Biblia Todo Logo
အွန်လိုင်း သမ္မာကျမ်းစာ

- ကြော်ငြာတွေ -




Hosea 2:21 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

21 Nitakufanya muke wangu milele; ukuwe wangu kwa sheria na haki, kwa wema na huruma.

အခန်းကိုကြည့်ပါ။ ကော်ပီ




Hosea 2:21
15 ပူးပေါင်းရင်းမြစ်များ  

Kama vile mvua na teluji inavyoshuka toka mbinguni, wala hairudi kule lakini inalowanisha udongo, kuuzalisha na kuchipukiza mimea, na kumupatia mupandaji mbegu na kuwapa watu chakula,


Hautaitwa tena: Aliyeachwa, wala inchi yako haitaitwa: “Ukiwa”. Lakini utaitwa: “Ninamufurahia”, na inchi yako itaitwa: “Aliyeolewa”. Maana Yawe amependezwa nawe, naye atakuwa kama mume wa inchi yako.


Maana kama vile kijana mwanaume anavyomwoa binti, ndivyo aliyekujenga atakavyokuwa mume wako. Kama bwana arusi anavyofurahi juu ya bibi arusi, ndivyo Mungu atakavyofurahi juu yako.


Hata mbele hawajaniita, mimi nitawaitikia; mbele hawajamaliza kusema, nitakuwa nimewajibu.


Nitawaokoa kutoka uchafu wenu wote. Nitaiamuru ngano iongezeke, wala sitawaletea njaa tena.


Vichipukizi vyao vitazaa sana, uzuri wao utakuwa kama mizeituni, harufu yao nzuri kama maua ya Lebanoni.


Alisikiliza, akajibu maombi yao, akasema: Sasa nitawapa tena ngano, divai na mafuta, nanyi mutashiba navyo. Sitawafanya muzarauliwe tena na mataifa.


Sehemu hiyo moja ya tatu itakayobaki, nitaipima na kuitakasa, kama vile mutu anavyosafisha feza, kama vile wanavyopima zahabu. Halafu wao wataniomba mimi, nami nitawajibu. Nitasema: Hawa ni watu wangu, nao watasema: Yawe, ndiye Mungu wetu.


Sasa nitaleta tena amani katika dunia, mvua itanyesha kama kawaida, udongo utatoa mazao, na mizabibu itazaa kwa wingi. Nitawapa watu wanaobaki wa taifa hili yale yote yakuwe mali yao.


na kuwafanya wakae katika Yerusalema. Wao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao; nitatawala juu yao kwa uaminifu na haki.


Mulete katika gala yangu zaka yote, kusudi katika nyumba yangu kuwe chakula cha kutosha. Kisha munaweza kunijaribu. Munipime namna hiyo nanyi mutaona kama sitayafungua madirisha ya mbinguni na kuwatiririshia baraka tele.


Wadudu waharibifu nitawazuia wasiyaharibu tena mazao yenu. Mizabibu yenu katika mashamba haitaacha kuzaa matunda.


Lakini ninyi mushugulikie kwanza Ufalme wa Mungu na kufuata haki mbele yake, naye atawaongezea vitu vile vyote.


Yeye hakumwacha Mwana wake wa pekee, lakini alimutoa kwa ajili yetu sisi wote. Namna gani atakosa kutupatia vilevile vitu vyote kwa njia ya mwana wake?


ကြှနျုပျတို့နောကျလိုကျပါ:

ကြော်ငြာတွေ


ကြော်ငြာတွေ