wakajongea na kumukamata Yesu na kumufunga.


Hamuwezi kuchangia kikombe cha Bwana na kikombe cha pepo. Vilevile hamuwezi kuchangia meza ya Bwana na meza ya pepo.


Basi musikuwe wenye kuabudu sanamu kama wamoja kati yao walivyokuwa; kama vile Maandiko haya Matakatifu yanavyosema: “Watu wakaikaa kula na kunywa na kisha wakasimama kwa kujifurahisha.”


Kufuatana na hiyo, zamani mulipitisha siku nyingi mukifanya matendo yanayolingana na ya wapagani. Mulizoea kuishi katika uasherati, tamaa mbaya, ulevi, karamu za ulafi, za ulevi na kuabudu sanamu.


Kisha wakaitupilia mbali miungu ya kigeni, wakamutumikia tena Yawe. Yawe hakuweza kuvumilia zaidi kuona taabu za Waisraeli.


Wakatoka na kwenda kwenye mashamba yao ya mizabibu, wakachuma zabibu halafu wakazikamua, wakatengeneza divai wakafanya sikukuu. Wakaingia kwenye nyumba ya mungu wao wakakula na kunywa, kisha wakamutukana Abimeleki.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ