Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 2:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Mumushitaki mama yenu, mumushitaki, maana sasa yeye si muke wangu wala mimi si mume wake. Mumushitaki aondoe vitambulisho vya uasherati juu ya uso wake, ajiepushe na mapambo ya uzinzi juu ya kifua chake.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 2:4
17 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Wakati Yoramu alipomwona Yehu, alimwuliza: “Yehu, unakuja kwa amani?” Yehu akamujibu: “Amani gani, wakati makahaba na wachawi wa Yezebeli ni wengi?”


Matawi ya miti yamekauka na kuvunjika; wanawake wanayaokota na kuyawasha moto. Watu hawa hawajaelewa kitu, kwa hiyo Mungu, Muumba wao, hatawahurumia, yeye aliyewafanya, hatawatendea mema.


Yawe anasema hivi: Kama nimeachana na mama yako Yerusalema, barua ya kuachana iko wapi? Nilikuwa na deni ya nani kwa kuwauzisha? Mukumbuke kwamba muliuzishwa kwa ajili ya maovu yenu, mama yenu alifukuzwa kwa ajili ya makosa yenu.


Lakini Yawe anasema: Mukuje hapa ninyi wana wa wake wachawi; ninyi wazao wa wachawi, wazinzi na makahaba.


Nitawagonganisha wao kwa wao hata baba na watoto. –Ni ujumbe wa Yawe.– Sitawahurumia, sitawaachilia wala sitawarehemu, mpaka nitakapowaangamiza.


Yawe anasema hivi: Usiingie katika nyumba yenye kilio wala usiende kuomboleza wala kuwalilia. Kwa maana sitawapatia watu hawa amani tena. Sitawatendea tena mema wala kuwasikilia huruma. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Nami nitakuelekezea kasirani yangu, nao watakutendea kwa hasira kali. Watakukata pua na masikio na watu wako watakaobaki watauawa kwa upanga. Watawatwaa wana na wabinti zako, na watu wako watakaobaki watateketezwa kwa moto.


Kwa sababu ya mambo hayo watasikia uzito wa kasirani yangu. Sitamwacha hata mutu mumoja aponyoke wala sitamwonea huruma mutu yeyote. Hata wakinililia kwa sauti kubwa mimi sitawasikiliza.


Kwa upande wangu, sitawaachilia wala kuwahurumia; nitawatendea kufuatana na matendo yao.


Yawe alipoanza kusema na Waisraeli kwa njia ya Hosea, alimwambia hivi: Kwenda kuoa mwanamuke muzinzi, uzae naye watoto wa uzinzi, maana watu wa inchi hii wanafanya uzinzi mwingi kwa kuniacha mimi.


Gomeri alipata mimba tena, akazaa mutoto mwanamuke. Yawe akamwambia Hosea: Umupange mutoto huyo jina la “Asiyehurumiwa”, maana sitawahurumia tena Waisraeli wala sitawasamehe.


Wamevunja uaminifu kwa Yawe, wamezaa watoto wa haramu. Mwezi mumoja utatosha kwa kuwaangamiza, pamoja na mashamba yao.


Halafu yule malaika wa Yawe akasema: Ee Yawe wa majeshi, kwa muda gani utaendelea kutokuwa na huruma juu ya muji Yerusalema na miji ya inchi ya Yuda ambayo umeikasirikia kwa muda wa miaka makumi saba?


Ninyi munafanya matendo yale baba yenu anayofanya.” Wakamujibu: “Sisi si watoto wa haramu. Tuko na baba mumoja, naye ndiye Mungu.”


Basi ufikiri juu ya wema wa Mungu na ukali wake vilevile. Yeye ni mukali kwa wale walioanguka, lakini yeye ni mwema kwako, ikiwa utaendelea katika wema wake. Kama si vile, wewe vilevile utakatwa.


Basi ni kusema kwamba Mungu anamuhurumia yule anayetaka, na kumufanya mugumu yule anayetaka.


Kwa sababu Mungu hatahurumia mutu yule asiyehurumia wengine. Lakini huruma ya Mungu itaishinda hukumu.


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ